< Isaya 48 >
1 “Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
Ecoutez ceci, maison de Jacob, qui êtes appelés du nom d'Israël, et qui êtes issus des eaux de Juda, qui jurez par le nom de l'Eternel, et qui faites mention du Dieu d'Israël, mais non pas conformément à la vérité, et à la justice.
2 ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
Car ils prennent leur nom de la sainte Cité, et s'appuient sur le Dieu d'Israël, duquel le nom est l'Eternel des armées.
3 Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
J'ai déclaré dès jadis les choses qui ont précédé, et elles sont sorties de ma bouche, et je les ai publiées; je les ai faites subitement, et elles sont arrivées.
4 Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
Parce que j'ai connu que tu étais revêche, et que ton cou était [comme une] barre de fer, et que ton front était d'airain;
5 Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
Je t'ai déclaré ces choses dès lors, et je te les ai fait entendre avant qu'elles arrivassent, de peur que tu ne disses; mes dieux ont fait ces choses, et mon image taillée, et mon image de fonte les ont commandées.
6 Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
Tu l'as ouï, vois tout ceci; et vous, ne l'annoncerez-vous pas? je te fais entendre dès maintenant des choses nouvelles, et qui étaient en réserve, et que tu ne savais pas.
7 Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
Maintenant elles ont été créées, et non pas dès jadis, et avant ce jour-ci tu n'en avais rien entendu, afin que tu ne dises pas; voici, je les savais bien.
8 Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
Encore n'as-tu pas entendu; encore n'as-tu pas connu, et depuis ce temps ton oreille n'a point été ouverte; car j'ai connu que tu agirais perfidement; aussi as-tu été appelé Transgresseur dès le ventre.
9 Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
Pour l'amour de mon Nom je différerai ma colère, et pour l'amour de ma louange je retiendrai mon courroux contre toi, afin de ne te retrancher pas.
10 Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
Voici, je t'ai épuré, mais non pas comme [on épure] l'argent; je t'ai élu au creuset de l'affliction.
11 Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
Pour l'amour de moi, pour l'amour de moi je le ferai; car comment [mon Nom] serait-il profané? certes je ne donnerai point ma gloire à un autre
12 “Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
Ecoute-moi, Jacob, et toi Israël, appelé par moi; c'est moi qui suis le premier, et qui suis aussi le dernier.
13 Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
Ma main aussi a fondé la terre, et ma droite a mesuré les cieux à l'empan; quand je le les appelle, ils comparaissent ensemble.
14 “Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
Vous tous, assemblez-vous, et écoutez; lequel de ceux-là a déclaré de telles choses? l'Eternel l'a aimé, il mettra en exécution son bon plaisir contre Babylone, et son bras sera contre les Chaldéens.
15 Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
C'est moi, c'est moi qui ai parlé, je l'ai aussi appelé, je l'ai amené, et ses desseins lui ont réussi.
16 “Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
Approchez-vous de moi, et écoutez ceci; dès le commencement je n'ai point parlé en secret, au temps que la chose a été faite, j'ai été là. Or maintenant le Seigneur l'Eternel, et son Esprit, m'ont envoyé.
17 Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
Ainsi a dit l'Eternel ton Rédempteur, le Saint d'Israël; je suis l'Eternel ton Dieu, qui t'enseigne à profiter, et qui te guide par le chemin où tu dois marcher.
18 Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
O si tu eusses été attentif à mes commandements! car ta paix eût été comme un fleuve, et ta justice comme les flots de la mer.
19 Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
Et ta postérité eût été [multipliée] comme le sable, et ceux qui sortent de tes entrailles, comme le gravier de la mer; son nom n'eût point été retranché ni effacé de devant ma face.
20 Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
Sortez de Bapylone, fuyez loin des Chaldéens; publiez ceci avec une voix de chant de triomphe, annoncez, publiez ceci, et le mandez dire jusques au bout de la terre; dites, l'Eternel a racheté son serviteur Jacob.
21 Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
Et ils n'ont point eu soif quand il les a fait marcher par les déserts; il leur a fait découler l'eau hors du rocher, même il leur a fendu le rocher, et les eaux en sont découlées.
22 “Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.
Il n'y a point de paix pour les méchants, a dit l'Eternel.