< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
And now thus saith the Lord that created thee, O Jacob, and formed thee, O Israel: Fear not, for I have redeemed thee, and called thee by thy name: thou art mine.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
When thou shalt pass through the waters, I will be with thee, and the rivers shall not cover thee: when thou shalt walk in the fire, thou shalt not be burnt, and the flames shall not burn in thee:
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
For I am the Lord thy God, the Holy One of Israel, thy Saviour: I have given Egypt for thy atonement, Ethiopia and Saba for thee.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Since thou becamest honourable in my eyes, thou art glorious: I have loved thee, and I will give men for thee, and people for thy life.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Fear not, for I am with thee: I will. bring thy seed from the east, and gather thee from the west.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
I will say to the north: Give up: and to the south: Keep not back: bring my sons from afar, and my daughters from the ends of the earth.
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
And every one that calleth upon my name, I have created him for my glory, I have formed him, and made him.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Bring forth the people that are blind, and have eyes: that are deaf, and have ears.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
All the nations are assembled together, and the tribes are gathered: who among you can declare this, and shall make us hear the former things? let them bring forth their witnesses, let them be justified, and hear, and say: It is truth.
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
You are my witnesses, saith the Lord, and my servant whom I have chosen: that you may know, and believe me, and understand that I myself am. Before me there was no God formed, and after me there shall be none.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
I am, I am the Lord: and there is no saviour besides me.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
I have declared, and have saved. I have made it heard, and there was no strange one among you. You are my witnesses, saith the Lord, and I am God.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
And from the beginning I am the same, and there is none that can deliver out of my hand: I will work, and who shall turn it away?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Thus saith the Lord your redeemer, the Holy One of Israel: For your sake I sent to Babylon, and have brought down all their bars, and the Chaldeans glorying in their ships.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
I am the Lord your Holy One, the Creator of Israel, your King.
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Thus saith the Lord, who made a way in the sea, and a path in the mighty waters.
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
Who brought forth the chariot and the horse, the army and the strong: they lay down to sleep together, and they shall not rise again: they are broken as flax, and are extinct.
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Remember not former things, and look not on things of old.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Behold I do new things, and now they shall spring forth, verily you shall know them: I will make a way in the wilderness, and rivers in the desert.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
The beast of the field shall glorify me, the dragons and the ostriches: because I have given waters in the wilderness, rivers in the desert, to give drink to my people, to my chosen.
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
This people have I formed for myself, they shall shew forth my praise.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
But thou hast not called upon me, O Jacob, neither hast thou laboured about me, O Israel.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Thou hast not offered me the ram of thy holocaust, nor hast thou glorified me with thy victims: I have not caused thee to serve with oblations, nor wearied thee with incense.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Thou hast bought me no sweet cane with money, neither hast thou filled me with the fat of thy victims. But thou hast made me to serve with thy sins, thou hast wearied me with thy iniquities.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
I am, I am he that blot out thy iniquities for my own sake, and I will not remember thy sins.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Put me in remembrance, and let us plead together: tell if thou hast any thing to justify thyself.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Thy brat father sinned, and thy teachers have transgressed against me.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
And I have profaned the holy princes, I have given Jacob to slaughter, and Israel to reproach.

< Isaya 43 >