< Isaya 49 >

1 Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
ای جزیره‌ها از من بشنوید! و‌ای طوایف از جای دور گوش دهید! خداوند مرا از رحم دعوت کرده واز احشای مادرم اسم مرا ذکر نموده است.۱
2 Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
و دهان مرا مثل شمشیر تیز ساخته، مرا زیر سایه دست خودپنهان کرده است. و مرا تیر صیقلی ساخته درترکش خود مخفی نموده است.۲
3 Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
و مرا گفت: ای اسرائیل تو بنده من هستی که از تو خویشتن راتمجید نموده‌ام!۳
4 Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
اما من گفتم که عبث زحمت کشیدم و قوت خود را بی‌فایده و باطل صرف کردم لیکن حق من با خداوند و اجرت من با خدای من می‌باشد.۴
5 Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
و الان خداوند که مرا از رحم برای بندگی خویش سرشت تا یعقوب را نزد اوبازآورم و تا اسرائیل نزد وی جمع شوند می‌گوید(و در نظر خداوند محترم هستم و خدای من قوت من است ).۵
6 yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
پس می‌گوید: این چیز قلیلی است که بنده من بشوی تا اسباط یعقوب را برپاکنی و ناجیان اسرائیل را باز آوری. بلکه تو را نورامت‌ها خواهم گردانید و تا اقصای زمین نجات من خواهی بود.۶
7 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
خداوند که ولی و قدوس اسرائیل می‌باشد به او که نزد مردم محقر و نزد امت ها مکروه و بنده حاکمان است چنین می‌گوید: پادشاهان دیده برپا خواهند شد و سروران سجده خواهند نمود، به‌سبب خداوند که امین است وقدوس اسرائیل که تو را برگزیده است.۷
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
خداوند چنین می‌گوید: «در زمان رضامندی تو را اجابت نمودم و در روز نجات تو را اعانت کردم. و تو را حفظ نموده عهد قوم خواهم ساخت تا زمین را معمور سازی و نصیب های خراب شده را (به ایشان ) تقسیم نمایی.۸
9 kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
و به اسیران بگویی: بیرون روید و به آنانی که درظلمتند خویشتن را ظاهر سازید. و ایشان درراهها خواهند چرید و مرتعهای ایشان بر همه صحراهای کوهی خواهد بود.۹
10 Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
گرسنه و تشنه نخواهند بود و حرارت و آفتاب به ایشان ضررنخواهد رسانید زیرا آنکه بر ایشان ترحم داردایشان را هدایت خواهد کرد و نزد چشمه های آب ایشان را رهبری خواهد نمود.۱۰
11 Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
و تمامی کوههای خود را طریق‌ها خواهم ساخت وراههای من بلند خواهد شد.۱۱
12 Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
اینک بعضی ازجای دور خواهند آمد و بعضی از شمال و ازمغرب و بعضی از دیار سینیم.»۱۲
13 Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
‌ای آسمانهاترنم کنید! و‌ای زمین وجد نما! و‌ای کوهها آوازشادمانی دهید! زیرا خداوند قوم خود را تسلی می‌دهد و بر مظلومان خود ترحم می‌فرماید.۱۳
14 Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
اما صهیون می‌گوید: «یهوه مرا ترک نموده و خداوند مرا فراموش کرده است.»۱۴
15 “Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
آیا زن بچه شیر خواره خود را فراموش کرده بر پسر رحم خویش ترحم ننماید؟ اینان فراموش می‌کنند امامن تو را فراموش نخواهم نمود.۱۵
16 Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
اینک تو را برکف دستهای خود نقش نمودم و حصارهایت دائم در نظر من است.۱۶
17 Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
پسرانت به تعجیل خواهند آمد و آنانی که تو را خراب و ویران کردند از تو بیرون خواهند رفت.۱۷
18 Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
چشمان خودرا به هر طرف بلند کرده، ببین جمیع اینها جمع شده، نزد تو می‌آیند. خداوند می‌گوید: «به حیات خودم قسم که خود را به جمیع اینها مثل زیورملبس خواهی ساخت و مثل عروس خویشتن رابه آنها خواهی آراست.۱۸
19 “Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
زیرا خرابه‌ها وویرانه های تو و زمین تو که تباه شده بود، اما الان تو از کثرت ساکنان تنگ خواهی شد و هلاک کنندگانت دور خواهند گردید.۱۹
20 Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
پسران تو که بی‌اولاد می‌بودی در سمع تو (به یکدیگر)خواهند گفت: این مکان برای من تنگ است، مراجایی بده تا ساکن شوم.۲۰
21 Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
و تو دردل خودخواهی گفت: کیست که اینها را برای من زاییده است و حال آنکه من بی‌اولاد و نازاد و جلای وطن و متروک می‌بودم. پس کیست که اینها راپرورش داد. اینک من به تنهایی ترک شده بودم پس اینها کجا بودند؟»۲۱
22 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
خداوند یهوه چنین می‌گوید: «اینک من دست خود را بسوی امت هادراز خواهم کرد و علم خویش را بسوی قوم هاخواهم برافراشت. و ایشان پسرانت را درآغوش خود خواهند‌آورد و دخترانت بر دوش ایشان برداشته خواهند شد.۲۲
23 Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
و پادشاهان لالاهای تو و ملکه های ایشان دایه های توخواهند بود و نزد تو رو به زمین افتاده، خاک پای تو را خواهند لیسید و تو خواهی دانست که من یهوه هستم و آنانی که منتظر من باشند خجل نخواهند گردید.۲۳
24 Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
آیا غنیمت از جبار گرفته شود یا اسیران ازمرد قاهر رهانیده گردند.۲۴
25 Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
زیرا خداوند چنین می‌گوید: «اسیران نیز از جبار گرفته خواهند شد وغنیمت از دست ستم پیشه رهانیده خواهدگردید. زیرا که من با دشمنان تو مقاومت خواهم نمود و من پسران تو را نجات خواهم داد.۲۵
26 Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
و به آنانی که بر تو ظلم نمایند گوشت خودشان راخواهم خورانید و به خون خود مثل شراب مست خواهند شد و تمامی بشر خواهند دانست که من یهوه نجات‌دهنده تو و ولی تو و قدیر یعقوب هستم.»۲۶

< Isaya 49 >