< Isaya 48 >

1 “Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
Poslušajte to, oh hiša Jakobova, ki ste imenovani z imenom Izrael in ste izšli iz Judovih vodá, ki prisegate pri Gospodovem imenu in omenjate Izraelovega Boga, vendar ne v resnici niti ne v pravičnosti.
2 ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
Kajti imenujejo se po svetem mestu in se naslanjajo na Izraelovega Boga; Gospod nad bojevniki je njegovo ime.
3 Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
Razglasil sem prejšnje stvari od začetka in izšle so iz mojih ust in pokazal sem jih; nenadoma sem jih naredil in zgodile so se.
4 Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
Ker sem vedel, da si trdovratna in je tvoj vrat železna kita in tvoja obrv bron,
5 Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
sem ti to celo od začetka razglasil; preden se je zgodilo, sem ti to pokazal, da ne bi rekla: ›Moj malik jih je naredil, moja rezana podoba in moja ulita podoba jim je zapovedala.‹
6 Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
Slišal si, videl si vse to in ali ne boš tega razglasil? Od tega časa sem ti pokazal nove stvari, celo skrite stvari in ti jih nisi poznal.
7 Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
Sedaj so ustvarjene in ne od začetka; celo pred dnevom, ko jih nisi slišal, da ne bi rekel: »Glej, poznal sem jih.«
8 Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
Da, ne slišiš; da, ne poznaš; da, od tistega časa, ko tvoje uho ni bilo odprto, kajti vedel sem, da boš postopal zelo zahrbtno in si bil od maternice imenovan prestopnik.
9 Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
Zaradi svojega imena bom odložil svojo jezo in zaradi svoje hvale se bom zadržal, da te ne odsekam.
10 Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
Glej, prečistil sem te, toda ne s srebrom; izbral sem te v talilni peči stiske.
11 Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
Zaradi sebe, celó zaradi sebe, bom to storil, kajti kako bi bilo moje ime umazano? In svoje slave ne bom dal drugemu.
12 “Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
Prisluhni mi, oh Jakob in Izrael, moj poklicani; jaz sem; jaz sem prvi, jaz sem tudi zadnji.
13 Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
Moja roka je tudi položila temelj zemlji in moja desnica je razpela nebo. Ko kličem k njima, skupaj vstaneta.
14 “Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
Vsi vi, zberite se in poslušajte; kdo izmed njih je razglasil te stvari? Gospod ga je ljubil. Storil bo, kar mu ugaja nad Babilonom in njegov laket bo na Kaldejcih.
15 Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
Jaz, celó jaz, sem govoril. Da, poklical sem ga. Privedel sem ga in svojo pot bo naredil uspešno.
16 “Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
Pridite blizu k meni, poslušajte to; od začetka nisem govoril na skrivnem; od časa, ko je to bilo, tam jaz sem. In sedaj me je poslal Gospod Bog in njegov Duh.«
17 Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
Tako govori Gospod, tvoj Odkupitelj, Sveti Izraelov: »Jaz sem Gospod, tvoj Bog, ki te učim, da boš imel koristi, ki te vodim po poti, po kateri naj bi šel.
18 Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
Oh, da bi prisluhnil mojim zapovedim! Potem bi bil tvoj mir kakor reka in tvoja pravičnost kakor morski valovi.
19 Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
Tudi tvojega semena bi bilo kakor peska in potomstvo tvoje notranjosti podobno njegovemu gramozu; njegovo ime ne bi bilo odrezano niti uničeno izpred mene.
20 Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
Pojdite naprej iz Babilona, pobegnite od Kaldejcev, z glasom petja razglasite, povejte to, izustite to celó do konca zemlje. Recite: › Gospod je odkupil svojega služabnika Jakoba.‹
21 Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
Niso bili žejni, ko jih je vodil skozi puščave. Zanje je vodam veleval, da tečejo iz skale. Razklal je tudi skalo in iz nje so pridrle vode.
22 “Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.
Tam ni miru, « govori Gospod, »zlobnemu.«

< Isaya 48 >