< Isaya 57 >
1 Mwenye haki hupotea, wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake; watu wanaomcha Mungu huondolewa, wala hakuna hata mmoja anayeelewa kuwa wenye haki wameondolewa ili wasipatikane na maovu.
The righteous man perisheth, and no one layeth it to heart; And pious men are taken away, and none considereth That because of the evil the righteous man is taken away.
2 Wale waendao kwa unyofu huwa na amani; hupata pumziko walalapo mautini.
He entereth into peace; He resteth in his bed, Every one that walketh in uprightness.
3 “Lakini ninyi: Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi, ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!
But draw near hither, ye sons of the sorceress, Ye brood of the adulterer and the harlot!
4 Mnamdhihaki nani? Ni nani mnayemcheka kwa dharau, na kumtolea ndimi zenu? Je, ninyi si watoto wa waasi, uzao wa waongo?
Of whom do ye make your sport, And at whom do ye make wide the mouth, And draw out the tongue? Are ye not rebellious children, a treacherous brood?
5 Mnawaka tamaa katikati ya mialoni na chini ya kila mti uliotanda matawi; mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde na chini ya majabali yenye mianya.
Burning with lust for idols Under every green tree, Slaying children in the valleys, Under the clefts of the rocks?
6 “Sanamu zilizo katikati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu; hizo ndizo sehemu yenu. Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji, na kutoa sadaka za nafaka. Katika haya yote, niendelee kuona huruma?
With the smooth stones of the valley is thy portion; These, these are thy lot; Here thou pourest out thy drink-offering, And presentest thy meat-offering; Can I see such things, and be at rest?
7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.
Upon a high and lofty mountain settest thou thy bed; Thither dost thou go up to offer sacrifice;
8 Nyuma ya milango yako na miimo yako umeweka alama zako za kipagani. Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako, umepanda juu yake na kukipanua sana; ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao, nawe uliangalia uchi wao.
Behind the doors and the posts dost thou place thy memorial; Thou departest from me, and uncoverest, and ascendest, and enlargest thy bed. Thou makest an agreement with them; Thou desirest their bed; Thou choosest a place.
9 Ulikwenda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe! (Sheol )
Thou goest to the king with oil, And takest much precious perfume; Thou sendest thine ambassadors afar, Yea, down to the under-world. (Sheol )
10 Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote, lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’ Ulipata uhuisho wa nguvu zako, kwa sababu hiyo hukuzimia.
In the length of thy journeys thou hast wearied thyself, But thou sayest not, “I will desist”; Thou yet findest life in thy hand, Therefore thou art not discouraged.
11 “Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa hata ukawa mwongo kwangu, wala hukunikumbuka au kutafakari hili moyoni mwako? Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu hata huniogopi?
On account of whom art thou anxious, and of whom art thou afraid, that thou hast proved false, And hast not remembered me, nor laid it to heart? Behold, I have been silent a long time; Therefore thou fearest me not.
12 Nitaifunua haki yako na matendo yako, nayo hayatakufaidi.
But now I announce thy deliverance, And thy works do not profit thee.
13 Utakapolia kwa kuhitaji msaada, sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe! Upepo utazipeperusha zote, pumzi peke yake itazipeperusha, Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake, atairithi nchi na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”
When thou criest, let thy host of idols deliver thee! But the wind shall bear them all away; A breath shall take them off; But he that putteth his trust in me Shall possess the land, And shall inherit my holy mountain.
14 Tena itasemwa: “Jengeni, jengeni, itengenezeni njia! Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”
Men shall say, Cast up, cast up, prepare the road; Remove every obstruction from the way of my people!
15 Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana, yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu: “Ninaishi mimi mahali palipoinuka na patakatifu, lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu na kuihuisha mioyo yao waliotubu.
For thus saith the high and lofty One That inhabiteth eternity, whose name is Holy: I dwell in the high and holy place; With him also that is of a contrite and humble spirit; To revive the spirit of the humble, And to revive the heart of the contrite ones.
16 Sitaendelea kulaumu milele, wala sitakasirika siku zote, kwa kuwa roho ya mwanadamu ingezimia mbele zangu: yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.
For I will not contend forever, Nor will I be always angry; For life would fail before me, And the souls which I created.
17 Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi; nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira, na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.
For the guilt of his covetousness I was angry; I smote him, I hid myself, and was angry; But yet he went on perversely in the way of his heart.
18 Nimeziona njia zake, lakini nitamponya, nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,
I have seen his ways, yet will I heal him; I will guide him, and I will restore comfort To him and to his mourners;
19 nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji katika Israeli. Amani, amani, kwa wale walio mbali na kwa wale walio karibu,” asema Bwana. “Nami nitawaponya.”
I create the fruit of the lips. Peace, peace to him that is far off, and to him that is nigh, Saith Jehovah; I will heal him.
20 Bali waovu ni kama bahari ichafukayo, ambayo haiwezi kutulia, mawimbi yake hutupa takataka na matope.
But the wicked is like the troubled sea, Which cannot rest, Whose waters cast up mire and dirt.
21 Mungu wangu asema, “Hakuna amani kwa waovu.”
There is no peace, saith my God, for the wicked.