< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
Et maintenant, ainsi parle Yahweh, celui qui t’a créé, ô Jacob, celui qui t’a formé, ô Israël: Ne crains point, car je t’ai racheté; je t’ai appelé par ton nom, tu es à moi!
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
Quand tu passeras par les eaux, je serai avec toi; par les fleuves, ils ne t’engloutiront point; quand tu marcheras au milieu du feu, tu ne seras point brûlé et la flamme ne t’embrasera point.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
Car moi, Yahweh, je suis ton Dieu; le Saint d’Israël est ton sauveur. J’ai donné l’Égypte pour ta rançon; l’Éthiopie et Saba en échange de toi.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Parce que tu es précieux à mes yeux, honorable, et que, moi, je t’aime, je donnerai des hommes en échange de toi, et des peuples en échange de ta vie.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Ne crains point, car je suis avec toi; de l’orient je ramènerai ta postérité, et de l’occident je te rassemblerai.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
Je dirai au septentrion: « Donne- les! » et au midi: « Ne les retiens pas! Ramène mes fils des pays lointains et mes filles de l’extrémité de la terre,
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
tous ceux qui portent mon nom, que j’ai créés pour ma gloire, que j’ai formés et que j’ai faits.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Fais sortir le peuple aveugle, et qui a des yeux, et les sourds, qui ont des oreilles. »
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
Que les nations s’assemblent toutes, et que les peuples se réunissent! Lequel d’entre eux a annoncé ces choses, et nous a fait entendre des prédictions anciennes? Qu’ils produisent leurs témoins et qu’ils se justifient; qu’on les entende et qu’on dise: « C’est vrai! »
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
Vous êtes mes témoins, — oracle de Yahweh, et mon serviteur que j’ai choisi, afin que vous reconnaissiez et que vous me croyiez, et que vous compreniez que c’est moi. Avant moi aucun Dieu n’a été formé, et il n’y en aura point après moi.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
C’est moi, moi qui suis Yahweh, et il n’y a point de sauveur en dehors de moi.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
C’est moi qui ai annoncé, qui ai sauvé, qui ai prédit; ce n’est pas un dieu étranger parmi vous; et vous êtes mes témoins, — oracle de Yahweh! C’est moi qui suis Dieu;
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
désormais aussi je le suis, et il n’y a personne qui délivre de ma main; j’agirai, et qui l’empêchera?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Ainsi parle Yahweh, votre rédempteur, le Saint d’Israël: À cause de vous, j’ai envoyé contre Babylone, et je les fais tous descendre en fugitifs, les Chaldéens, sur les navires dont ils sont si fiers!
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
Je suis Yahweh, votre Saint, le Créateur d’Israël, votre roi!
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Ainsi parle Yahweh, qui ouvrit un chemin dans la mer, un sentier dans les eaux puissantes;
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
qui mit en campagne chars et chevaux, armée et vaillants guerriers, — tous ensemble ils sont couchés pour ne plus se relever; ils ont été étouffés, ils se sont éteints comme une mèche: —
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Ne vous souvenez plus des événements passés, et ne considérez plus les choses d’autrefois!
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Voici que je vais faire une merveille nouvelle; elle est près d’éclore; ne la reconnaîtrez-vous pas? Je mettrai un chemin dans le désert, des fleuves dans la terre aride.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
Les bêtes des champs me glorifieront, les chacals et les autruches. Car je mettrai des eaux dans le désert, et des fleuves dans la terre aride, pour abreuver mon peuple, mon élu,
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
le peuple que j’ai formé pour moi, qui publiera ma louange.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
Cependant tu ne m’as pas invoqué, ô Jacob, et tu ne t’es pas mis en peine pour moi, Israël.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Tu ne m’as pas offert les brebis de tes holocaustes, et tu ne m’as pas honoré par tes sacrifices. Je ne t’ai pas été à charge pour des offrandes, et ne t’ai pas fatigué pour de l’encens.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Tu ne m’as point, à prix d’argent, acheté de roseau odoriférant, et tu ne m’as pas rassasié de la graisse de tes victimes; mais toi, tu m’as été à charge par tes péchés, tu m’as fatigué par tes iniquités.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
C’est moi, c’est moi qui efface tes fautes pour l’amour de moi, et je ne me souviendrai plus de tes péchés.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Réveille mes souvenirs, plaidons ensemble, parle toi-même pour te justifier.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Ton premier père a péché, et tes interprètes m’ont été infidèles.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
C’est pourquoi j’ai dégradé les princes du sanctuaire, j’ai livré Jacob à l’anathème et Israël aux outrages.

< Isaya 43 >