< Isaya 43 >
1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
But now thus hath said the Lord that created thee, O Jacob, and he that formed thee, O Israel, Fear not; for I have redeemed thee, I have called thee by thy name; mine art thou.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
Whenever thou passest through the waters, I am with thee; and through the rivers, —they shall not overflow thee: whenever thou walkest through the fire, thou shalt not be scorched; neither shall the flame burn on thee.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
For I am the Lord thy God, the Holy One of Israel, thy Saviour; I have given Egypt for thy ransom, Cush and Seba in place of thee.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Since thou art precious in my eyes, art honorable, and I indeed do love thee: therefore will I give men in place of thee, and nations instead of thy soul.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Fear not, for I am with thee; from the east will I bring thy seed, and from the west will I gather thee.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
I will say to the north, Give up; and to the south, Withhold not: bring my sons from afar, and my daughters from the ends of the earth;
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
Every one that is called by my name, and whom I have created for my glory; whom I have formed; yea, whom I have made.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Bring forward the blind people that have eyes, and the deaf that have ears.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
Let all the nations be gathered together, and let the people be assembled: who among them can announce this? and cause us to hear former things? let them bring forth their witnesses, that they may be justified: or let them hear, and say, It is truth.
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
Ye are my witnesses, saith the Lord, and my servant whom I have chosen: in order that ye may know and believe me, and understand, that I am he; before me there was no god formed, and after me there will be none.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
I, I am the Lord; and beside me there is no saviour.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
I myself have announced it, and I have saved, and I have let it be heard, and there was no strange [god] among you; and ye are my witnesses, saith the Lord, and I am God.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
Yea, from the [first] day am I he; and there is none that can deliver out of my hand: if I will work, is there one that can hinder it?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Thus hath said the Lord, the Holy One of Israel, For your sake did I send to Babylon, and in swift vessels brought I them all down, and the Chaldeans, in the ships of their joyful song.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
I am the Lord, the Holy One, the Creator of Israel, your King.
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Thus hath said the Lord, who maketh a way in the sea, and a path in the mighty waters;
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
Who bringeth forth chariot and horse, army and power: together shall they lie down, they shall not rise up again; they are extinct, like a wick are they quenched.
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Remember not the former things, and ancient events regard no more.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Behold, I will do a new thing; now shall it spring forth; will ye not acknowledge it? I will even make in the wilderness a way, and in the desert rivers.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
The beasts of the field shall honor me, the monsters and the ostriches; because I give waters in the wilderness, rivers in the desert, to give drink to my people, my elect;
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
This people which I have formed for myself; my praise shall they relate.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
But on me hast thou not called, O Jacob; for thou art become weary of me, O Israel.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Thou hast not brought unto me the lamb of thy burnt-offerings; and with thy sacrifices hast thou not honored me: I have not troubled thee with meat-offerings, nor wearied thee with frankincense.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Thou hast not bought for me sweet cane, and with the fat of thy sacrifices hast thou not satisfied me; but thou hast troubled me with thy sins, thou hast wearied me with thy iniquities.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
I, it is I that blot out thy transgressions for my own sake, and thy sins I will not remember.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Put me in remembrance; let us plead together: relate thou, in order that thou mayest be justified.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Thy first father did sin, and they that plead for thee transgressed against me.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
Therefore do I profane the holy princes, and I give up Jacob to the curse, and Israel to reproaches.