< Isaya 5 >

1 Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
Minä laulan ystävästäni, laulan rakkaani laulun hänen viinitarhastaan. Ystävälläni oli viinitarha lihavalla vuorenrinteellä.
2 Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
Hän kuokki ja kivesi sen ja istutti siihen jaloja köynnöksiä, rakensi sen keskelle tornin ja hakkasi sinne myös kuurnan. Ja hän odotti sen kasvavan rypäleitä, mutta se kasvoi villimarjoja.
3 “Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
Ja nyt, te Jerusalemin asukkaat ja Juudan miehet, tuomitkaa minun ja minun viinitarhani välillä.
4 Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
Mitä olisi viinitarhalleni vielä ollut tehtävä, jota en olisi sille tehnyt? Miksi se kasvoi villimarjoja, kun minä odotin sen kasvavan rypäleitä?
5 Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
Mutta nyt minä ilmoitan teille, mitä teen viinitarhalleni: minä poistan siitä aidan, niin että se jää hävitettäväksi, särjen siitä muurin, niin että se jää tallattavaksi.
6 Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
Minä hävitän sen: ei sitä enää vesota eikä kuokita, vaan se on kasvava ohdaketta ja orjantappuraa, ja minä kiellän pilvet sille vettä satamasta.
7 Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
Sillä Israelin heimo on Herran Sebaotin viinitarha, ja Juudan miehet ovat hänen ilo-istutuksensa. Ja hän odotti oikeutta, mutta katso, tuli oikeuttomuus, ja vanhurskautta, mutta katso, tuli vaikerrus.
8 Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
Voi niitä, jotka liittävät talon taloon, yhdistävät pellon peltoon, kunnes ei jää enää tilaa ja te yksin asutte maassa!
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
Minun korviini kuului Herran Sebaotin sana: Totisesti, ne monet talot tulevat autioiksi, ne suuret ja kauniit asujattomiksi.
10 Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
Sillä kymmenen auranalaa viinitarhaa on antava yhden bat-mitan, ja hoomerin kylvö on antava eefan.
11 Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
Voi niitä, jotka aamuvarhaisesta väkijuoman jäljessä juoksevat ja iltamyöhään viipyvät viinistä hehkuvina!
12 Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
Kanteleet, harput, vaskirummut, huilut ja viinit on heillä pidoissansa, mutta Herran tekoja he eivät tarkkaa, eivät näe hänen kättensä töitä.
13 Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
Sentähden minun kansani siirretään maastansa äkkiarvaamatta, sen ylhäiset kärsivät nälkää, ja sen remuava joukko nääntyy janoon.
14 Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol h7585)
Sentähden tuonela levittää kitansa ammolleen, avaa suunsa suunnattomaksi; ja sinne menee sen loisto, sen remuava ja pauhaava joukko, kaikki sen ilonpitäjät. (Sheol h7585)
15 Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
Silloin ihminen masentuu ja mies painuu maahan, maahan painuvat ylpeitten silmät;
16 Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
mutta Herra Sebaot on oleva korkea tuomiossa, pyhä Jumala on oleva pyhä vanhurskaudessa.
17 Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
Ja karitsat käyvät siellä niinkuin laitumillansa, ja vieraat syöttävät rikkaitten rauniosijoja.
18 Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
Voi niitä, jotka vetävät perässänsä rangaistusta turhuuden köysillä, synnin palkkaa kuin vaunujen valjailla;
19 kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
niitä, jotka sanovat: "Joutukoon pian hänen tekonsa, että me sen näemme; täyttyköön ja tapahtukoon Israelin Pyhän aivoitus, että me sen tiedämme!"
20 Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
Voi niitä, jotka sanovat pahan hyväksi ja hyvän pahaksi, jotka tekevät pimeyden valkeudeksi ja valkeuden pimeydeksi, jotka tekevät karvaan makeaksi ja makean karvaaksi!
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
Voi niitä, jotka ovat viisaita omissa silmissään ja ymmärtäväisiä omasta mielestänsä!
22 Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
Voi niitä, jotka ovat urhoja viinin juonnissa ja aimomiehiä väkijuoman sekoittamisessa,
23 wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
jotka lahjuksesta julistavat syyllisen syyttömäksi ja ottavat oikeuden siltä, joka oikeassa on!
24 Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Sentähden, niinkuin tulen kieli syö oljet ja kuloheinä raukeaa liekkiin, niin heidän juurensa mätänee, ja heidän kukkansa hajoaa tomuna ilmaan, sillä he ovat ylenkatsoneet Herran Sebaotin lain ja pitäneet pilkkanansa Israelin Pyhän sanaa.
25 Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Sentähden syttyi Herran viha hänen kansaansa kohtaan: hän ojensi kätensä sitä vastaan ja löi sitä, niin että vuoret vapisivat ja heidän raatonsa olivat tunkiona keskellä katuja. Tästä kaikesta ei hänen vihansa asettunut, vaan hänen kätensä on vielä ojennettuna.
26 Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
Ja hän pystyttää viirin kaukaiselle kansalle ja viheltää sen luokseen maan äärestä. Ja katso, se tulee viipymättä, nopeasti.
27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
Ei kukaan heistä väsy eikä kompastu, ei kukaan torku eikä nuku, ei vyö kupeilta aukene, eikä kengänpaula katkea.
28 Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
Sen nuolet ovat teroitetut, sen jouset kaikki jännitetyt, sen orhien kaviot ovat kuin pii, ja sen rattaat kuin rajuilma.
29 Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
Sen kiljunta on kuin naarasleijonan, se kiljuu kuin nuoret jalopeurat, se ärjyy ja tempaa saaliin ja vie sen pois, eikä pelastajaa ole.
30 Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.
Se ärjyy sille sinä päivänä, niinkuin meri ärjyy. Silloin tähyillään maata, mutta katso, on pimeys, on ahdistus, ja valo on pimennyt sen synkeyteen.

< Isaya 5 >