< Isaya 46 >

1 Beli anasujudu hadi nchi, Nebo anainama; sanamu zao zabebwa na wanyama wa mizigo. Vinyago hivi mnavyobeba kila mahali ni mzigo wa kulemea, mzigo kwa waliochoka.
Bel is bowed down, Nebo sinketh, their idols are [delivered] unto the beasts, and unto the cattle; those which were once carried by you are now laden up a burden to the weary beasts.
2 Vinyago pamoja na wale wanaovibeba wanainama chini; hiyo miungu haiwezi kuwaokoa watu, wote wanakwenda utumwani pamoja.
They are sunk, they are bowed down together; they could not deliver the burden, but they themselves are gone into captivity.
3 “Nisikilizeni mimi, ee nyumba ya Yakobo, ninyi nyote mliobaki wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao nimewategemeza tangu mlipotungwa mimba, nami nimewabeba tangu kuzaliwa kwenu.
Hearken unto me, O house of Jacob, and all the remnant of the house of Israel, who are borne [by me] from their birth, who are carried from the womb;
4 Hata mpaka wakati wa uzee wenu na mvi, Mimi ndiye, Mimi ndiye nitakayewasaidia ninyi. Nimewahuluku, nami nitawabeba, nitawasaidia ninyi na kuwaokoa.
And even unto old age I am the same; and even unto the time of hoary hairs will I bear: l have done it, and I will carry [you]; even I will bear, and deliver you.
5 “Mtanilinganisha na nani, au mtanihesabu kuwa sawa na nani? Ni nani mtakayenifananisha naye ili tuweze kulinganishwa?
To whom will ye liken and assimilate me, and compare me, that we may be like?
6 Wengine humwaga dhahabu kutoka kwenye mifuko yao, na kupima fedha kwenye mizani; huajiri mfua dhahabu kutengeneza mungu, kisha huisujudia na kuiabudu.
[There are those] that lavish gold out of the bag, and weigh silver in the balance; that hire a melter, that he may make of it a god; they [then] bend the knee, yea, they bow themselves down;
7 Huiinua mabegani na kuichukua; huiweka mahali pake, papo hapo ndipo isimamapo. Wala haiwezi kusogea kutoka mahali pale. Ingawa mtu huililia, haimjibu; haiwezi kumwokoa kwenye taabu zake.
They carry him, upon the shoulder they bear him, and set up him in his spot, and he remaineth standing, from his place he doth not move: yea, though one should cry unto him, he cannot answer, out of his trouble he cannot help him.
8 “Kumbukeni hili, litieni akilini, liwekeni moyoni, enyi waasi.
Remember this, and take courage: take it again to heart, O ye transgressors.
9 Kumbukeni mambo yaliyopita, yale ya zamani za kale; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine; mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi.
Remember the former things of olden times; for I am God, and there is no one else; I am God, and there is nothing like me.
10 Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
Declaring from the beginning the end, and from the earliest days the things that have not yet been done, saying, My counsel shall stand firm, and all my pleasure will I do:
11 Kutoka mashariki ninaita ndege awindaye; kutoka nchi ya mbali, mtu atakayetimiza kusudi langu. Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza; lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda.
Calling from the east the eagle, from a far-off country the man of my counsel; yea, I have spoken it, I will also bring it to pass; I have purposed it, I will also execute it.
12 Nisikilizeni, ninyi wenye mioyo migumu, ninyi mlio mbali na haki.
Hearken unto me, ye stout of heart, that are far from righteousness:
13 Ninaleta haki yangu karibu, haiko mbali; wala wokovu wangu hautachelewa. Nitawapa Sayuni wokovu, Israeli utukufu wangu.
I have brought near my righteousness; it shall not be far off, and my salvation shall not tarry: and I will grant unto Zion salvation, unto Israel my glory.

< Isaya 46 >