< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
And now thus says the Lord who created you, O Jacob, and who formed you, O Israel: Do not be afraid. For I have redeemed you, and I have called you by your name. You are mine.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
When you pass through the waters, I will be with you, and the rivers will not cover you. When you walk through fire, you will not be burned, and the flames will not scorch you.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
For I am the Lord your God, the Holy One of Israel, your Savior. I have presented Egypt as your atonement, Ethiopia and Seba on your behalf.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Since then, you have become honorable in my eyes, and glorious. I have loved you, and I will present men on behalf of you, and people on behalf of your life.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Fear not, for I am with you. I will lead your offspring from the East, and I will gather you from the West.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
I will say to the North, “Release him,” and to the South, “Do not turn him away.” Bring my sons from far away, and my daughters from the ends of the earth.
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
And each one who calls upon my name, I have created for my glory. I have formed him, and I have made him.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Lead forth the people who are blind and have eyes, who are deaf and have ears.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
All the nations have been assembled together, and the tribes have been collected. Who among you will announce this, and who will cause us to listen to the things that are first? Let them present their witnesses. Let them act justly, and listen, and say: “It is true.”
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
You are my witnesses, says the Lord, and you are my servant, whom I have chosen, so that you may know, and may believe in me, and so that you may understand that I am the same. Before me, there was no god formed, and after me there will be none.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
I am. I am the Lord. And there is no savior apart from me.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
I have announced, and I have saved. I have caused it to be heard. And there was no stranger among you. You are my witnesses, says the Lord, and I am God.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
And from the beginning, I am the same. And there is no one who can rescue from my hand. I act, and who can turn it aside?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Thus says the Lord, your Redeemer, the Holy One of Israel: For your sake, I sent to Babylon, and tore down all their bars, with the Chaldeans who glory in their ships.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
I am the Lord, your Holy One, the Creator of Israel, your King.
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Thus says the Lord, who gave you a way through the sea and a path through the torrent of waters,
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
who led out the chariot and the horse, the column of robust troops. They went to sleep together, and they will not arise. They have been crushed like flax, and they have been extinguished.
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
You need not call to mind the past, nor consider the things of antiquity.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Behold, I am accomplishing new things. And presently, they will spring forth. With certainty, you will know them. I will make a way in the desert, and rivers in an impassible place.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
The wild beasts of the field will glorify me, with the serpents and the ostriches. For I have brought waters to the desert, rivers to inaccessible places, in order to give drink to my people, to my elect.
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
This is the people whom I have formed for myself. They will speak my praise.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
But you have not called upon me, O Jacob, nor have you struggled for me, O Israel.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
You have not offered me the ram of your holocaust, and you have not glorified me with your victims. I have not burdened you with oblations, nor have I wearied you with incense.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
You have bought me no sweet cane with money, and you have not inebriated me with the fat of your victims. Yet truly, you have burdened me with your sins; you have wearied me with your iniquities.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
I am. I am the very One who wipes away your iniquities for my own sake. And I will not remember your sins.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Call me to mind, and let us go to judgment together. If you have anything to justify yourself, explain it.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Your first father sinned, and your interpreters have betrayed me.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
And so, I have defiled the holy leaders. I have handed over Jacob to slaughter, and Israel to calumny.

< Isaya 43 >