< Isaya 43 >
1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
But nowe thus sayeth the Lord, that created thee, O Iaakob: and hee that formed thee, O Israel, Feare not: for I haue redeemed thee: I haue called thee by thy name, thou art mine.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
When thou passest through the waters, I wil be with thee, and through the floods, that they doe not ouerflowe thee. When thou walkest through the very fire, thou shalt not be burnt, neither shall the flame kindle vpon thee.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
For I am the Lord thy God, the holy one of Israel, thy Sauiour: I gaue Egypt for thy ransome, Ethiopia, and Seba for thee.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Because thou wast precious in my sight, and thou wast honourable, and I loued thee, therefore will I giue man for thee, and people for thy sake.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Feare not, for I am with thee: I will bring thy seede from the East, and gather thee from the West.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
I will say to the North, Giue: and to the South, Keepe not backe: bring my sonnes from farre, and my daughters from the ends of the earth.
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
Euery one shall be called by my Name: for I created him for my glorie, formed him and made him.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
I will bring foorth the blinde people, and they shall haue eyes, and the deafe, and they shall haue eares.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
Let all the nations be gathered together, and let the people be assembled: who among them can declare this and shewe vs former things? let them bring foorth their witnesses, that they may be iustified: but let them heare, and say, It is truth.
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
You are my witnesses, saith the Lord, and my seruant, whom I haue chosen: therefore yee shall knowe and beleeue me and yee shall vnderstand that I am: before me there was no God formed, neither shall there be after me.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
I, euen I am the Lord, and beside me there is no Sauiour.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
I haue declared, and I haue saued, and I haue shewed, when there was no strange god among you: therefore you are my witnesses, sayeth the Lord, that I am God.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
Yea, before the day was, I am, and there is none that can deliuer out of mine hand: I will doe it, and who shall let it?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Thus sayeth the Lord your redeemer, the holy one of Israel, For your sake I haue sent to Babel, and brought it downe: they are all fugitiues, and the Chaldeans crie in the shippes.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
I am the Lord your holy one, the creator of Israel, your King.
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Thus sayeth the Lord which maketh a way in the Sea, and a path in the mighty waters.
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
When hee bringeth out the charet and horse, the armie and the power lie together, and shall not rise: they are extinct, and quenched as towe.
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Remember yee not the former things, neither regard the things of olde.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Behold, I do a new thing: now shall it come foorth: shall you not knowe it? I wil euen make a way in the desert, and floods in the wildernesse.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
The wilde beastes shall honour mee, the dragons and the ostriches, because I gaue water in the desert, and floods in the wildernesse to giue drinke to my people, euen to mine elect.
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
This people haue I formed for my selfe: they shall shewe foorth my praise.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
And thou hast not called vpon mee, O Iaakob, but thou hast wearied me, O Israel.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Thou hast not brought me the sheepe of thy burnt offrings, neither hast thou honoured me with thy sacrifices. I haue not caused thee to serue with an offring, nor wearied thee with incense.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Thou boughtest mee no sweete sauour with money, neither hast thou made mee drunke with the fatte of thy sacrifices, but thou hast made mee to serue with thy sinnes, and wearied mee with thine iniquities.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
I, euen I am he that putteth away thine iniquities for mine owne sake, and will not remember thy sinnes.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Put me in remembrance: let vs be iudged together: count thou that thou maist be iustified.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Thy first father hath sinned, and thy teachers haue transgressed against me.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
Therefore I haue prophaned the rulers of the Sanctuarie, and haue made Iaakob a curse, and Israel a reproche.