< Isaya 46 >
1 Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama; sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo. Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea, mzigo kwa waliochoka.
Bel s'incline. Nebo se baisse. Leurs idoles sont portées par des animaux, et sur le bétail. Les choses que vous avez transportées sont des charges lourdes, un fardeau pour ceux qui sont fatigués.
2 Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini; hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu, wote wanakwenda utumwani pamoja.
Ils s'abaissent et se prosternent ensemble. Ils ne pouvaient pas délivrer le fardeau, mais ils sont partis en captivité.
3 “Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo, ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba, nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.
« Écoutez-moi, maison de Jacob, et tout le reste de la maison d'Israël, qu'ils portent depuis leur naissance, qui ont été portés depuis l'utérus.
4 Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye, Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi. Nimewahuluku, nami nitawabeba, nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.
Je suis lui même jusqu'à la vieillesse, et même jusqu'aux cheveux blancs, je te porterai. J'ai fait, et je supporterai. Oui, je vais porter, et je vais livrer.
5 “Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani? Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?
« A qui me comparerez-vous, et me considérerez-vous comme mon égal? et me comparer, comme si nous étions pareils?
6 Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao, na kupima fedha kwenye mizani; huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu, kisha huisujudia na kuiabudu.
Certains versent l'or du sac, et peser l'argent dans la balance. Ils engagent un orfèvre, et il en fait un dieu. Ils tombent... Oui, ils adorent.
7 Huiinua mabegani na kuichukua; huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo. Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale. Ingawa mtu huililia, haimjibu; haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.
Ils le portent sur leur épaule. Ils le portent, le mettent à sa place, et il reste là. Il ne peut pas bouger de sa place. Oui, on peut crier vers elle, mais elle ne peut pas répondre. Cela ne peut pas le sauver de ses problèmes.
8 “Kumbukeni hili, litieni akilini, liwekeni moyoni, enyi waasi.
« Souvenez-vous de cela, et montrez-vous des hommes. Rappelez-le encore une fois, vous les transgresseurs.
9 Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi.
Souviens-toi des choses anciennes; car je suis Dieu, et il n'y en a pas d'autre. Je suis Dieu, et il n'y a personne comme moi.
10 Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
Je déclare la fin dès le commencement, et depuis les temps anciens des choses qui ne sont pas encore faites. Je le dis: Mon conseil sera maintenu, et je ferai tout ce qui me plaît.
11 Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye; kutoka nchi ya mbali, mtu atakayetimiza kusudi langu. Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza; lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
J'appelle un oiseau vorace de l'est, l'homme de mon conseil d'un pays lointain. Oui, j'ai parlé. Je le ferai aussi passer. J'ai tout prévu. Je le ferai aussi.
12 Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu, ninyi mlio mbali na haki.
Écoutez-moi, vous qui vous obstinez, qui sont loin de la justice!
13 Ninaleta haki yangu karibu, haiko mbali; wala wokovu wangu hautachelewa. Nitawapa Sayuni wokovu, Israeli utukufu wangu.
Je fais approcher ma justice. Ce n'est pas loin, et mon salut n'attendra pas. J'accorderai le salut à Sion, ma gloire à Israël.