< Isaya 5 >

1 Nitaimba wimbo kwa ajili ya mmoja nimpendaye, kuhusu shamba lake la mizabibu: Mpendwa wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima chenye rutuba.
Let me sing please to beloved [one] my a song of beloved my of vineyard his a vineyard it belonged to beloved [one] my on a horn of a son of oil.
2 Alililima na kuondoa mawe na akaliotesha mizabibu bora sana. Akajenga mnara wa ulinzi ndani yake, na kutengeneza shinikizo la kukamulia divai pia. Kisha akatazamia kupata mazao ya zabibu nzuri, lakini lilizaa matunda mabaya tu.
And he dug it and he cleared of stones it and he planted it a choice vine and he built a tower in [the] middle of it and also a wine-vat he dug out in it and he waited to produce grapes and it produced wild grapes.
3 “Basi enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.
And therefore O inhabitant[s] of Jerusalem and everyone of Judah judge please between me and between vineyard my.
4 Ni nini zaidi ambacho kingeweza kufanyika kwa shamba langu la mizabibu kuliko yale niliyofanya? Nilipotazamia kupata zabibu nzuri, kwa nini lilizaa zabibu mbaya tu?
What? [is] to do still for vineyard my and not I have done for it why? did I wait to produce grapes and did it produce wild grapes.
5 Sasa nitawaambia lile nitakalolitendea shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake, nalo litaharibiwa, nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa.
And therefore let me make know please you [that] which I [am] about to do to vineyard my I will remove hedge its and it will become grazing I will break down wall its and it will become a trampling place.
6 Nitalifanya nchi ya ukiwa isiyokaliwa na watu, halitakatiwa matawi wala kulimwa, nayo michongoma na miiba itamea huko, nitaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.”
And I will make it a desolation not it will be pruned and not it will be hoed and it will grow up thorn[s] and bush[es] and to the clouds I will command from raining on it rain.
7 Shamba la mzabibu la Bwana Mwenye Nguvu Zote ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni bustani yake ya kumpendeza. Alitazamia haki, lakini akaona umwagaji damu, alitazamia uadilifu, lakini akasikia vilio vya taabu.
For [the] vineyard of Yahweh of hosts [is] [the] house of Israel and everyone of Judah [is] [the] plantation of delight his and he waited for justice and there! bloodshed for righteousness and there! an outcry.
8 Ole wenu mnaoongeza nyumba baada ya nyumba na kuunganisha mashamba baada ya mashamba hadi hakuna nafasi iliyobaki, nanyi mnaishi peke yenu katika nchi.
Woe to! [those who] make touch a house a house a field on a field they bring near until there not [is] room and you are made to dwell to alone you in [the] midst of the land.
9 Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema nikisikia: “Hakika nyumba kubwa zitakuwa ukiwa, nayo majumba ya fahari yatabaki bila kukaliwa.
In ears my Yahweh of hosts if not houses many a waste they will become great [houses] and good [houses] from not inhabitant.
10 Shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja ya divai, na homeri ya mbegu zilizopandwa itatoa efa moja tu ya nafaka.”
For ten acres of vineyard they will produce a bath one and seed of a homer it will produce an ephah.
11 Ole wao wale waamkao asubuhi na mapema wakikimbilia kunywa vileo, wale wakawiao sana mpaka usiku, mpaka wamewaka kwa mvinyo.
Woe to! [those who] rise early in the morning strong drink they pursue [those who] delay in the twilight wine it inflames them.
12 Wana vinubi na zeze kwenye karamu zao, matari, filimbi na mvinyo, lakini hawayajali matendo ya Bwana, wala hawana heshima kwa ajili ya kazi ya mikono yake.
And it will be harp and lyre tambourine and flute and wine feast their and [the] deed[s] of Yahweh not they pay attention to and [the] work of hands his not they see.
13 Kwa hiyo watu wangu watakwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ufahamu, watu wao wenye vyeo watakufa kwa njaa na watu wao wengi watakauka kwa kiu.
Therefore it will go into exile people my because not knowledge and honor its [will be] men of hunger and multitude its [will be] parched of thirst.
14 Kwa hiyo kaburi limeongeza hamu yake na kupanua mdomo wake bila kikomo, ndani mwake watashuka wakuu wao na wingi wa watu, pamoja na wagomvi wao, na wafanyao sherehe wote. (Sheol h7585)
Therefore it will enlarge Sheol throat its and it will open wide mouth its to not limit and it will go down splendor its and multitude its and uproar its and [one] exulting in it. (Sheol h7585)
15 Hivyo mwanadamu atashushwa, na binadamu kunyenyekezwa, macho ya wenye majivuno yatanyenyekezwa.
And he has been humbled everyone and he has become low everyone and [the] eyes of proud [people] they will become low.
16 Lakini Bwana Mwenye Nguvu Zote atatukuzwa kwa ajili ya haki yake, naye Mungu Mtakatifu atajionyesha mwenyewe kuwa mtakatifu kwa haki yake.
And he was exalted Yahweh of hosts by judgment and God holy [will] show himself holy by righteousness.
17 Kondoo watajilisha kwenye malisho yao wenyewe, wana-kondoo watajilisha katika magofu ya matajiri.
And they will graze lambs like own pasture their and [the] ruins of fatlings sojourners they will eat.
18 Ole wao wanaovuta dhambi kwa kamba za udanganyifu na uovu kama kwa kamba za mkokoteni,
Woe to! [those who] draw along iniquity with [the] cords of emptiness and like [the] rope of cart sin.
19 kwa wale wanaosema, “Mungu na afanye haraka, aharakishe kazi yake ili tupate kuiona. Huo mpango wa Aliye Mtakatifu wa Israeli na ukamilike, tena udhihirike ili tupate kuujua.”
Those [who] say let it hurry - let it make haste! work his so that we may see and it may draw near and let it come! [the] plan of [the] holy [one] of Israel so we may know.
20 Ole wao wanaoita ubaya ni wema, na wema ni ubaya, wawekao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza, wawekao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu.
Woe to! those [who] say of evil good and of good evil [those who] make darkness into light and light into darkness [those who] make bitter into sweet and sweet into bitter.
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.
Woe to! [people] wise in own eyes their and before own faces their discerning [people].
22 Ole wao walio mashujaa kwa kunywa mvinyo, nao walio hodari katika kuchanganya vileo,
Woe to! [men] mighty for drinking wine and people of ability for mixing strong drink.
23 wale wanaoachilia wenye hatia kwa kupokea hongo, lakini huwanyima haki wasio na hatia.
[those who] justify a wicked [person] [the] consequence of A bribe and [the] righteousness of righteous [people] they take away from him.
24 Kwa hiyo, kama ndimi za moto zirambavyo nyasi, na kama vile majani makavu yazamavyo katika miali ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza na maua yao yatakavyopeperushwa kama mavumbi; kwa kuwa wameikataa sheria ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na kulisukumia mbali neno la Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Therefore as consumes stubble a tongue of fire and dry grass a flame it sinks down root their like rottenness it will be and blossom their like dust it will go up for they have rejected [the] law of Yahweh of hosts and [the] word of [the] holy [one] of Israel they have spurned.
25 Kwa hiyo hasira ya Bwana inawaka dhidi ya watu wake, mkono wake umeinuliwa na anawapiga. Milima inatetemeka, maiti ni kama takataka kwenye barabara. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
There-fore it has burned [the] anger of Yahweh on people his and he has stretched out hand his on it and he has struck it and they have quaked the mountains and it was corpse their like offal in [the] middle of [the] streets for all this not it has turned away anger his and still hand his [is] stretched out.
26 Yeye anainua bendera kwa ajili ya mataifa yaliyo mbali, anapiga filimbi kwa ajili ya wale walio kwenye miisho ya dunia. Tazama wamekuja, kwa kasi na kwa haraka!
And he will lift up a standard for the nations from a distance and he will whistle for it from [the] end of the earth and there! quickly swift it will come.
27 Hakuna hata mmoja wao anayechoka wala kujikwaa, hakuna hata mmoja anayesinzia wala kulala, hakuna mkanda uliolegezwa kiunoni, hakuna gidamu ya kiatu iliyokatika.
There not [is] a weary [one] and there not [is one who] stumbles among it not anyone will slumber and not anyone will sleep and not it has been opened [the] waistband of loins its and not it has been torn apart a thong of sandals its.
28 Mishale yao ni mikali, pinde zao zote zimevutwa, kwato za farasi wao ziko kama jiwe la gumegume, magurudumu ya magari yao ya vita ni kama upepo wa kisulisuli.
Which arrows its [are] sharpened and all bows its [are] bent [the] hooves of horses its like flint they are regarded and wheels its like storm-wind.
29 Ngurumo yao ni kama ile ya simba, wananguruma kama wana simba, wanakoroma wanapokamata mawindo yao, na kuondoka nayo pasipo yeyote wa kuokoa.
Roaring of it [is] like lion (it will roar *Q(K)*) like young lions so it may growl and it may seize prey so it may carry [it] off and there not [is] a deliverer.
30 Katika siku ile watanguruma juu yake kama ngurumo za bahari. Kama mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhiki; hata nuru itatiwa giza kwa mawingu.
And it may growl over it in the day that like [the] growling of [the] sea and someone will look to the land and there! darkness distress and light it has become dark by clouds its.

< Isaya 5 >