< Isaya 5 >
1 Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
Nu tad, es dziedāšu savam mīļam, sava drauga dziesmu par Viņa vīna dārzu: manam mīļam bija vīna dārzs taukā pakalnā.
2 Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
Un Viņš to aptaisīja ar sētu un tīrija no akmeņiem un tur stādīja labus vīna kokus un uztaisīja torni vidū un raka vīna spaidu iekšā un gaidīja, ka tas nesīs labus ogu ķekarus, bet tas nesa sūrus ķekarus.
3 “Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
Nu tad, Jeruzālemes iedzīvotāji un Jūda vīri, tiesājat jel starp Mani un Manu vīna dārzu.
4 Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
Ko tad vēl vairāk bija darīt pie Mana vīna dārza, nekā Es esmu darījis? Kāpēc Es esmu gaidījis, ka tas labus ogu ķekarus nestu, un viņš nesis sūrus ķekarus?
5 Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
Nu tad, Es jums teikšu, ko Es ar Savu vīna dārzu darīšu. Es atņemšu viņa sētu, ka viņš top noganīts, Es noārdīšu viņa mūri, ka viņš top samīts.
6 Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
Un Es viņu darīšu par postažu: viņš netaps apgraizīts nedz apkapāts, bet dadži un ērkšķi tur uzdīgs, un Es pavēlēšu padebešiem, ka uz to nebūs līt lietum.
7 Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
Tiešām, Tā Kunga Cebaot vīna dārzs ir Israēla nams, un Jūda vīri ir Viņa līksmības stādi. Viņš gaida uz tiesu, un redzi, asins plūdi, uz taisnību, un redzi, vaidi!
8 Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
Ak vai, tiem, kas rauj namu pie nama, krāj tīrumu pie tīruma, kamēr vietas vairs neatliek, un ka jūs paliekat tie vienīgie iedzīvotāji zemē!
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
Tas Kungs Cebaot saka manās ausīs: tiešām, daudz namu būs postā, lieli un skaisti bez iedzīvotāja.
10 Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
Tiešām, desmit vīna dārza birzumi nesīs vienu vienīgu batu, un viens gomers sēklas nesīs vienu ēfu.
11 Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
Ak vai, tiem, kas agri cēlušies skrien pēc stipra dzēriena, un kavējās līdz tumsai, kamēr vīns tos sakarsē!
12 Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
Un tur ir kokles un soma stabules, bungas un stabules un vīns viņu dzīrēs; bet Tā Kunga darbu tie neuzlūko, uz Viņa roku darbu tie nerauga.
13 Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
Tādēļ Mani ļaudis cietumā taps aizvesti no nejauši, un viņu cienīgie cietīs badu, un viņu dzīrenieki iztvīks no slāpēm.
14 Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol )
Tādēļ elle atpletusi savu rīkli un atdarījusi savu muti bez mēra, ka nogrimst (Jeruzālemes) greznums un viņas ļaužu drūzma, un viņas troksnis, un kas tur līksmojās. (Sheol )
15 Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
Tad ļaudis taps locīti un vīri pazemoti, un lepno acis taps pazemotas.
16 Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
Bet Tas Kungs Cebaot parādīsies augsts tiesā, un Dievs, tas svētais, parādīsies svēts taisnībā.
17 Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
Tad jēri (tur) barosies kā savās ganībās, un svešinieki noēdīs bagāto izpostītās vietas.
18 Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
Ak vai, tiem, kas netaisnību velk ar nelietības valgiem, un grēku kā ar ratu virvēm!
19 kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
Kas saka: Lai Viņš steidzās, lai Viņš drīz dara Savu darbu, ka mēs to redzam, un lai tuvojās un nāk tas padoms, kas Israēla Svētajam, ka mēs to manam.
20 Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
Ak vai, tiem, kas ļaunu saka labu esam un labu esam ļaunu, kas tumsību dara par gaismu un gaismu par tumsību, kas rūgtu dara par saldu un saldu par rūgtu!
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
Ak vai, tiem, kas gudri savās acīs un prātīgi pēc pašu prāta!
22 Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
Ak vai, tiem, kas varoņi uz vīna dzeršanu un spēka vīri uz stipru dzērienu.
23 wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
Kas dāvanu dēļ bezdievīgo attaisno un taisniem atrauj taisnību!
24 Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Tādēļ tā kā uguns liesma aprij rugājus un kā svelmē siens sagrūst, tāpat būs viņu sakne kā prauli, un viņu ataugas izputēs kā putekļi, tādēļ ka tie atmet Tā Kunga Cebaot bauslību un nicina Israēla Svētaja vārdus.
25 Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Tādēļ Tā Kunga dusmība iedegās pret Viņa ļaudīm, un Viņš izstiepj Savu roku pret tiem un tos sit, ka kalni dreb, un viņu miroņi ir kā dubļi ielas vidū. Ar visu to Viņa dusmība nenovēršas, un Viņa roka vēl ir izstiepta.
26 Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
Un Viņš paceļ karogu tiem pagāniem, kas tālu, un pasvilps kādam no zemes gala. Un redzi, ātri un steigšus tas nāk.
27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
Neviens nepiekūst un neklūp viņu starpā, neviens nesnauž nedz guļ, nedz viņa gurnu josta ir atraisīta, nedz viņa kurpju siksna sarauta.
28 Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
Viņa bultas ir asas un visi viņa stopi uzvilkti, viņa zirgu nagi tik cieti kā akmens, un viņu rati kā viesulis.
29 Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
Viņu rūkšana ir kā briesmīgām lauvām, un tie rūc kā jauni lauvas un tas kauc un satver laupījumu un aiznes, un glābēja nav.
30 Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.
Un tas kauc pret viņiem tai diena, kā jūra kauc; kad zemi uzlūko, redzi, tā ir tumša, rīb un zib, tumši pār tiem arī debesis.