< Isaya 48 >

1 “Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
Listen to these things, O house of Jacob, you who are called by the name of Israel, and who went forth from the waters of Judah. You swear by the name of the Lord and you call to mind the God of Israel, but not in truth, and not in justice.
2 ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
For they have been called from the holy city, and they have been founded upon the God of Israel. The Lord of hosts is his name.
3 Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
From that time, I announced the former things. They went forth from my mouth, and I have caused them to be heard. I wrought these things suddenly, and they were fulfilled.
4 Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
For I knew that you are stubborn, and that your neck is like an iron sinew, and that your forehead is like brass.
5 Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
From that time, I foretold to you. Before these things happened, I revealed them to you, lest you say: “My idols have accomplished these things, and my graven and molten images have commanded them.”
6 Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
See all the things that you have heard. But were you the ones who announced them? From that time, I caused you to hear about new things, and you do not know how these were preserved.
7 Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
They are created now, and not in that time. And even before today, you did not hear of them; otherwise, you might say, “Behold, I knew them.”
8 Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
You have neither heard, nor known, nor were your ears open in that time. For I knew that you would transgress greatly, and so I called you a transgressor from the womb.
9 Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
For the sake of my name, I will take the face of my fury far away. And for the sake of my praise, I will bridle you, lest you perish.
10 Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
Behold, I have refined you, but not like silver. I have chosen you for the furnace of poverty.
11 Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
For my sake, for my own sake, I will do it, so that I may not be blasphemed. For I will not give my glory to another.
12 “Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
Listen to me, O Jacob, and Israel whom I call. I am the same, I am the first, and I am the last.
13 Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
Also, my hand has founded the earth, and my right hand has measured the heavens. I will call them, and they will stand together.
14 “Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
Gather together, all of you, and listen. Who among them has announced these things? The Lord has loved him; he will do his will with Babylon, and his arm is upon the Chaldeans.
15 Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
I am, I have spoken, and I have called him. I have led him forward, and his way has been straight.
16 “Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
Draw near to me, and listen to this. From the beginning, I have not spoken in secret. From the time before it happened, I was there. And now, the Lord God has sent me, and his Spirit.
17 Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
Thus says the Lord, your Redeemer, the Holy One of Israel: I am the Lord, your God, who teaches you beneficial things, who guides you in the way that you walk.
18 Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
If only you had paid attention to my commandments! Your peace would have been like a river, and your justice would have been like the waves of the sea,
19 Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
and your offspring would have been like the sand, and the stock from your loins would have been like its stones. His name would not have passed away, nor would it have been worn away before my face.
20 Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
Depart from Babylon! Flee from the Chaldeans! Announce it with a voice of exultation. Cause it to be heard, and carry it even to the ends of the earth. Say: “The Lord has redeemed his servant Jacob.”
21 Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
They did not thirst in the desert, when he led them out. He produced water from the rock for them. For he split the rock, and the waters flowed out.
22 “Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.
“There is no peace for the impious,” says the Lord.

< Isaya 48 >