< Isaya 48 >

1 “Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
Ecoutez ceci, maison de Jacob, vous qui êtes appelés du nom d’Israël, et êtes sortis des eaux de Juda, qui jurez au nom du Seigneur, qui vous souvenez du Dieu d’Israël, mais non dans la vérité et la justice.
2 ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
Car ils ont été appelés du nom de la cité sainte, et sur le Dieu d’Israël ils se sont appuyés; le Seigneur des armées est son nom.
3 Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
J’ai annoncé dès lors les événements passés; c’est de ma bouche qu’ils sont sortis et je les ai fait entendre; je les ai accomplis tout d’un coup, et ils sont arrivés.
4 Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
Car je savais que tu es dur, que ton cou est une chaîne de fer, et ton front d’airain.
5 Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
Je t’ai prédit dès lors ces choses; avant qu’elles vinssent je te les ai indiquées, de peur que tu ne dises: Ce sont mes idoles qui les ont faites, et mes images taillées au ciseau et jetées en fonte qui les ont ordonnées.
6 Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
Les choses que tu as entendues, vois-les toutes; mais vous, est-ce que vous les avez annoncées? Je t’en ai fait entendre dès lors de nouvelles; et il en est de réservées que tu ne connais pas;
7 Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
C’est maintenant qu’elles ont été créées, et non pas alors; avant un jour seulement, et tu ne les as pas entendues, de peur que tu ne dises: Voici que moi je les connaissais.
8 Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
Tu n’as entendu, ni connu, ton oreille même alors n’était pas ouverte; car je sais que prévariquant, tu prévariqueras, et je t’ai appelé transgresseur dès le sein de ta mère.
9 Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
À cause de mon nom, j’éloignerai ma fureur, et pour ma gloire je te mettrai un frein, pour que tu ne périsses pas,
10 Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
Je t’ai purifié par le feu, mais non comme l’argent: j’ai choisi pour toi le fourneau de la pauvreté.
11 Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
C’est à cause de moi, à cause de moi que je ferai que mon nom ne soit pas blasphémé, et je ne donnerai pas ma gloire à un autre.
12 “Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
Ecoute-moi, Jacob, et toi, Israël, que j’appelle; moi qui suis, moi le premier, et moi le dernier.
13 Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
Ma main aussi a fondé la terre, et ma droite a étendu les cieux; moi, je les appellerai, et ils seront là tous ensemble.
14 “Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
Rassemblez-vous tous et écoutez-moi: qui d’entre eux a annoncé ces choses? Le Seigneur l’a aimé, il fera sa volonté dans Babylone; et il sera son bras parmi les Chaldéens.
15 Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
C’est moi, c’est moi qui ai parlé, et je l’ai appelé; je l’ai amené, et sa voie est aplanie.
16 “Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
Approchez-vous de moi, et écoutez ceci: dès le principe je n’ai pas parlé en secret; dans le temps même, avant l’événement, j’étais là; et maintenant le Seigneur et son esprit m’ont envoyé.
17 Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
Voici ce que dit le Seigneur ton rédempteur, le saint d’Israël: Moi le Seigneur ton Dieu, je t’enseigne des choses utiles, je te dirige dans la voie par laquelle tu marches.
18 Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
Oh! si tu avais été attentif à mes commandements, ta paix aurait été comme un fleuve, et ta justice comme les flots de la mer;
19 Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
Ta postérité eût été comme le sable de ses rivages, et les rejetons de ton sein comme les petites pierres de ses bords; le nom de la race n’aurait pas péri, et il n’eût pas été effacé de devant ma face.
20 Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
Sortez de Babylone, fuyez de chez les Chaldéens, avec la voix de l’exultation annoncez cette nouvelle, faites-la entendre et portez-la jusqu’aux extrémités de la terre. Dites: Le Seigneur a racheté son serviteur Jacob.
21 Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
Ils n’ont pas eu soif dans le désert, lorsqu’il les ramenait; il fit sortir de l’eau d’une pierre pour eux, et il fendit la pierre et des eaux coulèrent.
22 “Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.
Il n’y a point de paix pour les impies, dit le Seigneur.

< Isaya 48 >