< Isaya 5 >
1 Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
Jeg vil synge om min elskede, synge min venns sang om hans vingård. Min venn hadde en vingård på en fruktbar haug.
2 Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
Og han gravde den om og renset den for sten og plantet edle vintrær i den og bygget et tårn i dens midte og hugg også ut en perse i den; og han ventet at den skulde bære gode druer, men den bar ville.
3 “Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
Og nu, I Jerusalems innbyggere og Judas menn, døm mellem mig og min vingård!
4 Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
Hvad var det mere å gjøre med min vingård, som jeg ikke har gjort med den? Hvorfor bar den ville druer når jeg ventet at den skulde bære gode?
5 Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
Så vil jeg nu la eder vite hvad jeg vil gjøre med min vingård: Jeg vil ta bort dens gjerde, så den blir avgnaget; jeg vil rive ned dens mur, så den blir nedtrådt.
6 Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
Og jeg vil la den ligge øde; den skal ikke skjæres og ikke hakkes, så den skyter op i torn og tistel, og skyene vil jeg byde at de ikke skal la regn falle på den.
7 Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
For Herrens, hærskarenes Guds vingård er Israels hus, og Judas menn hans kjæreste plantning; og han ventet rett, men se, der er blodsutgydelse; han ventet rettferdighet, men se, der er skrik.
8 Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
Ve eder som legger hus til hus og mark til mark, inntil det ikke er mere rum tilbake, så I blir boende alene i landet.
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
I mine ører lyder det fra Herren, hærskarenes Gud: Sannelig, mange hus skal bli øde, store og gode hus skal stå tomme;
10 Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
for en vingård på ti dagers plogland skal gi en bat, og en homers utsæd skal gi en efa.
11 Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
Ve dem som står tidlig op om morgenen og jager efter sterk drikk, som sitter langt utover aftenen, glødende av vin!
12 Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
Citar og harpe, pauke og fløite og vin har de i sine drikkelag; men Herrens verk ser de ikke, og hans henders gjerning har de ikke øie for.
13 Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
Derfor blir mitt folk bortført uforvarende, dets stormenn lider hunger, og dets larmende hop vansmekter av tørst.
14 Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol )
Derfor blir dødsriket ennu grådigere og spiler op sin munn umåtelig, og ned farer byens fornemme og dens larmende hop og dens buldrende sverm og alle som jubler i den. (Sheol )
15 Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
Og mennesket blir bøiet, og mannen ydmyket, og de overmodiges øine blir ydmyket.
16 Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
Og høi blir Herren, hærskarenes Gud, ved dommen, og den hellige Gud viser sig hellig ved rettferdighet.
17 Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
Og lam skal beite der som på sin egen mark, og de rikes jord legges øde og fortæres av fremmede.
18 Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
Ve dem som drar på misgjerningen med løgnens tauger og på synden som med vognrep,
19 kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
de som sier: La ham skynde sig, la ham haste med sin gjerning, så vi kan få se den! La det råd som Israels Hellige har tatt, nærme sig, la det komme, så vi kan lære det å kjenne!
20 Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
Ve dem som kaller det onde godt og det gode ondt, som gjør mørke til lys og lys til mørke, som gjør bittert til søtt og søtt til bittert!
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
Ve dem som er vise i egne øine og forstandige i egne tanker!
22 Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
Ve dem som er helter til å drikke vin og dyktige til å blande sterk drikk,
23 wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
de som for gave gir rett til den som har urett, og tar retten fra de rettferdige!
24 Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Derfor, som ilden fortærer halm, og høi synker sammen i luen, så skal deres rot råtne, og deres blomst fare op som støv; for de har forkastet Herrens, hærskarenes Guds lov og foraktet Israels Helliges ord.
25 Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Derfor optendes Herrens vrede over hans folk, og han rekker ut sin hånd mot det og slår det, så fjellene bever, og likene ligger som skarnet midt på gatene. Men med alt dette vender hans vrede ikke tilbake, og ennu er hans hånd rakt ut.
26 Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
Og han løfter et banner for hedningefolkene langt borte og piper fienden hit fra jordens ende; og se, hastig og lett kommer han.
27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
Der er ingen trett og ingen som snubler blandt dem, ingen som blunder eller sover; beltet om lendene går ikke op, og ingen skorem sønderrives.
28 Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
Fiendens piler er hvesset, og alle hans buer spent; hans hesters hover kan lignes med flintesten, og hans vognhjul er som stormvinden.
29 Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
Hans brøl er som løvinnens, han brøler som de unge løver og brummer og griper sitt rov og bærer det bort, og der er ingen som redder.
30 Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.
Og det bruser over det på den dag, likesom havet bruser; og skuer en til jorden, se, da er det mørke! Trengsel og lys! Det blir mørkt på dets skydekte himmel.