< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
Or maintenant, ainsi a parlé l’Eternel, ton Créateur, ô Jacob, ton Auteur, ô Israël! Ne crains rien car je vais te libérer; je t’ai appelé par ton nom, tu es à moi!
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
Quand tu passeras par les eaux, je serai avec toi; par les torrents, ils ne te submergeront pas; quand tu marcheras à travers le feu, tu ne seras pas brûlé; à travers la flamme, elle n’aura point prise sur toi.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
C’Est que je suis l’Eternel, ton Dieu, le Saint d’Israël, ton défenseur. Je donne l’Egypte pour ta rançon, Couch et Seba en échange de toi.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Parce que tu es cher à mes yeux et digne d’estime, parce que je t’aime, je livre des hommes à ta place, et des peuples pour racheter ta personne.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Ne crains point, je suis avec toi! Du Levant je ramènerai tes enfants et du Couchant je te rassemblerai.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
Je dirai au Nord: "Donne!" au Midi: "Ne les retiens pas! Ramène des pays lointains mes fils, et des confins de la terre mes filles,
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
tous ceux qui se réclament de mon nom, tous ceux que, pour ma gloire, j’ai créés, formés, organisés."
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Laissez sortir ce peuple qui était aveugle, quoiqu’il eût des yeux, et sourd, quoiqu’il eût des oreilles!
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
Que tous les peuples se réunissent ensemble, que les nations se groupent! Qui d’entre eux est capable d’annoncer ces choses, de nous communiquer les prédictions de jadis? Qu’ils produisent leurs témoins et qu’ils se justifient, afin qu’on les entende et qu’on dise: "C’Est vrai!"
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
Vous, vous êtes mes témoins, dit l’Eternel, et le serviteur choisi par moi pour reconnaître, pour croire en moi et être convaincu que moi je suis; qu’avant moi, nul Dieu n’a existé, et qu’après moi, il n’y en aura point.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
C’Est moi, moi, l’Eternel, et en dehors de moi il n’est point de sauveur.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
C’Est moi qui ai fait les révélations, opéré le salut, annoncé les événements, aucun dieu étranger ne s’est manifesté parmi vous. Vous êtes donc mes témoins, dit l’Eternel, comme je suis votre Dieu.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
Oui, dès l’origine des jours, je suis le même, personne ne saurait sauver de ma main; mon action, qui peut l’entraver?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Ainsi parle l’Eternel, votre libérateur, le Saint d’Israël: "En votre faveur, j’ai envoyé un mandataire à Babylone. Je les ai jetés bas, tous ont recours à la fuite, les Chaldéens gagnent les vaisseaux qu’ils prônaient.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
Je suis l’Eternel, votre Saint, le Créateur d’Israël, votre roi.
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Ainsi parle l’Eternel, qui trace un chemin dans la mer, une route à travers les eaux impétueuses,
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
qui fait sortir chars et coursiers, une armée puissante; tous ensemble ils se sont couchés pour ne plus se relever, ils se sont consumés et éteints comme un lumignon:
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
"Ne rappelez plus les événements passés, ne méditez pas sur les temps antiques.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Voici, je vais créer des choses nouvelles, déjà elles éclosent: ne les remarquez-vous pas? Oui, je vais établir un chemin dans le désert et des cours d’eau dans l’aride solitude.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
Les bêtes des champs me rendent hommage chacals et autruches parce que je mets de l’eau dans le désert, des rivières dans la solitude aride, afin de fournir à boire au peuple de mon choix.
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
Ce peuple, je l’ai formé pour moi, pour qu’il publie ma gloire.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
Et pourtant ce n’est pas moi que tu as invoqué, Jacob! Non, tu t’es lassé de moi, Israël!
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Ce n’est pas à moi que tu as apporté l’agneau de tes holocaustes, ni moi que tu as honoré de tes sacrifices; je ne t’ai point importuné pour des oblations, ni excédé pour de l’encens.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Tu n’as pas, à prix d’argent, acheté pour moi des aromates, tu ne m’as pas saturé de la graisse de tes victimes. En revanche, tu m’as importuné par tes péchés, excédé par tes iniquités.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
Et c’est moi, moi-même qui efface tes péchés, par égard pour moi, et tes fautes, je ne veux plus m’en souvenir.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Fais appel à ma mémoire, discutons ensemble! Prends, toi, la parole, afin d’obtenir gain de cause!
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Déjà ton premier aïeul a failli et tes intercesseurs m’ont été infidèles.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
Je devrais donc réprouver ces princes du sanctuaire, vouer Jacob à l’anathème et Israël aux outrages.

< Isaya 43 >