< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
But now thus says Jehovah who created thee, O Jacob, and he who formed thee, O Israel: Fear not, for I have redeemed thee. I have called thee by thy name, Thou are mine.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
When thou pass through the waters, I will be with thee, and through the rivers, they shall not overflow thee. When thou walk through the fire, thou shall not be burned, nor shall the flame kindle upon thee.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
For I am Jehovah thy God, the Holy One of Israel, thy Savior. I have given Egypt as thy ransom, Ethiopia and Seba in thy stead.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
Since thou have been precious in my sight, and honorable, and I have loved thee, therefore I will give men in thy stead, and peoples instead of thy life.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
Fear not, for I am with thee. I will bring thy seed from the east, and gather thee from the west.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
I will say to the north, Give up, and to the south, Keep not back. Bring my sons from far, and my daughters from the end of the earth,
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
everyone who is called by my name, and whom I have created for my glory, whom I have formed, yea, whom I have made.
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
Bring forth the blind people who have eyes, and the deaf who have ears.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
Let all the nations be gathered together, and let the peoples be assembled. Who among them can declare this, and show us former things? Let them bring their witnesses that they may be justified, or let them hear, and say, It is truth.
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
Ye are my witnesses, says Jehovah, and my servant whom I have chosen, that ye may know and believe me, and understand that I am he. Before me there was no God formed, nor shall there be after me.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
I, even I, am Jehovah, and besides me there is no savior.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
I have declared, and I have saved, and I have shown, and there was no strange god among you. Therefore ye are my witnesses, says Jehovah, and I am God.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
Yea, since the day was I am he, and there is none that can deliver out of my hand. I will work, and who can hinder it?
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
Thus says Jehovah, your Redeemer, the Holy One of Israel: For your sake I have sent to Babylon, and I will bring down all of them as fugitives, even the Chaldeans, in the ships of their rejoicing.
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
I am Jehovah, your Holy One, the Creator of Israel, your King.
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
Thus says Jehovah, who makes a way in the sea, and a path in the mighty waters,
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
who brings forth the chariot and horse, the army and the mighty man (they lie down together; they shall not rise; they are extinct; they are quenched as a wick):
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
Do not remember ye the former things, nor consider the things of old.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
Behold, I will do a new thing. Now it shall spring forth. Shall ye not know it? I will even make a way in the wilderness, and rivers in the desert.
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
The beasts of the field shall honor me, the jackals and the ostriches, because I give waters in the wilderness, and rivers in the desert, to give drink to my people, my chosen,
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
the people whom I formed for myself, that they might set forth my praise.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
Yet thou have not called upon me, O Jacob, but thou have been weary of me, O Israel.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
Thou have not brought me from thy sheep for burnt offerings, nor have thou honored me with thy sacrifices. I have not burdened thee with offerings, nor wearied thee with frankincense.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
Thou have bought me no sweet cane with money, nor have thou filled me with the fat of thy sacrifices. But thou have burdened me with thy sins. Thou have wearied me with thine iniquities.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
I, even I, am he who blots out thy transgressions for my own sake, and I will not remember thy sins.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
Put me in remembrance. Let us plead together. Set thou forth thy case that thou may be justified.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
Thy first father sinned, and thy teachers have transgressed against me.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
Therefore I will profane the rulers of the sanctuary, and I will make Jacob a curse, and Israel a reviling.

< Isaya 43 >