< Isaya 53 >
1 Ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?
Who has believed our report? And to whom has the arm of the Lord been revealed?
2 Alikua mbele yake kama mche mwororo na kama mzizi katika nchi kavu. Hakuwa na uzuri wala utukufu wa kutuvutia kwake, hakuwa na chochote katika sura yake cha kutufanya tumtamani.
And he will rise up like a tender plant in his sight, and like a root from the thirsty ground. There is no beautiful or stately appearance in him. For we looked upon him, and there was no aspect, such that we would desire him.
3 Alidharauliwa na kukataliwa na wanadamu, mtu wa huzuni nyingi, ajuaye mateso. Kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, alidharauliwa, wala hatukumhesabu kuwa kitu.
He is despised and the least among men, a man of sorrows who knows infirmity. And his countenance was hidden and despised. Because of this, we did not esteem him.
4 Hakika alichukua udhaifu wetu na akajitwika huzuni zetu, hata hivyo tulidhania kuwa amepigwa na Mungu, akapigwa sana naye, na kuteswa.
Truly, he has taken away our weaknesses, and he himself has carried our sorrows. And we thought of him as if he were a leper, or as if he had been struck by God and humiliated.
5 Lakini alitobolewa kwa ajili ya makosa yetu, alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu; adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake, na kwa majeraha yake sisi tumepona.
But he himself was wounded because of our iniquities. He was bruised because of our wickedness. The discipline of our peace was upon him. And by his wounds, we are healed.
6 Sisi sote, kama kondoo, tumepotea, kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe, naye Bwana aliweka juu yake maovu yetu sisi sote.
We have all gone astray like sheep; each one has turned aside to his own way. And the Lord has placed all our iniquity upon him.
7 Alionewa na kuteswa, hata hivyo hakufungua kinywa chake; aliongozwa kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, kama vile kondoo anyamazavyo mbele ya wao wamkataye manyoya, hivyo hakufungua kinywa chake.
He was offered up, because it was his own will. And he did not open his mouth. He will be led like a sheep to the slaughter. And he will be mute like a lamb before his shearer. For he will not open his mouth.
8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa. Nani awezaye kueleza kuhusu kizazi chake? Kwa maana alikatiliwa mbali na nchi ya walio hai, alipigwa kwa ajili ya makosa ya watu wangu.
He was lifted up from anguish and judgment. Who will describe his life? For he has been cut off from the land of the living. Because of the wickedness of my people, I have struck him down.
9 Wakamfanyia kaburi pamoja na waovu, pamoja na matajiri katika kifo chake, ingawa hakutenda jeuri, wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
And he will be given a place with the impious for his burial, and with the rich for his death, though he has done no iniquity, nor was deceit in his mouth.
10 Lakini yalikuwa ni mapenzi ya Bwana kumchubua na kumsababisha ateseke. Ingawa Bwana amefanya maisha yake kuwa sadaka ya hatia, ataona uzao wake na kuishi siku nyingi, nayo mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake.
But it was the will of the Lord to crush him with infirmity. If he lays down his life because of sin, he will see offspring with long lives, and the will of the Lord will be directed by his hand.
11 Baada ya maumivu ya nafsi yake, ataona nuru ya uzima na kuridhika; kwa maarifa yake, mtumishi wangu mwenye haki atawafanya wengi kuwa wenye haki, naye atayachukua maovu yao.
Because his soul has labored, he will see and be satisfied. By his knowledge, my just servant will himself justify many, and he himself will carry their iniquities.
12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu miongoni mwa wakuu, naye atagawana nyara pamoja na wenye nguvu, kwa sababu aliyamimina maisha yake hadi mauti, naye alihesabiwa pamoja na wakosaji. Kwa kuwa alichukua dhambi za wengi, na kuwaombea wakosaji.
Therefore, I will allot to him a great number. And he will divide the spoils of the strong. For he has handed over his life to death, and he was reputed among criminals. And he has taken away the sins of many, and he has prayed for the transgressors.