< Isaya 52 >
1 Amka, amka, ee Sayuni, jivike nguvu. Vaa mavazi yako ya fahari, ee Yerusalemu, mji mtakatifu. Asiyetahiriwa na aliye najisi hataingia kwako tena.
Heräjä, heräjä, pukeudu voimaasi, Siion; pukeudu juhlapukuusi, Jerusalem, sinä pyhä kaupunki. Sillä ei koskaan enää astu sinun sisällesi ympärileikkaamaton eikä saastainen.
2 Jikungʼute mavumbi yako, inuka, uketi kwenye kiti cha enzi, ee Yerusalemu. Jifungue minyororo iliyo shingoni mwako, ee Binti Sayuni uliye mateka.
Pudista päältäsi tomu, nouse istuimellesi, Jerusalem; irroita kahleet kaulastasi, sinä vangittu tytär Siion.
3 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Mliuzwa pasipo malipo, nanyi mtakombolewa bila fedha.”
Sillä näin sanoo Herra: Ilmaiseksi teidät myytiin, rahatta teidät lunastetaan.
4 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Hapo kwanza watu wangu walishuka Misri kuishi, hatimaye, Ashuru wakawaonea.
Sillä näin sanoo Herra, Herra: Minun kansani meni ensin alas Egyptiin asumaan siellä muukalaisena, ja sitten Assur sorti sitä ilman syytä.
5 “Basi sasa nina nini hapa?” asema Bwana. “Kwa kuwa watu wangu wamechukuliwa pasipo malipo, nao wale wanaowatawala wanawadhihaki,” asema Bwana. “Mchana kutwa jina langu limetukanwa bila kikomo.
Ja nyt, mitä minulla on tekemistä täällä, sanoo Herra, kun minun kansani on viety pois ilmaiseksi? Sen valtiaat elämöivät, sanoo Herra, ja minun nimeäni pilkataan alati, kaiket päivät.
6 Kwa hiyo watu wangu watalijua Jina langu; kwa hiyo katika siku ile watajua kwamba ndimi niliyetangulia kulisema. Naam, ni mimi.”
Sentähden minun kansani on tunteva minun nimeni, sentähden se on tunteva sinä päivänä, että minä olen se, joka sanon: "Katso, tässä minä olen".
7 Tazama jinsi miguu ya wale waletao habari njema ilivyo mizuri juu ya milima, wale wanaotangaza amani, wanaoleta habari njema, wanaotangaza wokovu, wauambiao Sayuni, “Mungu wako anatawala!”
Kuinka suloiset ovat vuorilla ilosanoman tuojan jalat, hänen, joka julistaa rauhaa, ilmoittaa hyvän sanoman, joka julistaa pelastusta, sanoo Siionille: "Sinun Jumalasi on kuningas!"
8 Sikiliza! Walinzi wako wanapaza sauti zao, pamoja wanapaza sauti zao kwa furaha. Wakati Bwana atakaporejea Sayuni, wataliona kwa macho yao wenyewe.
Kuule! Vartijasi korottavat äänensä, kaikki he riemuitsevat, sillä he näkevät silmästä silmään, kuinka Herra palajaa Siioniin.
9 Pazeni sauti ya nyimbo za furaha pamoja, enyi magofu ya Yerusalemu, kwa maana Bwana amewafariji watu wake, ameikomboa Yerusalemu.
Huutakaa ilosta, riemuitkaa, kaikki te Jerusalemin rauniot, sillä Herra lohduttaa kansansa, lunastaa Jerusalemin.
10 Mkono mtakatifu wa Bwana umefunuliwa machoni pa mataifa yote, nayo miisho yote ya dunia itaona wokovu wa Mungu wetu.
Herra paljastaa pyhän käsivartensa kaikkien kansojen nähden, ja kaikki maan ääret saavat nähdä meidän Jumalamme autuuden.
11 Ondokeni, ondokeni, tokeni huko! Msiguse kitu chochote kilicho najisi! Tokeni kati yake mwe safi, ninyi mchukuao vyombo vya Bwana.
Pois, pois! Lähtekää sieltä, älkää koskeko saastaiseen; lähtekää sen keskeltä, puhdistautukaa, te Herran aseenkantajat.
12 Lakini hamtaondoka kwa haraka, wala hamtakwenda kwa kukimbia; kwa maana Bwana atatangulia mbele yenu, Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi nyuma yenu.
Sillä ei teidän tarvitse kiiruusti lähteä, ei paeten kulkea; sillä Herra käy teidän edellänne, Israelin Jumala seuraa suojananne.
13 Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa hekima; atatukuzwa, na kuinuliwa juu, na kukwezwa sana.
Katso, minun palvelijani menestyy, hän on nouseva, kohoava ja sangen korkea oleva.
14 Kama walivyokuwa wengi walioshangazwa naye, kwani uso wake ulikuwa umeharibiwa sana zaidi ya mtu yeyote na umbo lake kuharibiwa zaidi ya mfano wa mwanadamu:
Niinkuin monet kauhistuivat häntä-sillä niin runneltu, ei enää ihmisenkaltainen, oli hänen muotonsa, hänen hahmonsa ei ollut ihmislasten hahmo-
15 hivyo atayashangaza mataifa mengi, nao wafalme watafunga vinywa vyao kwa sababu yake. Kwa kuwa yale ambayo hawakuambiwa, watayaona, nayo yale wasiyoyasikia, watayafahamu.
niin hän on saattava ihmetyksiin monet kansat, hänen tähtensä kuninkaat sulkevat suunsa. Sillä mitä heille ei ikinä ole kerrottu, sen he saavat nähdä, mitä he eivät ole kuulleet, sen he saavat havaita.