< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
Bet nu Tas Kungs, tavs Radītājs, Jēkab, un tavs darītājs, Israēl, saka tā: nebīsties, jo Es tevi esmu atpestījis, Es tevi esmu saucis pie tava vārda; tu esi Mans.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
Kad tu iesi caur ūdeņiem, tad Es būšu pie tevis, un caur upēm, tad tās tevi nepārplūdīs. Kad tu iesi caur uguni, tad tu nesadegsi, un liesma tevi neaizdedzinās.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
Jo Es esmu Tas Kungs, tavs Dievs, tas Svētais iekš Israēla, tavs Pestītājs. Ēģipti Es dodu par tavu izpirkšanas maksu, Moru zemi un Sabu tavā vietā.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Tāpēc ka tu esi dārgs Manās acīs un cienīgs, un Es tevi mīļoju, Es esmu devis cilvēkus tavā vietā un tautas par tavu dvēseli.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Nebīsties, jo Es esmu pie tevis, Es atvedīšu tavu dzimumu no rīta puses un tevi sapulcināšu no vakara puses.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
Es sacīšu uz ziemeli: Dod šurp! Un uz dienvidu: Neaiztur! Atved Manus dēlus no tālienes un Manas meitas no zemes galiem,
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
Ikkatru, kas pēc Mana Vārda nosaukts, un ko Es esmu radījis Sev par godu, ko esmu taisījis un darījis.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Atved tos aklos ļaudis, kam tomēr acis, un tos kurlos, kam tomēr ausis.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
Lai visi pagāni top sapulcināti, un tautas lai sanāk kopā. Kurš no tiem to stāstīs? Lai tie mums stāsta tās pagājušās lietas, lai tie atved savus lieciniekus un taisnojās, ka šie dzird un saka: Tas ir tiesa.
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
Jūs esat Mani liecinieki, saka Tas Kungs, un Mans kalps, ko esmu izredzējis, lai jūs atzīstat un Man ticat un saprotat, ka Es tas esmu. Priekš Manis neviens dievs nav bijis un pēc Manis neviens nebūs.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
Es, Es esmu Tas Kungs, un Pestītāja nav kā vien Es.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
Es esmu pasludinājis, Es esmu palīdzējis, Es esmu zināmu darījis, un sveša(dieva) nebija jūsu starpā. Un jūs esat Mani liecinieki, saka Tas Kungs, ka Es esmu Dievs.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
Arī no šīs dienas Es esmu tas pats, un neviena nav, kas var izglābt no Manas rokas; ko Es daru, kas to var novērst?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Tā saka Tas Kungs, jūsu Pestītājs, tas Svētais iekš Israēla: jūsu dēļ Es uz Bābeli esmu sūtījis un visus Kaldejus aizdzinis, ka bija jābēg ar tām laivām, ar kurām bija līksmojušies.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
Es esmu Tas Kungs, jūsu Svētais, Israēla Radītājs, jūsu ķēniņš!
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Tā saka Tas Kungs, kas ceļu darījis jūrā un teku stipros ūdeņos,
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
Kas izved ratus un zirgus, kara pulku un spēku, - kopā tie ir apgūlušies, tie necelsies atkal augšām, tie ir izdzēsti, kā dakts tie ir izdzisuši.
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Nepieminiet tās vecās lietas un nedomājiet vairs uz to, kas pagājis.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Redzi, Es daru jaunas lietas; jau plaukst, jūs to atzīsiet; Es darīšu ceļu tuksnesī un upes tukšās vietās.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
Zvēri laukā Mani godās, šakāļi un strausi, jo Es ūdeni došu tuksnesī un upes tukšā vietā, dzirdināt Savus ļaudis, Savus izredzētos.
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
Šos ļaudis Es Sev esmu radījis, tie teiks Manu slavu.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
Un tu Mani neesi piesaucis, Jēkab, nedz Manis pēc pūlējies, Israēl!
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Tu Man neesi atnesis savu dedzināmo upuru avis, nedz Mani godājis ar saviem kaujamiem upuriem. Es tevi neesmu kalpinājis ar ēdamiem upuriem, nedz tevi apgrūtinājis ar vīraku.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Tu Man neesi par naudu pircis smaržīgas kalmes un neesi Mani mielojis ar savu upuru taukiem. Bet tu Mani esi kalpinājis ar saviem grēkiem, tu Mani esi apgrūtinājis ar saviem noziegumiem.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
Es, Es tas esmu, kas izdeldu tavus pārkāpumus Sevis dēļ un nepieminu tavus grēkus.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Atgādini Mani, lai mēs kopā tiesājamies, teic jel, kā tu vari taisnoties.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Tavs pirmais tēvs ir grēkojis un tavi aizstāvētāji pret Mani noziegušies.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
Tāpēc Es esmu licis negodā svētuma virsniekus un Jēkabu nodevis lāstam un Israēli kaunam.

< Isaya 43 >