< Isaya 46 >
1 Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama; sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo. Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea, mzigo kwa waliochoka.
Bels grūst, Nebus krīt, viņu tēlus uzliek kustoņiem un lopiem; ko jūs nesat, ir nesama nasta piekusušiem (lopiem).
2 Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini; hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu, wote wanakwenda utumwani pamoja.
Tie visi kopā klūp un krīt, tie nevar izglābt to nastu, bet iet paši cietumā.
3 “Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo, ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba, nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.
Klausies uz Mani, Jēkaba nams, un visi atlikušie no Israēla nama, ko esmu nesis no mātes miesām un uzņēmis no mātes klēpja.
4 Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye, Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi. Nimewahuluku, nami nitawabeba, nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.
Un līdz pašam vecumam Es būšu tas pats, kamēr jūs topat sirmi, Es nesīšu. Es to esmu darījis, un Es jūs uzņemšu, un Es nesīšu un izglābšu.
5 “Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani? Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?
Kam jūs Mani līdzināsiet un turēsiet līdzīgu? Ar ko Mani salīdzināsiet, ka būtu vienādi?
6 Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao, na kupima fedha kwenye mizani; huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu, kisha huisujudia na kuiabudu.
Tie izber zeltu no maka un sver sudrabu ar svaru, tie sader sudraba kalēju, un tas to iztaisa par dievekli, tie metās ceļos un to pielūdz.
7 Huiinua mabegani na kuichukua; huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo. Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale. Ingawa mtu huililia, haimjibu; haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.
Tie to ceļ uz pleciem, to nes, un to noliek savā vietā. Tur viņš stāv un neatstājās no savas vietas; viņu arī piesauc, bet tas neatbild un neviena neizglābj no bēdām.
8 “Kumbukeni hili, litieni akilini, liwekeni moyoni, enyi waasi.
Pieminiet to un turaties stipri, jūs pārkāpēji, ņemiet to pie sirds.
9 Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi.
Pieminiet pagājušās lietas no vecu veciem laikiem; jo Es esmu Dievs, un cits neviens, Es esmu Dievs, un nav neviena kā Es,
10 Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
Kas no iesākuma galu dara zināmu, un no senlaikiem to, kas vēl nav noticis, kas saka: Mans padoms pastāvēs, un Es darīšu visu, kas Man patīk.
11 Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye; kutoka nchi ya mbali, mtu atakayetimiza kusudi langu. Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza; lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
Es aicināju ērgli no rīta puses un vīru pēc Sava padoma no tālas zemes. Es to esmu runājis un tam likšu nākt, Es to esmu apņēmies, Es to arī izdarīšu.
12 Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu, ninyi mlio mbali na haki.
Klausāties uz Mani, cietsirdīgie, kas esat tālu no taisnības.
13 Ninaleta haki yangu karibu, haiko mbali; wala wokovu wangu hautachelewa. Nitawapa Sayuni wokovu, Israeli utukufu wangu.
Es Savu taisnību tuvu esmu atnesis, tā nebūs tālu, un Mana pestīšana nekavēsies, jo Es došu pestīšanu Ciānā, iekš Israēla Savu godību.