< Isaya 49 >
1 Nisikilizeni, enyi visiwa, sikieni hili, ninyi mataifa mlio mbali: Kabla sijazaliwa, Bwana aliniita, tangu kuzaliwa kwangu, amelitaja jina langu.
Pay attention, you islands, and listen closely, you far away peoples. The Lord has called me from the womb; from the womb of my mother, he has been mindful of my name.
2 Akafanya kinywa changu kuwa kama upanga ulionolewa, katika uvuli wa mkono wake akanificha; akanifanya kuwa mshale uliosuguliwa, na kunificha katika podo lake.
And he has appointed my mouth as a sharp sword. In the shadow of his hand, he has protected me. And he has appointed me as an elect arrow. In his quiver, he has hidden me.
3 Akaniambia, “Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika yeye nitaonyesha utukufu wangu.”
And he has said to me: “You are my servant, Israel. For in you, I will glory.”
4 Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa Bwana, nao ujira wangu uko kwa Mungu wangu.”
And I said: “I have labored toward emptiness. I have consumed my strength without purpose and in vain. Therefore, my judgment is with the Lord, and my work is with my God.”
5 Sasa Bwana asema: yeye aliyeniumba tumboni kuwa mtumishi wake, kumrudisha tena Yakobo kwake na kumkusanyia Israeli, kwa maana nimepata heshima machoni pa Bwana, naye Mungu wangu amekuwa nguvu yangu;
And now, says the Lord, who formed me from the womb as his servant, so that I may bring back Jacob to him, for Israel will not be gathered together, but I have been glorified in the eyes of the Lord and my God has become my strength,
6 yeye asema: “Je, ni jambo dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kurejeza makabila ya Yakobo, na kuwarudisha wale Waisraeli niliowahifadhi? Pia nitakufanya uwe nuru kwa ajili ya watu wa Mataifa, ili upate kuleta wokovu wangu hata miisho ya dunia.”
and so he has said: “It is a small thing that you should be my servant so as to raise up the tribes of Jacob, and so as to convert the dregs of Israel. Behold, I have offered you as a light for the Gentiles, so that you may be my salvation, even to the furthest regions of the earth.”
7 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye Mkombozi na Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwake yeye aliyedharauliwa na kuchukiwa na taifa, kwa mtumishi wa watawala: “Wafalme watakuona na kusimama, wakuu wataona na kuanguka kifudifudi, kwa sababu ya Bwana, aliye mwaminifu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, aliyekuchagua wewe.”
Thus says the Lord, the Redeemer of Israel, his Holy One, to a contemptible soul, to an abominable nation, to the servant of lords: The kings will see, and the princes will rise up, and they will adore, because of the Lord. For he is faithful, and he is the Holy One of Israel, who has chosen you.
8 Hili ndilo asemalo Bwana: “Wakati wangu uliokubalika nitakujibu, nami katika siku ya wokovu nitakusaidia; nitakuhifadhi, nami nitakufanya kuwa agano kwa ajili ya watu, ili kurudisha nchi na kugawanyia urithi tena wale waliokuwa ukiwa,
Thus says the Lord: In a pleasing time, I have heeded you, and in the day of salvation, I have assisted you. And I have preserved you, and I have presented you as a covenant of the people, so that you would lift up the earth, and possess the scattered inheritances,
9 kuwaambia mateka, ‘Tokeni nje,’ nao wale walio gizani, ‘Kuweni huru!’ “Watajilisha kando ya barabara na kupata malisho yao juu ya kila kilima kilicho kitupu.
so that you would say to those who are bound, “Go forth!” and to those who are in darkness, “Be released!” They will pasture along the roads, and their pastures will be in every open place.
10 Hawataona njaa wala kuona kiu, wala hari ya jangwani au jua halitawapiga. Yeye mwenye huruma juu yao atawaonyesha njia, na kuwaongoza kando ya chemchemi za maji.
They will not hunger or thirst, nor will the heat of the sun beat down upon them. For the one who takes pity on them will rule them, and he will give them to drink from fountains of waters.
11 Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara, na njia kuu zangu zitainuliwa.
And I will make all my mountains into a road, and my paths will be exalted.
12 Tazama, watakuja kutoka mbali: wengine kutoka kaskazini, wengine kutoka magharibi, wengine kutoka nchi ya Sinimu.”
Behold, some will come from far away, and behold, others from the north and from the sea, and still others from the land of the south.
13 Pigeni kelele kwa furaha, enyi mbingu; furahi, ee dunia; pazeni sauti kwa kuimba, enyi milima! Kwa maana Bwana anawafariji watu wake, naye atakuwa na huruma kwa watu wake walioumizwa.
Give praise, O heavens! And exult, O earth! Let the mountains give praise with jubilation! For the Lord has consoled his people, and he will take pity on his poor ones.
14 Lakini Sayuni alisema, “Bwana ameniacha, Bwana amenisahau.”
And Zion said: “The Lord has abandoned me, and the Lord has forgotten me.”
15 “Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya, wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa? Ingawa anaweza kusahau, mimi sitakusahau wewe!
Can a woman forget her infant, so as not to take pity on the child of her womb? But even if she would forget, still I shall never forget you.
16 Tazama, nimekuchora kama muhuri katika vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.
Behold, I have engraved you on my hands. Your walls are always before my eyes.
17 Wana wako wanaharakisha kurudi, nao wale waliokuteka wanaondoka kwako.
Your builders have arrived. Those who would tear you down and destroy you, they will depart from you.
18 Inua macho yako ukatazame pande zote: wana wako wote wanakusanyika na kukujia. Kwa hakika kama vile niishivyo, utawavaa wote kama mapambo, na kujifunga nao kama bibi arusi,” asema Bwana.
Lift up your eyes all around, and see: all these have been gathered together; they have come to you. As I live, says the Lord, you shall be clothed with all these things, as if with an ornament. And like a bride, you shall wrap these things all around you.
19 “Ingawa uliangamizwa na kufanywa ukiwa, na nchi yako ikaharibiwa, sasa nafasi itakuwa finyu kwa ajili ya watu wako, nao wale waliokuangamiza watakuwa mbali sana.
For your deserts, and your solitary places, and the land of your ruination will now be too narrow, because of all the inhabitants. And those who devoured you will be chased far away.
20 Watoto waliozaliwa wakati wa msiba wako bado watakuambia, ‘Mahali hapa ni finyu sana kwetu, tupe eneo kubwa zaidi la kuishi.’
Even the children of your barrenness will say in your ears: “This place is too narrow for me. Make me a spacious place in which to dwell.”
21 Ndipo utasema moyoni mwako, ‘Ni nani aliyenizalia hawa? Nilikuwa nimefiwa, tena tasa; nilikuwa nimehamishwa na kukataliwa. Ni nani aliyewalea hawa? Niliachwa peke yangu, lakini hawa wametoka wapi?’”
And you will say in your heart: “Who has conceived them? I was barren and unable to give birth. I was taken away and held captive. And so, who has raised them? I was destitute and alone. And so, where have they been?”
22 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Tazama, nitawaashiria watu wa Mataifa, nitainua bendera yangu kwa mataifa; watawaleta wana wako mikononi yao, na kuwabeba binti zenu juu ya mabega yao.
Thus says the Lord God: Behold, I will lift up my hand to the Gentiles, and I will exalt my sign before the peoples. And they will carry your sons in their arms, and they will bear your daughters on their shoulders.
23 Wafalme watakuwa baba zenu wa kuwalea, na malkia wao watakuwa mama zenu wa kuwalea. Watasujudu mbele yako nyuso zao zikigusa ardhi; wataramba mavumbi yaliyo miguuni mwako. Ndipo utajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana; wale wanaonitumaini mimi hawataaibika.”
And kings will be your caretakers, and queens will be your nursemaids. They will reverence you with their face to the ground, and they will lick the dust at your feet. And you will know that I am the Lord. For those who hope in him will not be confounded.
24 Je, nyara zaweza kuchukuliwa kutoka kwa mashujaa wa vita, au mateka kuokolewa kutoka kwa watu wakali?
Can prey be taken from the strong? Or is anything taken captive by the powerful able to be saved?
25 Lakini hili ndilo asemalo Bwana: “Naam, mateka watachukuliwa kutoka kwa mashujaa, na nyara zitapokonywa kutoka kwa watu wakali. Nitashindana na wale wanaoshindana nawe, nami nitawaokoa watoto wako.
For thus says the Lord: Certainly, even the captives will be taken away from the strong, even what has been taken by the powerful will be saved. And truly, I will judge those who have judged you, and I will save your children.
26 Nitawafanya wale wanaokuonea kula nyama yao wenyewe, watalewa kwa damu yao wenyewe, kama vile kwa mvinyo. Ndipo wanadamu wote watajua ya kuwa Mimi, Bwana, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
And I will feed your enemies their own flesh. And they will be inebriated with their own blood, as with new wine. And all flesh will know that I am the Lord, who saves you, and your Redeemer, the Strong One of Jacob.