< Isaya 46 >

1 Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama; sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo. Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea, mzigo kwa waliochoka.
Bel s'écroule, Nébo s'affaisse; on met leurs images sur des animaux, des bêtes de somme; ces idoles que vous portiez sont chargées, comme un fardeau pesant, sur les bêtes fatiguées.
2 Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini; hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu, wote wanakwenda utumwani pamoja.
Ils s'affaissent, ils s'écroulent ensemble; ils ne peuvent sauver le fardeau; ils s'en vont eux-mêmes en captivité.
3 “Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo, ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba, nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.
Ecoutez-moi, maison de Jacob, et vous tous, reste de la maison d'Israël, vous dont je me suis chargé dès votre naissance, que j'ai portés dès le sein de votre mère.
4 Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye, Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi. Nimewahuluku, nami nitawabeba, nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.
Jusqu'à votre vieillesse je serai le même, jusqu'à vos cheveux blancs je vous soutiendrai. Je l'ai déjà fait, et je vous porterai encore; je vous soutiendrai, je vous délivrerai.
5 “Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani? Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?
A qui me comparerez-vous, et de qui me ferez-vous l'égal? A qui m'assimilerez-vous, que nous soyons pareils?
6 Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao, na kupima fedha kwenye mizani; huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu, kisha huisujudia na kuiabudu.
Ils tirent l'or de leur bourse, et pèsent l'argent à la balance; ils engagent un fondeur afin qu'il en fasse un dieu, et ils se prosternent et adorent.
7 Huiinua mabegani na kuichukua; huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo. Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale. Ingawa mtu huililia, haimjibu; haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.
Ils le portent sur l'épaule, ils le soutiennent, et vont le poser en son lieu; et il s'y tient sans bouger de sa place. Même lorsqu'on crie vers lui, il ne répond pas, il ne sauve personne de la détresse.
8 “Kumbukeni hili, litieni akilini, liwekeni moyoni, enyi waasi.
Pensez à cela et montrez-vous hommes; rebelles, prenez-le à cœur,
9 Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi.
rappelez-vous les choses passées des jours d'autrefois. Oui, moi, je suis Dieu, et il n'y en a point d'autre;
10 Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
je suis Dieu et nul n'est semblable à moi: moi qui, dès le commencement, annonce la fin, et, longtemps à l'avance, ce qui n'est pas encore; qui dis: " Mon dessein subsistera, et je ferai toute ma volonté; "
11 Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye; kutoka nchi ya mbali, mtu atakayetimiza kusudi langu. Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza; lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
qui de l'Orient appelle l'aigle, d'un pays éloigné l'homme de mon dessein. J'ai parlé, j'accomplirai; j'ai résolu, j'exécuterai!
12 Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu, ninyi mlio mbali na haki.
Ecoutez-moi, hommes au cœur opiniâtre, qui êtes loin de la justice.
13 Ninaleta haki yangu karibu, haiko mbali; wala wokovu wangu hautachelewa. Nitawapa Sayuni wokovu, Israeli utukufu wangu.
Je fais approcher ma justice; elle n'est pas loin, et mon salut ne tardera pas; je donnerai le salut à Sion, ma gloire à Israël.

< Isaya 46 >