< Isaya 5 >

1 Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
I schal synge for my derlyng the song of myn vnclis sone, of his vyner. A vyner was maad to my derlyng, in the horne in the sone of oile.
2 Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
And he heggide it, and chees stoonys therof, and plauntide a chosun vyner; and he bildide a tour in the myddis therof, and rerede a presse ther ynne; and he abood, that it schulde bere grapis, and it bare wielde grapis.
3 “Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
Now therfor, ye dwelleris of Jerusalem, and ye men of Juda, deme bitwixe me and my viner.
4 Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
What is it that Y ouyt to do more to my vyner, and Y dide not to it? whether that Y abood, that it schulde bere grapis, and it bare wielde grapis?
5 Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
And now Y schal schewe to you, what Y schal do to my vyner. Y schal take awei the hegge therof, and it schal be in to rauyschyng; Y schal caste doun the wal therof, and it schal be in to defoulyng; and Y schal sette it desert,
6 Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
ether forsakun. It schal not be kit, and it schal not be diggid, and breris and thornes schulen `growe vp on it; and Y schal comaunde to cloudis, that tho reyne not reyn on it.
7 Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
Forsothe the vyner of the Lord of oostis is the hous of Israel, and the men of Juda ben the delitable buriownyng of hym. Y abood, that it schal make doom, and lo! wickidnesse; and that it schulde do riytfulnesse, and lo! cry.
8 Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
Wo to you that ioynen hows to hous, and couplen feeld to feeld, `til to the ende of place. Whether ye aloone schulen dwelle in the myddis of the lond?
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
These thingis ben in the eeris of me, the Lord of oostis; if many housis ben not forsakun, grete housis and faire, with outen dwellere, bileue ye not to me.
10 Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
For whi ten acris of vynes schulen make a potel, and thretti buschels of seed schulen make thre buschels.
11 Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
Wo to you that risen togidere eerli to sue drunkennesse, and to drinke `til to euentid, that ye brenne with wyn.
12 Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
Harpe, and giterne, and tympan, and pipe, and wyn ben in youre feestis; and ye biholden not the werk of the Lord, nether ye biholden the werkis of hise hondis.
13 Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
Therfor my puple is led prisoner, for it hadde not kunnyng; and the noble men therof perischiden in hungur, and the multitude therof was drye in thirst.
14 Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol h7585)
Therfor helle alargide his soule, and openyde his mouth with outen ony ende; and strong men therof, and the puple therof, and the hiy men, and gloriouse men therof, schulen go doun to it. (Sheol h7585)
15 Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
And a man schal be bowid doun, and a man of age schal be maad low; and the iyen of hiy men schulen be pressid doun.
16 Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
And the Lord of oostis schal be enhaunsid in doom, and hooli God schal be halewid in riytfulnesse.
17 Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
And lambren schulen be fed bi her ordre, and comelyngis schulen ete desert places turned in to plentee.
18 Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
Wo to you that drawen wickydnesse in the cordis of vanyte, and drawen synne as the boond of a wayn; and ye seien,
19 kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
The werk of hym haaste, and come soone, that we se; and the counsel of the hooli of Israel neiy, and come, and we schulen knowe it.
20 Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
Wo to you that seien yuel good, and good yuel; and putten derknessis liyt, and liyt derknessis; and putten bittir thing in to swete, and swete thing in to bittir.
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
Wo to you that ben wise men in youre iyen, and ben prudent bifor you silf.
22 Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
Wo to you that ben myyti to drynke wyn, and ben stronge to meddle drunkenesse;
23 wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
and ye iustifien a wickid man for yiftis, and ye taken awei the riytfulnesse of a iust man fro hym.
24 Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
For this thing, as the tunge of fier deuourith stobil, and the heete of flawme brenneth, so the roote of hem schal be as a deed sparcle, and the seed of hem schal stie as dust; for thei castiden awei the lawe of the Lord of oostis, and blasfemyden the speche of the hooli of Israel.
25 Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
Therfor the strong veniaunce of the Lord was wrooth ayens his puple, and he stretchide forth his hond on it, and smoot it; and hillis weren disturblid, and the deed bodies of hem weren maad as a toord in the myddis of stretis. In alle these thingis the stronge vengeaunce of him was not turned awei, but yit his hond was stretchid forth.
26 Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
And he schal reise a signe among naciouns afer, and he schal hisse to hym fro the endis of erthe; and lo! he schal haaste, and schal come swiftli.
27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
Noon is failynge nethir trauelynge in that oost; he schal not nappe, nether slepe, nether the girdil of his reynes schal be vndo, nether the lace of his scho schal be brokun.
28 Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
Hise arowis ben scharpe, and alle hise bowis ben bent; the houys of hise horsis ben as a flynt, and hise wheelis ben as the feersnesse of tempest.
29 Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
His roryng schal be as of lioun; he schal rore as the whelpis of liouns; and he schal gnaste, and schal holde prey, and schal biclippe, and noon schal be, that schal delyuere.
30 Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.
And he schal sowne on it in that dai, as doith the soun of the see; we schulen biholde in to the erthe, and lo! derknessis of tribulacioun, and liyt is maad derk in the derknesse therof.

< Isaya 5 >