< Isaya 53 >

1 Ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?
Qui a cru à ce qu’il a entendu de nous? et à qui le bras du Seigneur a-t-il été révélé?
2 Alikua mbele yake kama mche mwororo na kama mzizi katika nchi kavu. Hakuwa na uzuri wala utukufu wa kutuvutia kwake, hakuwa na chochote katika sura yake cha kutufanya tumtamani.
Et il montera comme une branche menue devant lui, et comme un rejeton d’une terre altérée; il n’a ni éclat ni beauté; et nous l’avons vu, et il n’avait pas un aspect agréable, et nous l’avons désiré;
3 Alidharauliwa na kukataliwa na wanadamu, mtu wa huzuni nyingi, ajuaye mateso. Kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, alidharauliwa, wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Méprisé, et le dernier des hommes, homme de douleur, et connaissant l’infirmité; son visage était comme caché, et méprisé, et nous l’avons compté pour rien.
4 Hakika alichukua udhaifu wetu na akajitwika huzuni zetu, hata hivyo tulidhania kuwa amepigwa na Mungu, akapigwa sana naye, na kuteswa.
Il a vraiment lui-même pris nos langueurs sur lui, et il a lui-même porté nos douleurs; et nous l’avons considéré comme un lépreux, frappé de Dieu et humilié.
5 Lakini alitobolewa kwa ajili ya makosa yetu, alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu; adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake, na kwa majeraha yake sisi tumepona.
Mais lui-même il a été blessé à cause de nos iniquités, il a été brisé à cause de nos crimes; le châtiment, prix de notre paix, est tombé sur lui; et par ses meurtrissures nous avons été guéris.
6 Sisi sote, kama kondoo, tumepotea, kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe, naye Bwana aliweka juu yake maovu yetu sisi sote.
Nous tous, comme des brebis, nous avons erré; chacun s’est détourné vers sa voie; et le Seigneur a mis sur lui l’iniquité de nous tous.
7 Alionewa na kuteswa, hata hivyo hakufungua kinywa chake; aliongozwa kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, kama vile kondoo anyamazavyo mbele ya wao wamkataye manyoya, hivyo hakufungua kinywa chake.
Il a été offert parce que lui-même l’a voulu, et il n’a pas ouvert sa bouche; comme une brebis, il sera conduit à la tuerie, et comme un agneau devant celui qui le tond, il sera muet, et il n’ouvrira pas sa bouche.
8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa. Nani awezaye kueleza kuhusu kizazi chake? Kwa maana alikatiliwa mbali na nchi ya walio hai, alipigwa kwa ajili ya makosa ya watu wangu.
À la suite des angoisses et d’un jugement il a été enlevé; qui racontera sa génération? car il a été retranché de la terre des vivants; à cause du crime de mon peuple, je l’ai frappé.
9 Wakamfanyia kaburi pamoja na waovu, pamoja na matajiri katika kifo chake, ingawa hakutenda jeuri, wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
Et il donnera des impies pour sa sépulture, et un riche pour sa mort, parce qu’il n’a pas commis d’iniquité, et que la tromperie n’a pas été dans sa bouche.
10 Lakini yalikuwa ni mapenzi ya Bwana kumchubua na kumsababisha ateseke. Ingawa Bwana amefanya maisha yake kuwa sadaka ya hatia, ataona uzao wake na kuishi siku nyingi, nayo mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake.
Mais le Seigneur a voulu le briser dans son infirmité; s’il donne, pour le péché, son âme, il verra une race de longue durée, et la volonté du Seigneur, par sa main, sera dirigée.
11 Baada ya maumivu ya nafsi yake, ataona nuru ya uzima na kuridhika; kwa maarifa yake, mtumishi wangu mwenye haki atawafanya wengi kuwa wenye haki, naye atayachukua maovu yao.
De ce que son âme a souffert, il verra le fruit, et il sera rassasié; par sa science mon serviteur justifiera lui-même un grand nombre d’hommes, et leurs iniquités, lui-même les portera.
12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu miongoni mwa wakuu, naye atagawana nyara pamoja na wenye nguvu, kwa sababu aliyamimina maisha yake hadi mauti, naye alihesabiwa pamoja na wakosaji. Kwa kuwa alichukua dhambi za wengi, na kuwaombea wakosaji.
C’est pour cela que je lui départirai un très grand nombre d’hommes, et il distribuera les dépouilles des forts, parce qu’il a livré à la mort son âme, et qu’il a été compté parmi les scélérats; parce qu’il a porté les péchés d’un grand nombre, et qu’il a prié pour les transgresseurs.

< Isaya 53 >