< Isaya 48 >

1 “Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
oJanjiño zao, ry anjomba’ Iakobe, ie tokaveñe ami’ty tahina’ Israele, ry niboak’ ami’ty figoangoa’ Iehodà; o mifanta ami’ty tahina’ Iehovà naho mitalily i Andrianañahare’ Israeleo, fe tsy an-katò, tsy an-kavantañañe.
2 ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
Ie manao ho mpiamy rova miavakey, naho mpiato aman’ Añahare’ Israele, Iehovà’ i Màroy ty tahina’e.
3 Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
Fa nitaroñeko haehae o raha taoloo; eka fa nionjoñe boak’am-bavako ao, nitaroñeko le tsipaepae’e te nifetsake;
4 Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
Amy te napotako t’ie mitangingìñe, naho viñe ty tali-bozìn-kàto’o, Vaho torisìke ty lahara’o;
5 Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
Aa le nivolañako boake taolo añe, ie mbe tsy nitondroke le nitaroñako, tsy mone hatao’o ty hoe; Nihenefa’ i hazomangakoy, naho i sare pinateko an-kataey, vaho, i raha natranakoy ty nandily izay.
6 Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
F’ie nahajanjiñe, heheke iaby o raha zao: aa vaho tsy ho taroñe’ areo? F’ie nitaroñeko raha vao henaneo, raha mietake mbe tsy nifohi’o.
7 Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
Nifonireñe henaneo, fa tsy haehae, tsy nijanjiña’o taolo’ ty andro toy, tsy mone hatao’o ty hoe t’ie nifanta’o.
8 Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
Eka, tsy jinanji’o tsy napota’o; toe tsy nisokake o ravembia’oo haehae izay; fe napotako t’ie hikabo-draha, ihe natao mpiola boak’ an-koviñe ao.
9 Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
Aa le ty añarako ty hampihankàñe o fifombokoo, i fandrengeañe ahiy ty ifoneñako, tsy mone haitoako irehe.
10 Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
Ie hinasohasoko, fa tsy hoe volafoty; nitsoheko an-toñan-kaloviloviañe ao.
11 Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
Izaho, eka izaho, ty hanao izay; fa akore te ho tivaeñe ty añarako? toe tsy hatoloko ami’ty ila’e o engekoo.
12 “Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
Haoño iraho ry Iakobe, ry Israele kinanjiko; Izaho ro Ie, Izaho ty fifotora’e, naho Izaho ty figadoña’e.
13 Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
Eka, nandaharen-tañako ty faha’ ty tane toy, nilamahen-tañako havana o likerañeo; ie tokavako, mitrao-piongake.
14 “Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
Mitontoña, ie iaby, vaho mijanjiña: ia am’ iereo ty nitsey o raha zao? Hanao ty satrin-arofo’e e Bavele añe t’i kokoa’ Iehovà, ie hisenge ty sira’e amo nte-Kasdio.
15 Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
Izaho le Izaho avao ty nivolañe, eka Izaho ty nitoka aze, Izaho ty nanese aze, Ie ty hampiraorao o lala’eo.
16 “Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
Mitotoha amako le janjiño: Boak’ am-baloha’e raho tsy nivolañe añ’etake; ie vaho namoroñe le tao iraho; ie amy zao fa nañirak’ ahy naho i Arofo’ey t’Iehovà Talè
17 Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
Hoe t’Iehovà, Mpijebañe azo, t’i Masi’ Israele; Izaho Iehovà, Andrianañahare’o, I mpañòke azo ho ami’ty hasoa’oy, I mpiaolo azo an-dalan-kombà’oy.
18 Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
Naho ho nihaoñe’ areo o lilikoo! le ho nanahake o oñeo ty fierañeraña’o, vaho hoe onjan-driake ty havantaña’o.
19 Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
Le ho nira amo faseñeo o tiri’oo, o tariram-pañova’oo ami’ty hamaro’ ty haminjilita’e; naho tsy napitsoke ndra naitoañe aoloko ka ty tahina’e.
20 Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
Iakaro i Bavele, Ivoratsaho o nte-Kasdio; am-peo-pisaboañe, tseizo, pazapazaho, koiho pak’ añ’olo’ ty tane toy; Ano ty hoe: Fa jineba’ Iehovà ty mpitoro’e Iakobe.
21 Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
Ie tsy nitaliñiereñe te niaoloa’e hitsake o fatram-beio; Nampipororoaha’e rano i vatoy; tsinera’e i lamilamiy vaho nidoandoañe i ranoy.
22 “Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.
Po-panintsiñañe, hoe t’Iehovà, o tsivokatseo.

< Isaya 48 >