< Isaya 53 >

1 Ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?
Któż uwierzył naszemu głoszeniu, a komu jest objawione ramię PANA?
2 Alikua mbele yake kama mche mwororo na kama mzizi katika nchi kavu. Hakuwa na uzuri wala utukufu wa kutuvutia kwake, hakuwa na chochote katika sura yake cha kutufanya tumtamani.
Wyrósł bowiem przed nim jak latorośl i jak korzeń z suchej ziemi. Nie miał kształtu ani urody; i gdy widzieliśmy go, nie było wyglądu, który by się nam podobał.
3 Alidharauliwa na kukataliwa na wanadamu, mtu wa huzuni nyingi, ajuaye mateso. Kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, alidharauliwa, wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Wzgardzony i odrzucony przez ludzi; mąż boleści i doświadczony cierpieniem. I przed nim ukrywaliśmy jakby swoją twarz; wzgardzony tak, że mieliśmy go za nic.
4 Hakika alichukua udhaifu wetu na akajitwika huzuni zetu, hata hivyo tulidhania kuwa amepigwa na Mungu, akapigwa sana naye, na kuteswa.
Zaprawdę on wziął na siebie nasze cierpienia i nosił naszą boleść. A my uważaliśmy, że jest zraniony, uderzony przez Boga i utrapiony.
5 Lakini alitobolewa kwa ajili ya makosa yetu, alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu; adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake, na kwa majeraha yake sisi tumepona.
Lecz on był zraniony za nasze występki, starty za nasze nieprawości. Kara dla naszego pokoju była na nim, a jego ranami zostaliśmy uzdrowieni.
6 Sisi sote, kama kondoo, tumepotea, kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe, naye Bwana aliweka juu yake maovu yetu sisi sote.
Wszyscy jak owce zbłądziliśmy, każdy z nas zboczył na swą drogę, a PAN włożył na niego nieprawość nas wszystkich.
7 Alionewa na kuteswa, hata hivyo hakufungua kinywa chake; aliongozwa kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, kama vile kondoo anyamazavyo mbele ya wao wamkataye manyoya, hivyo hakufungua kinywa chake.
Uciśniony i gnębiony, ale nie otworzył swoich ust. Jak baranek na rzeź prowadzony i jak owca przed tymi, którzy ją strzygą, zamilkł i nie otworzył swoich ust.
8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa. Nani awezaye kueleza kuhusu kizazi chake? Kwa maana alikatiliwa mbali na nchi ya walio hai, alipigwa kwa ajili ya makosa ya watu wangu.
Został zabrany z więzienia i z sądu. Kto wypowie jego pokolenie? Został bowiem wyrwany z ziemi żyjących i zraniony za przestępstwo mojego ludu.
9 Wakamfanyia kaburi pamoja na waovu, pamoja na matajiri katika kifo chake, ingawa hakutenda jeuri, wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
I wyznaczono mu grób z niegodziwcami, a z bogaczami była jego śmierć, choć nieprawości nie uczynił ani nie znaleziono fałszu w jego ustach.
10 Lakini yalikuwa ni mapenzi ya Bwana kumchubua na kumsababisha ateseke. Ingawa Bwana amefanya maisha yake kuwa sadaka ya hatia, ataona uzao wake na kuishi siku nyingi, nayo mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake.
Lecz spodobało się PANU zetrzeć go i zgnębić. A po złożeniu swojej duszy na ofiarę za grzech, ujrzy swoje potomstwo, przedłuży swoje dni i to, co się podoba PANU, przez jego rękę szczęśliwie się spełni.
11 Baada ya maumivu ya nafsi yake, ataona nuru ya uzima na kuridhika; kwa maarifa yake, mtumishi wangu mwenye haki atawafanya wengi kuwa wenye haki, naye atayachukua maovu yao.
Z udręki swojej duszy ujrzy [owoc] i nasyci się. Mój sprawiedliwy sługa swoim poznaniem usprawiedliwi wielu, bo sam poniesie ich nieprawości.
12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu miongoni mwa wakuu, naye atagawana nyara pamoja na wenye nguvu, kwa sababu aliyamimina maisha yake hadi mauti, naye alihesabiwa pamoja na wakosaji. Kwa kuwa alichukua dhambi za wengi, na kuwaombea wakosaji.
Dlatego dam mu dział wśród wielkich, aby dzielił się zdobyczami z mocarzami, ponieważ wylał swoją duszę na śmierć. Został zaliczony do przestępców, sam poniósł grzech wielu i wstawił się za przestępcami.

< Isaya 53 >