< Isaya 48 >

1 “Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
Ecoutez ceci, maison de Jacob, vous qui êtes appelés du nom d'Israël, et qui êtes sortis de la source de Juda; vous qui jurez par le nom de Yahweh, et qui célébrez le Dieu d'Israël, mais sans sincérité ni droiture.
2 ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
Car ils tirent leur nom de la ville sainte, et ils s'appuient sur le Dieu d'Israël, dont le nom est Yahweh des armées.
3 Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
Dès longtemps, j'ai annoncé les premières choses; elles sortirent de ma bouche; je les proclamai; soudain j'ai agi, et elles sont arrivées.
4 Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
Comme je savais que tu es dur, que ton cou est une barre de fer, et que ton front est d'airain,
5 Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
je t'ai annoncé ces choses il y a longtemps; je te les ai déclarées avant qu'elles n'arrivent, de peur que tu ne dises: " Mon idole les a faites; mon dieu de bois ou de fonte les a ordonnées. "
6 Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
Tu l'as entendu; vois, tout s'est accompli; mais vous, ne le déclarerez-vous pas? Maintenant, je te fais entendre des choses nouvelles, cachées, que tu ne connais point.
7 Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
C'est maintenant qu'elles sont créées, et non auparavant; jusqu'à ce jour, tu n'en avais point entendu parler, de peur que tu ne dises: " Voici, je le savais! "
8 Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
Tu n'en as rien entendu, tu n'en as rien su; jamais ton oreille n'en a rien perçu, parce que je savais que tu es tout à fait infidèle, que ton nom est Prévaricateur dès le sein de ta mère.
9 Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
A cause de mon nom, je retiens ma colère, et à cause de ma gloire, je patiente avec toi, pour ne pas t'exterminer.
10 Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
Voici, je t'ai fondu, mais sans obtenir l'argent; je t'ai éprouvé au creuset de l'affliction.
11 Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
C'est pour l'amour de moi, pour l'amour de moi que je le fais; car comment mon nom serait-il profané? Je ne donnerai pas ma gloire à un autre.
12 “Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
Ecoute-moi, Jacob, et toi, Israël, que j'ai appelé; c'est moi, moi qui suis le premier, moi aussi qui suis le dernier.
13 Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
C'est aussi ma main qui a fondé la terre, et ma droite qui a étendu les cieux; c'est moi qui les appelle, et aussitôt ils se présentent.
14 “Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
Assemblez-vous tous et écoutez: qui d'entre eux a annoncé ces choses? — Celui qu'aime Yahweh accomplira sa volonté dans Babel, et son bras sera contre les Chaldéens. —
15 Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
Moi, moi, j'ai parlé, et je l'ai appelé; je l'ai fait venir, et sa voie sera prospère.
16 “Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
Approchez-vous de moi, entendez ceci: Dès l'origine je n'ai point parlé en cachette; depuis que ces choses arrivent, je suis là; — Et maintenant le Seigneur Yahweh m'envoie avec son Esprit. —
17 Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
Ainsi parle Yahweh, ton rédempteur, le Saint d'Israël: Moi, Yahweh, ton Dieu, je t'enseigne pour ton bien, je te conduis dans le chemin où tu dois marcher.
18 Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
Oh! sois attentif à mes commandements, et ta paix sera comme un fleuve, ta justice comme les flots de la mer;
19 Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
ta postérité sera comme le sable et le fruit de tes entrailles comme les grains de sable; son nom ne sera ni retranché ni effacé devant moi.
20 Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
Sortez de Babylone, fuyez les Chaldéens avec des cris de joie! Publiez-le, proclamez-le, faites-le savoir jusqu'à l'extrémité de la terre! Dites: " Yahweh a racheté son serviteur Jacob!
21 Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
Ils n'ont pas soif dans le désert où il les a conduits; il fait couler pour eux l'eau du rocher; il fend le rocher, et les eaux jaillissent! "
22 “Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.
Il n'y a point de paix pour les méchants, dit Yahweh.

< Isaya 48 >