< Isaya 49 >

1 Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
Listen to me, ye distant lands! Attend, ye nations from afar! Jehovah called me at my birth; In my very childhood he called me by name.
2 Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
He made my mouth like a sharp sword; In the shadow of his hand did he hide me. He made me a polished shaft; In his quiver did he hide me.
3 Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
He said to me, Thou art my servant; Israel, in whom I will be glorified.
4 Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
Then I said, I have labored in vain; For naught, for vanity, have I spent my strength; Yet my cause is with Jehovah, And my reward with my God.
5 Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
And now thus saith Jehovah, Who formed me from my birth to be his servant To bring Jacob to him again, And that Israel might be gathered to him, —For I am honored in the eyes of Jehovah, And my God is my strength, —
6 yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
He said, It is a small tiling that thou shouldst be my servant, To raise up the tribes of Jacob, And to restore the preserved of Israel; I will also make thee the light of the nations, That my salvation may reach the ends of the earth.
7 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
Thus saith Jehovah, the Redeemer of Israel, his Holy One, To him that is despised by men, abhorred by the people, To the servant of tyrants; Kings shall see, and stand up, Princes, and they shall pay homage, On account of Jehovah, who is faithful, The Holy One of Israel, who hath chosen thee.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
Thus saith Jehovah; In the time of favor will I hear thee; In the day of deliverance will I help thee; I will preserve thee, and make thee a mediator for the people, To restore the land, to distribute the desolated inheritances;
9 kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
To say to the prisoners, Go forth! To them that are in darkness, Come to the light! They shall feed in the ways, And on all high places shall be their pasture.
10 Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
They shall not hunger, neither shall they thirst; Neither shall the heat nor the sun smite them; For he that hath compassion on them shall lead them; To springs of water shall he guide them.
11 Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
And I will make all my mountains a highway; And my roads shall be prepared.
12 Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
Behold! these shall come from far; And behold! these from the North and from the West, And these from the land of Sinim.
13 Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
Sing, O ye heavens, and rejoice, O earth! Break forth into singing, ye mountains! For Jehovah comforteth his people, And hath compassion on his afflicted ones.
14 Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
Zion saith, “Jehovah hath forsaken me; The Lord hath forgotten me.”
15 “Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
Can a woman forget her sucking child, So as not to have compassion on the son of her womb? Yet, should they forget, I will never forget thee!
16 Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
Behold, I have graven thee on the palms of my hands; Thy walls are ever before my eyes.
17 Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
Thy children shall make haste; They that destroyed and laid thee waste shall depart from thee.
18 Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
Lift up thine eyes around, and see! They all assemble themselves, and come to thee. As I live, saith Jehovah, Thou shalt surely clothe thee with them all, as with a rich dress; Thou shalt bind them on thee, as a bride her jewels.
19 “Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
For thy waste and desolate places, and thy land laid in ruins, Shall now be too narrow for the inhabitants; And they that devoured thee shall be far away.
20 Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
Thou, that hast been childless, shalt yet hear thy sons exclaim: “The place is too narrow for me; make room for me that I may dwell.”
21 Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
And thou shalt say in thy heart, Who hath begotten me these? I surely was childless and unfruitful, An exile, and an outcast; who then hath brought up these? Behold, I was left alone; these, then, where were they?
22 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
Thus saith the Lord Jehovah: I will lift up my hand to the nations, And set up my standard to the kingdoms; They shall bring thy sons in their arms, And thy daughters upon their shoulders.
23 Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
And kings shall be thy nursing fathers, And queens thy nursing mothers; Upon their faces shall they bow down before thee, And lick the dust of thy feet. Thus shalt thou know that I am Jehovah; And they who trust in me shall not be put to shame.
24 Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
Shall the prey be taken away from the mighty? Or shall the spoil of the terrible be rescued?
25 Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
Yea, thus saith Jehovah, The prey shall be taken away from the mighty, And the spoil of the terrible shall be rescued; For with him that contendeth with thee will I contend, And I will save thy children.
26 Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
And I will cause thine oppressors to eat their own flesh; With their own blood shall they be drunk, as with new wine; And all flesh shall know that I Jehovah am thy saviour; That thy redeemer is the Mighty One of Jacob.

< Isaya 49 >