< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
Et maintenant, voici ce que dit le Seigneur, qui t’a créé, ô Jacob, et qui ta formé, ô Israël: Ne crains point, parce que je t’ai racheté, et appelé par ton nom; tu es mien, toi.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
Lorsque tu passeras au travers des eaux, je serai avec toi, et les fleuves ne te submergeront pas; lorsque tu marcheras dans le feu, tu ne seras pas brûlé; et la flamme n’aura pas d’ardeur pour toi;
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
Parce que je suis le Seigneur ton Dieu, le saint d’Israël, ton Sauveur; j’ai donné pour toi, afin de t’être propice, l’Egypte, l’Ethiopie et Saba.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Depuis que tu es devenu honorable à mes yeux et glorieux, moi, je t’ai aimé; je donnerai des hommes pour toi, et des peuples pour ton âme.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Ne crains point, parce que moi je suis avec toi; de l’Orient je ramènerai ta race; et de l’Occident je te rassemblerai.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
Je dirai à l’aquilon: Donne; et au midi: Ne retiens pas; amène mes fils de loin, et mes filles des extrémités de la terre.
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
Car quiconque invoque mon nom, je l’ai créé pour ma gloire, je l’ai formé, et je l’ai fait.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Fais sortir un peuple aveugle et qui a des yeux; sourd, et il a des oreilles.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
Toutes les nations se sont réunies ensemble, et des tribus se sont liées; qui parmi vous annoncera cela, et nous fera entendre les choses qui furent les premières? qu’ils produisent leurs témoins, qu’ils se justifient, et qu’ils entendent, et qu’ils disent: C’est vrai.
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
Vous êtes mes témoins, dit le Seigneur, vous et mon serviteur que j’ai choisi; afin que vous sachiez, que vous me croyiez, et que vous compreniez que c’est moi-même qui suis. Avant moi il n’y a pas eu de Dieu formé, et après moi il n’y en aura pas.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
C’est moi qui suis, c’est moi qui suis le Seigneur; et il n’y a pas, hors moi, de sauveur.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
C’est moi qui ai annoncé, et qui ai sauvé; j’ai fait entendre, et il n’y a pas eu parmi vous d’étranger; vous êtes mes témoins, dit le Seigneur, et moi, je suis Dieu.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
Et dès le commencement je suis, et il n’y a personne qui arrache de ma main; j’agirai, et qui m’en détournera?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Voici ce que dit le Seigneur, votre rédempteur, le saint d’Israël: À cause de vous j’ai envoyé à Babylone, et j’ai arraché toutes ses barres, et les Chaldéens qui se glorifiaient dans leurs vaisseaux.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
Je suis le Seigneur, votre saint, le créateur d’Israël, votre roi.
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Voici ce que dit le Seigneur, qui a fait dans la mer une voie, et au milieu des eaux impétueuses un sentier.
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
Qui a fait sortir le quadrige et le cheval, l’armée et le fort; ils se sont endormis ensemble, ils ne se relèveront pas; ils ont été brisés comme le lin, et ils se sont éteints.
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Ne vous souvenez plus des choses passées, et les anciennes, ne les regardez pas.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Voici que moi je fais des choses nouvelles; c’est maintenant qu’elles paraîtront; certainement vous les connaîtrez; je ferai dans le désert une voie, et dans un chemin impraticable des fleuves.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
La bête des champs me glorifiera, ainsi que les dragons et les autruches, parce que j’ai mis dans le désert des eaux, des fleuves dans un chemin impraticable, afin de donner à boire à mon peuple, à mon élu.
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
J’ai formé ce peuple pour moi; il publiera ma louange.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
Cependant tu ne m’as pas invoqué, Jacob, et tu n’as pas travaillé pour moi, Israël.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Tu ne m’as pas offert ton bélier d’holocauste, et par tes victimes tu ne m’as pas glorifié; je ne t’ai pas forcé à me faire des oblations, et je ne t’ai pas donné la peine de m’offrir de l’encens.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Tu ne m’as pas acheté avec ton argent de canne odorante, et de la graisse de tes victimes tu ne m’as pas rassasié; mais tu m’as rendu ton esclave par tes péchés; tu m’as donné du mal par tes iniquités.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
C’est moi, c’est moi-même qui efface tes iniquités à cause de moi; et de tes péchés je ne me souviendrai pas.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Remets-moi en mémoire, et plaidons ensemble; raconte, si tu as quelque chose pour te justifier.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Ton père le premier a péché, et tes interprètes ont prévariqué contre moi.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
C’est pourquoi j’ai déclaré souillés les princes saints; j’ai livré Jacob à la tuerie, et Israël à l’outrage.

< Isaya 43 >