< Isaya 58 >

1 “Piga kelele, usizuie. Paza sauti yako kama tarumbeta. Watangazieni watu wangu uasi wao, na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao.
Cry aloud, spare not, Lift up thy voice like a trumpet, And show my people their transgression, And the house of Jacob their sins!
2 Kwa maana kila siku hunitafuta, wanaonekana kutaka kujua njia zangu, kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa, na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake. Hutaka kwangu maamuzi ya haki, nao hutamani Mungu awakaribie.
Yet they seek me daily, And desire to know my ways, As a nation that hath done righteousness, And hath not forsaken the ordinances of their God; They inquire of me concerning the judgments which bring salvation; They long for the coming of God.
3 Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona? Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’ “Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote.
“Wherefore do we fast, and thou seest not? Wherefore do we afflict our souls, and thou dost not regard it?” Behold, in the day of your fasts ye pursue your pleasure, And exact all your labors.
4 Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano, na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu. Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu.
Behold, ye fast in strife and contention, And smiting with the fist of wickedness. Ye do not fast now So that your voice shall be heard on high.
5 Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua, siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza? Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete, na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu? Je, huo ndio mnaouita mfungo, siku iliyokubalika kwa Bwana?
Is this the fast that I approve, A day for a man to afflict his soul? Is it that he should bow down his head like a bulrush, And lie down in sackcloth and ashes? Wilt thou call this a fast, And a day acceptable to Jehovah?
6 “Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua: kufungua minyororo ya udhalimu, na kufungua kamba za nira, kuwaweka huru walioonewa, na kuvunja kila nira?
Is not this the fast that I approve, —To loose the bands of wickedness, To undo the heavy burdens, To let the oppressed go free, And to break in pieces every yoke?
7 Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi, unapomwona aliye uchi, umvike, wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe?
Is it not to break thy bread to the hungry, And to bring the poor, that are cast out, to thy house? When thou seest the naked, that thou clothe him, And that thou hide not thyself from thine own flesh?
8 Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko na uponyaji wako utatokea upesi; ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako, na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako.
Then shall thy light break forth like the morning, And thy health shall spring forth speedily; Thy salvation shall go before thee, And the glory of Jehovah shall bring up thy rear.
9 Ndipo utaita, naye Bwana atajibu, utalia kuomba msaada, naye atasema: Mimi hapa. “Kama ukiiondoa nira ya udhalimu, na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu,
Then shalt thou call, and Jehovah will answer; Thou shalt cry, and he shall say, Lo, here I am! If thou remove from the midst of thee the yoke, The pointing of the finger, and the injurious speech.
10 nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu na kutosheleza mahitaji ya walioonewa, ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani, nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.
If thou bring forth thy bread to the hungry, And satisfy the afflicted soul, Then in obscurity shall light arise to thee; Yea, thy darkness shall become as noonday;
11 Bwana atakuongoza siku zote, atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame, naye ataitia nguvu mifupa yako. Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri, kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.
Jehovah shall lead thee continually, And satisfy thee in the time of drought, And strengthen thy bones; Thou shalt be like a watered garden, and a spring of water, Whose waters never fail.
12 Watu wako watajenga tena magofu ya zamani na kuinua misingi ya kale; utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka, Mwenye Kurejeza Barabara za Makao.
Thy people shall build the ancient desolations, The ruins of many generations shall they restore; Thou shalt be called the repairer of the breach, The restorer of ways for inhabitants.
13 “Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato, na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu, kama ukiita Sabato siku ya furaha na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa, kama utaiheshimu kwa kutoenenda katika njia zako mwenyewe, na kutokufanya yakupendezayo au kusema maneno ya upuzi,
If thou restrain thy foot from the sabbath, From doing thy pleasure on my holy day, If thou shalt call the sabbath a delight, The holy day of Jehovah honorable, And shalt honor it by refraining from thy work, From doing thy pleasure, and speaking vain words,
14 ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana, nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.” Kinywa cha Bwana kimenena haya.
Then shalt thou delight thyself in Jehovah. And I will cause thee to ride upon the high places of the earth, And cause thee to enjoy the inheritance of Jacob, thy father; For the mouth of Jehovah hath spoken it.

< Isaya 58 >