< Isaya 57 >
1 Mwenye haki hupotea, wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake; watu wanaomcha Mungu huondolewa, wala hakuna hata mmoja anayeelewa kuwa wenye haki wameondolewa ili wasipatikane na maovu.
Le juste périt, et il n’est personne qui y pense en son cœur; les hommes de miséricorde sont enlevés du monde, parce qu’il n’est personne qui ait de l’intelligence; car c’est à cause de la malice qu’a été enlevé le juste.
2 Wale waendao kwa unyofu huwa na amani; hupata pumziko walalapo mautini.
Vienne la paix; qu’il repose sur sa couche, celui qui a marché dans sa ligne droite.
3 “Lakini ninyi: Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi, ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!
Mais vous, approchez ici, fils d’une devineresse, race d’un adultère et d’une prostituée.
4 Mnamdhihaki nani? Ni nani mnayemcheka kwa dharau, na kumtolea ndimi zenu? Je, ninyi si watoto wa waasi, uzao wa waongo?
De qui vous êtes-vous joués? contre qui avez-vous ouvert la bouche et tiré la langue? Est-ce que vous n’êtes pas, vous, des fils criminels, une race mensongère?
5 Mnawaka tamaa katikati ya mialoni na chini ya kila mti uliotanda matawi; mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde na chini ya majabali yenye mianya.
Vous qui vous consolez dans vos dieux, sous tout arbre feuillu; immolant vos enfants dans les torrents, sous les pierres avancées?
6 “Sanamu zilizo katikati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu; hizo ndizo sehemu yenu. Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji, na kutoa sadaka za nafaka. Katika haya yote, niendelee kuona huruma?
Dans les parties d’un torrent est ta part; c’est là ton sort; et tu y as répandu une libation, tu as offert un sacrifice. Est-ce que de cela je ne serai pas indigné?
7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.
Sur une montagne haute et élevée, tu as posé ton lit; tu y es montée afin d’immoler des hosties.
8 Nyuma ya milango yako na miimo yako umeweka alama zako za kipagani. Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako, umepanda juu yake na kukipanua sana; ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao, nawe uliangalia uchi wao.
Et derrière la porte, et en arrière du poteau tu as placé ton souvenir; parce que près de moi tu as découvert ta couche, et tu as reçu des adultères; tu as agrandi ton lit et tu as fait avec eux une alliance; tu as aimé leur couche à main ouverte.
9 Ulikwenda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe! (Sheol )
Et tu t’es parée d’un parfum royal, et tu as multiplié tes essences. Tu as envoyé des messagers au loin, et tu as été abaissée jusqu’aux enfers. (Sheol )
10 Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote, lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’ Ulipata uhuisho wa nguvu zako, kwa sababu hiyo hukuzimia.
Dans la multitude de les voies, tu t’es fatiguée, tu n’as pas dit: Je me reposerai. Tu as trouvé la vie de ta main, à cause de cela tu ne m’as pas prié.
11 “Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa hata ukawa mwongo kwangu, wala hukunikumbuka au kutafakari hili moyoni mwako? Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu hata huniogopi?
Qui t’a rendue inquiète, qui as-tu craint, après que tu as menti, que tu ne t’es pas souvenue de moi, tu n’as pas pensé en ton cœur? C’est parce que je me tais, et que je suis comme ne voyant pas, que tu m’as oublié.
12 Nitaifunua haki yako na matendo yako, nayo hayatakufaidi.
Pour moi j’annoncerai ta justice, et tes œuvres ne te serviront pas.
13 Utakapolia kwa kuhitaji msaada, sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe! Upepo utazipeperusha zote, pumzi peke yake itazipeperusha, Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake, atairithi nchi na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”
Lorsque tu crieras, qu’ils te délivrent ceux que tu as rassemblés, et un vent les emportera, une brise les enlèvera. Mais celui qui a confiance en moi héritera de la terre, et il possédera ma montagne sainte.
14 Tena itasemwa: “Jengeni, jengeni, itengenezeni njia! Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”
Et je dirai: Faites une voie, préparez un chemin, détournez-vous du sentier, ôtez les pierres d’achoppement de la voie de mon peuple.
15 Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana, yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu: “Ninaishi mimi mahali palipoinuka na patakatifu, lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu na kuihuisha mioyo yao waliotubu.
Parce que voici ce que dit le Très-Haut, le sublime, qui habite l’éternité, et dont le nom est saint, et qui habite dans un lieu très élevé, et dans un lieu saint, et avec un coeur contrit et un esprit humble, afin de vivifier l’esprit des humbles et le cœur des contrits.
16 Sitaendelea kulaumu milele, wala sitakasirika siku zote, kwa kuwa roho ya mwanadamu ingezimia mbele zangu: yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.
Car je ne disputerai pas éternellement, et je ne me mettrai pas en colère pour toujours: parce qu’un esprit sortira de ma face, et que je créerai des souffles de vie.
17 Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi; nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira, na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.
À cause de l’iniquité de son avarice, j’ai été irrité, et je l’ai frappé; je t’ai caché ma face, et j’ai été indigné; et il est allé, vagabond, dans la voie de son cœur.
18 Nimeziona njia zake, lakini nitamponya, nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,
Ses voies, je les ai vues, et je l’ai guéri, et je l’ai ramené, et je lui ai rendu des consolations, à lui et à ceux qui le pleuraient.
19 nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji katika Israeli. Amani, amani, kwa wale walio mbali na kwa wale walio karibu,” asema Bwana. “Nami nitawaponya.”
J’ai créé un fruit de lèvres, paix, paix pour celui qui est loin, et pour celui qui est proche, dit le Seigneur, et je les ai guéris.
20 Bali waovu ni kama bahari ichafukayo, ambayo haiwezi kutulia, mawimbi yake hutupa takataka na matope.
Mais les impies sont comme une mer impétueuse qui ne peut s’apaiser, et dont les îlots rejettent de l’écume et du limon.
21 Mungu wangu asema, “Hakuna amani kwa waovu.”
Il n’est pas de paix pour les impies, dit le Seigneur Dieu.