< Isaya 53 >
1 Ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?
Who bileuyde to oure heryng? and to whom is the arm of the Lord schewide?
2 Alikua mbele yake kama mche mwororo na kama mzizi katika nchi kavu. Hakuwa na uzuri wala utukufu wa kutuvutia kwake, hakuwa na chochote katika sura yake cha kutufanya tumtamani.
And he schal stie as a yerde bifore hym, and as a roote fro thirsti lond. And nether schap nether fairnesse was to hym; and we sien hym, and no biholdyng was;
3 Alidharauliwa na kukataliwa na wanadamu, mtu wa huzuni nyingi, ajuaye mateso. Kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, alidharauliwa, wala hatukumhesabu kuwa kitu.
and we desiriden hym, dispisid, and the laste of men, a man of sorewis, and knowynge sikenesse. And his cheer was as hid and dispisid; wherfor and we arettiden not hym.
4 Hakika alichukua udhaifu wetu na akajitwika huzuni zetu, hata hivyo tulidhania kuwa amepigwa na Mungu, akapigwa sana naye, na kuteswa.
Verili he suffride oure sikenessis, and he bar oure sorewis; and we arettiden hym as a mesel, and smytun of God, and maad low.
5 Lakini alitobolewa kwa ajili ya makosa yetu, alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu; adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake, na kwa majeraha yake sisi tumepona.
Forsothe he was woundid for oure wickidnessis, he was defoulid for oure greet trespassis; the lernyng of oure pees was on hym, and we ben maad hool bi his wannesse.
6 Sisi sote, kama kondoo, tumepotea, kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe, naye Bwana aliweka juu yake maovu yetu sisi sote.
Alle we erriden as scheep, ech man bowide in to his owne weie, and the Lord puttide in hym the wickidnesse of vs alle.
7 Alionewa na kuteswa, hata hivyo hakufungua kinywa chake; aliongozwa kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, kama vile kondoo anyamazavyo mbele ya wao wamkataye manyoya, hivyo hakufungua kinywa chake.
He was offrid, for he wolde, and he openyde not his mouth; as a scheep he schal be led to sleyng, and he schal be doumb as a lomb bifore hym that clippith it, and he schal not opene his mouth.
8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa. Nani awezaye kueleza kuhusu kizazi chake? Kwa maana alikatiliwa mbali na nchi ya walio hai, alipigwa kwa ajili ya makosa ya watu wangu.
He is takun awey fro angwisch and fro doom; who schal telle out the generacioun of hym? For he was kit doun fro the lond of lyueris. Y smoot hym for the greet trespas of my puple.
9 Wakamfanyia kaburi pamoja na waovu, pamoja na matajiri katika kifo chake, ingawa hakutenda jeuri, wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
And he schal yyue vnfeithful men for biriyng, and riche men for his deth; for he dide not wickidnesse, nether gile was in his mouth;
10 Lakini yalikuwa ni mapenzi ya Bwana kumchubua na kumsababisha ateseke. Ingawa Bwana amefanya maisha yake kuwa sadaka ya hatia, ataona uzao wake na kuishi siku nyingi, nayo mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake.
and the Lord wolde defoule hym in sikenesse. If he puttith his lijf for synne, he schal se seed long durynge, and the wille of the Lord schal be dressid in his hond.
11 Baada ya maumivu ya nafsi yake, ataona nuru ya uzima na kuridhika; kwa maarifa yake, mtumishi wangu mwenye haki atawafanya wengi kuwa wenye haki, naye atayachukua maovu yao.
For that that his soule trauelide, he schal se, and schal be fillid. Thilke my iust seruaunt schal iustifie many men in his kunnyng, and he schal bere the wickidnessis of hem.
12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu miongoni mwa wakuu, naye atagawana nyara pamoja na wenye nguvu, kwa sababu aliyamimina maisha yake hadi mauti, naye alihesabiwa pamoja na wakosaji. Kwa kuwa alichukua dhambi za wengi, na kuwaombea wakosaji.
Therfor Y schal yelde, ethir dele, to hym ful many men, and he schal departe the spuilis of the stronge feendis; for that that he yaf his lijf in to deth, and was arettid with felenouse men; and he dide a wei the synne of many men, and he preiede for trespassouris.