< Isaya 46 >

1 Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama; sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo. Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea, mzigo kwa waliochoka.
Bel sinketh down; Nebo falleth; Their images are laid upon beasts and cattle; Those that ye once bore are packed upon them; A burden to the weary beast!
2 Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini; hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu, wote wanakwenda utumwani pamoja.
They sink down; they fall together; They cannot rescue the burden; They themselves go into captivity.
3 “Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo, ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba, nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.
Hearken to me, O house of Jacob, And all the remnant of the house of Israel; Ye that have been borne by me from your birth, That have been carried by me from your earliest breath!
4 Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye, Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi. Nimewahuluku, nami nitawabeba, nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.
Even to your old age I am the same; Even to hoar hairs I will carry you; I have done it, and I will still bear you; I will carry, and will deliver you.
5 “Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani? Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?
To whom will ye liken me, and compare me? Yea, to whom will ye compare me, that we may be like?
6 Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao, na kupima fedha kwenye mizani; huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu, kisha huisujudia na kuiabudu.
They lavish gold out of the bag, And weigh silver in the balance; They hire a goldsmith, and he maketh it a god; They fall down, yea, they worship it.
7 Huiinua mabegani na kuichukua; huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo. Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale. Ingawa mtu huililia, haimjibu; haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.
They lift him upon the shoulder, and carry him; They set him in his place, and there he standeth; From his place he moveth not; Yea, one may cry to him, yet doth he not answer, Nor save him out of his distress.
8 “Kumbukeni hili, litieni akilini, liwekeni moyoni, enyi waasi.
Remember these things, and show yourselves men; Lay them to heart, ye apostates!
9 Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi.
Remember the former things in ancient times! For I am God, and there is none else; I am God, and there is none like me.
10 Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
Declaring the end from the beginning; From ancient times the things that were not yet done; Saying, My purpose shall stand, And I will do all my pleasure;
11 Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye; kutoka nchi ya mbali, mtu atakayetimiza kusudi langu. Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza; lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
Calling from the East the eagle, The man that executeth my purpose from a far country; I have spoken it, I will also bring it to pass; I have purposed it, I will also do it.
12 Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu, ninyi mlio mbali na haki.
Hearken to me, ye stubborn-hearted, That are far from deliverance!
13 Ninaleta haki yangu karibu, haiko mbali; wala wokovu wangu hautachelewa. Nitawapa Sayuni wokovu, Israeli utukufu wangu.
I have brought near my deliverance; it is not far off; My salvation shall not tarry; I will give to Zion salvation, To Israel, my glory.

< Isaya 46 >