< Isaya 43 >

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
但是現今,雅各伯啊!那創造你的,以色列啊!那形成你的上主這樣說:「你不要害怕!因為我救贖了你,我以你的名子召叫了你,你是我的。
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
當你由水中經過時,我必與你在一起;當你渡河時,河水不得淹沒你;當你在火中走過時,你不致烙傷,火燄也燒不著你。
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
因為我是上主,你的天主;以色列的聖者,你的救主;我使埃及作你的贖價,以雇士和色巴來代替你。
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
因為你在我眼中是寶貴的,是貴重的,我愛慕你;所以我拿別人交換了你,拿別的民族交換了你的性命。
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
不要害怕!因為我同你在一起,我要從東方領回你的子女,從西方將你召集在一起;
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
我要向北方說:「交出來!」向南方說:「不要攔阻他們,要將我的兒子們從遠方帶來,要將我的女兒們由地極領回,
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
就是凡歸於我名下,並為了我的光榮而創造、形成和造化的人。」
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
領那有眼而瞎,有耳而聾的民族出來罷!
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
讓列國聚在一起,萬民集合起來!他們中誰能預言這事呢﹖誰能預先報告給我們過去的事呢﹖讓他們找出證人來,為證實自己有理,好讓聽眾能說:「對啊! 」
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
你們就是我的證人--上主的斷語--你們是我揀選的僕人,為叫你們認識和信仰我,並明白我就是「那位;」在我以前,沒有受造的神,在我以後,也決不會有。
11 Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
我,只有我是上主,我以外沒有救主;
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
是我預言了,是我施行了拯救,是我宣佈過的;你們中沒有別的神。你們是我的證人--上主的斷語--我是天主,
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
且由永遠就是;沒有人能從我手中救出誰來;我要做的,誰能扭轉﹖
14 Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
上主,你們的救主,以色列的聖者這樣說:「為了你們,我派了人到巴比倫去,我要打斷一切門閂,將加色丁人的狂歡變為悲哀。
15 Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
我是上主,你們的聖者,以色列的造主,你們的君王。」
16 Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
上主這樣說:--他曾在海中開了一條路,在怒潮中闢了一條道;
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
曾使車、馬、軍隊和將領一同前來,使他們沉沒,再未浮起,他們遂被消滅,像燈心一樣被熄滅--「
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
你們不必追念古代的事,也不必回憶過去的事!
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
看哪!我要行一件新事,如今即要發生,你們不知道嗎﹖看哪!我要在荒野中開闢道路,在沙漠裏開掘河流。
20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
田野間的走獸、豺狼和鴕鳥都要讚美我,因為我在曠野中使水湧出,在沙漠裏使河流成渠,為賜給我揀選的百姓喝:
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
就是我為自己所造化的人民,好叫他們講述我的榮耀。」「
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
但是,雅各伯啊!你並沒有呼號我;以色列啊!你竟厭煩了我。
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
你沒有獻給我全燔祭羔羊,也沒有用你的犧牲光榮我;我從來沒有因了素祭而勞累你,也沒有因了馨香祭而煩擾你。
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
你不但沒有花錢給我買香蒲,也沒有以你犧牲的肥脂供養我,反而用你的罪惡勞累了我,以你的愆尤煩擾了我。
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
是我,是我自己,為了我自己的緣故,免除了你的過犯,不再懷念你的罪惡。
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
請你提醒我,讓我們一起來辯論:你先說罷!好表示你無罪。
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
你的祖先犯了罪,你的中保背叛了我!
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
為此,我使你的聖君受了褻瀆,使雅各伯遭受了毀滅,使以色列遭到了恥辱。」

< Isaya 43 >