< Isaya 49 >

1 Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
Écoutez-moi, îles. Écoutez, vous, peuples, de loin: Yahvé m'a appelé depuis le ventre de ma mère; de l'intérieur de ma mère, il a mentionné mon nom.
2 Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
Il a rendu ma bouche semblable à une épée tranchante. Il m'a caché dans l'ombre de sa main. Il m'a fait une tige polie. Il m'a gardé près de lui dans son carquois.
3 Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
Il m'a dit: « Tu es mon serviteur, Israël, en qui je serai glorifié. »
4 Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
Mais j'ai dit: « C'est en vain que j'ai travaillé. J'ai dépensé mes forces en vain pour rien; mais c'est à Yahvé que revient la justice qui m'est due, et ma récompense auprès de mon Dieu. »
5 Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
Or, Yahvé, celui qui m'a formé dès le ventre de ma mère pour être son serviteur, dit de lui ramener Jacob, et de rassembler Israël auprès de lui, car je suis honorable aux yeux de Yahvé, et mon Dieu est devenu ma force.
6 yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
En effet, il dit: « C'est une chose trop légère que tu sois mon serviteur pour relever les tribus de Jacob, et de restaurer les préservés d'Israël. Je te donnerai aussi comme lumière aux nations, afin que tu sois mon salut jusqu'au bout du monde. »
7 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
Yahvé, le Rédempteur d'Israël, et son Saint, dit à celui que l'homme méprise, à celui que la nation abhorre, à un serviteur des chefs: « Les rois verront et se lèveront, les princes, et ils se prosterneront, à cause de Yahvé qui est fidèle, le Saint d'Israël, qui t'a choisi. »
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
Yahvé dit: « Je t'ai répondu au bon moment. Je vous ai aidé au jour du salut. Je te garderai et te donnerai comme alliance du peuple, pour relever le pays, pour leur faire hériter de l'héritage dévasté,
9 kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
en disant à ceux qui sont liés: « Sortez! »; à ceux qui sont dans les ténèbres: « Montrez-vous! « Ils se nourriront le long des chemins, et leur pâturage sera sur toutes les hauteurs sans arbres.
10 Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
Ils n'auront ni faim ni soif; ni la chaleur ni le soleil ne les frapperont, car celui qui a pitié d'eux les conduira. Il les guidera vers des sources d'eau.
11 Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
Je ferai de toutes mes montagnes une route, et mes autoroutes seront exaltées.
12 Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
Voici, ils viennent de loin, et voici ceux du nord et de l'ouest, et ceux-ci du pays de Sinim. »
13 Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
Chantez, cieux, et soyez joyeux, terre! Laissez-vous aller à chanter, montagnes! Car Yahvé a réconforté son peuple, et aura de la compassion pour ses affligés.
14 Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
Mais Sion dit: « Yahvé m'a abandonné, et le Seigneur m'a oublié. »
15 “Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
« Une femme peut-elle oublier son enfant qu'elle allaite, pour qu'elle n'ait pas de compassion pour le fils de ses entrailles? Oui, ils peuvent oublier, mais je ne vous oublierai pas!
16 Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
Voici, je vous ai gravés sur les paumes de mes mains. Vos murs sont continuellement devant moi.
17 Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
Vos enfants se dépêchent. Vos destructeurs et ceux qui vous ont dévasté vous quitteront.
18 Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
Lève les yeux tout autour, et regarde: tous ceux-là se rassemblent et viennent à toi. Je suis vivant, dit Yahvé, et tu t'en revêtiras comme d'une parure, et habille-toi avec, comme une mariée.
19 “Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
« En effet, pour ce qui est de tes déchets et de tes lieux désolés, et votre terre qui a été détruite, Il est certain que maintenant cette terre sera trop petite pour les habitants, et ceux qui t'ont englouti seront loin.
20 Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
Les enfants de ton deuil diront à tes oreilles, Cet endroit est trop petit pour moi. Donnez-moi un endroit où vivre.
21 Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
Alors tu diras dans ton cœur: « Qui les a conçus pour moi, puisque je suis privé de mes enfants? et que je suis seul, exilé, et que j'erre de long en large? Qui les a évoqués? Voici, j'ai été laissé seul. Où étaient-ils? »
22 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
Le Seigneur Yahvé dit: « Voici que je lève ma main vers les nations, et je lèverai ma bannière vers les peuples. Ils porteront vos fils dans leur sein, et vos filles seront portées sur leurs épaules.
23 Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
Les rois seront vos pères nourriciers, et leurs reines vos mères nourricières. Ils se prosterneront devant toi, le visage tourné vers la terre, et lécher la poussière de vos pieds. Alors vous saurez que je suis Yahvé; et ceux qui m'attendent ne seront pas déçus. »
24 Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
Le butin sera pris aux puissants, ou que les captifs légitimes soient délivrés?
25 Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
Mais Yahvé dit: « Même les captifs des puissants seront emmenés, et le butin récupéré sur le féroce, car je me battrai avec celui qui se battra avec vous. et je sauverai vos enfants.
26 Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Je nourrirai de leur propre chair ceux qui vous oppriment; et ils s'enivreront de leur propre sang, comme d'un vin doux. Alors toute chair saura que moi, Yahvé, je suis votre Sauveur. et ton rédempteur, le Puissant de Jacob. »

< Isaya 49 >