< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
But now this is what Yahweh says, he who created you, Jacob, and he who formed you, Israel: “Do not be afraid, for I have redeemed you; I have called you by your name, you are mine.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
When you pass through the waters, I will be with you; and through the rivers, they will not overwhelm you. When you walk through the fire you will not be burned, and the flames will not destroy you.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
For I am Yahweh your God, the Holy One of Israel, your Savior. I have given Egypt as your ransom, Cush and Seba in exchange for you.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Since you are precious and special in my sight, I love you; therefore I will give people in exchange for you, and other peoples in exchange for your life.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Do not be afraid, for I am with you; I will bring your offspring from the east, and gather you from the west.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
I will say to the north, 'Hand them over;' and to the south, 'Do not hold any back;' Bring my sons from afar, and my daughters from the remote regions of the earth,
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
everyone who is called by my name, whom I have created for my glory, whom I have formed, yes, whom I have made.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Bring out the people who are blind, even though they have eyes, and the deaf, even though they have ears.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
All the nations gather together, and the peoples assemble. Who among them could have declared this and announced to us earlier events? Let them bring their witnesses to prove themselves right, let them listen and affirm, 'It is true.'
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
You are my witnesses,” declares Yahweh, “and my servant whom I have chosen, so that you may know and believe in me, and understand that I am he. Before me there was no god formed, and there will be none after me.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
I, I am Yahweh, and there is no savior but me.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
I have declared, saved, and proclaimed, and there is no other god among you. You are my witnesses,” declares Yahweh, “I am God.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
From this day on I am he, and no one can rescue anyone from my hand. I act, and who can turn it back?”
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
This is what Yahweh says, your Redeemer, the Holy One of Israel: “For your sake I send to Babylon and lead them all down as fugitives, turning the Babylonians' expressions of joy into songs of lamentation.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
I am Yahweh, your Holy One, the Creator of Israel, your King.”
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
This is what Yahweh says (who opened a way through the sea and a path in the mighty waters,
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
who led out the chariot and horse, the army and the mighty host. They fell down together; they will never rise again; they are extinguished, quenched like a burning wick.)
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
“Do not think about these former things, nor consider the things of long ago.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Look, I am about to do a new thing; now it begins to happen; do you not perceive it? I will make a road in the desert and streams of water in the wilderness.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
The wild animals of the field will honor me, the jackals and the ostriches, because I give water in the wilderness, and rivers in the desert, for my chosen people to drink,
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
this people whom I formed for myself, that they might recount my praises.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
But you have not called on me, Jacob; you have become tired of me, Israel.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
You have not brought me any of your sheep as burnt offerings, or honored me with your sacrifices. I have not burdened you with grain offerings, nor wearied you with demands for incense.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
You have bought me no sweet-smelling cane with money, neither have you poured out to me the fat of your sacrifices; but you have burdened me with your sins, you have wearied me with your evil deeds.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
I, yes, I, am he who blots out your offenses for my own sake; and I will not call to mind your sins any longer.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Remind me of what happened. Let us debate together; present your cause, that you may be proved innocent.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Your first father sinned, and your leaders have transgressed against me.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
Therefore I will defile the holy officials; I will hand Jacob over to complete destruction, and Israel to abusive humiliation.”

< Isaya 43 >