< Isaya 41 >

1 “Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
Mianjiña, hijanjiña’ areo ahy, ry tokonoseo, ampaozareñe ondatio; hañarinea’ iareo mb’etoy, hisaontsy; Antao hototoke mb’eo hitsarañe.
2 “Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
Ia ty nampitsekake i boak’ atiñanañey hitroara’e an-kavañonañe? Ie apo’e aolo’e ey o kilakila ondatio naho ampiambanè’e o mpanjakao? Idemohe’ i fibara’ey ho deboke, ahofahofa i fale’ey hoe t’ie kafo’e.
3 Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
Niheañe’e iereo, nirefe tsy an-joy; an-dalañe mbe lia tsy niliam-pandia’e.
4 Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
Ia ty nitsakore vaho nahatafetetse? Ie nikanjy o tarira­tseo am’baloha’e añe. Izaho Iehovà, ty valoha’e, vaho ty fara’e, Ie iRaho.
5 Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
Nañeveñe o tokonoseo te nahaoniñe; nihondrahondra o olon-taneo; nitotoke iereo vaho nimb’atoy.
6 kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
Mifañimba o mpifankarineo, songa manao aman-drahalahi’e: Mihaozara.
7 Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
Aa le hafatrare’ i mpandranjiy ty mpitsene volamena, risihe’ i mpamañe añ’ana-batoy i mipeke renem-batoy; le ata’e ty hoe i fanodirañey: Soa zao. Rekete’e am-pati-by tsy hitroetroe.
8 “Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
F’ihe Israele, mpitoroko, Iakobe jinoboko, tirin’ Avrahame Rañeko;
9 nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
Ie rinambeko añ’olo’ ty tane toy añe naho nitoka azo an-tsietoitane añe, nanao ty hoe ama’o: Mpitoroko irehe, jinoboko fa tsy nifarieko;
10 Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Ko hemban-drehe, fa indrezako, ko mijilojilo: Izaho ro Andrianañahare’o; le hampaozareko toe hañimb’ azo iraho; Eka, ho tohanako an-tañan-kavanan- kavantàñako.
11 “Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
Toe fonga ho salareñe naho aliheñe ze navaivay ama’o; harotsake o nañatreatre azoo, hafotsake tsy ho vente’e.
12 Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
Ho paia’o fa tsy ho isa’o o nifañotokotok’ ama’oo; ho hakoahañe o nialy ama’oo, vata’e kòake.
13 Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
Amy te Izaho Iehovà Andrianañahare’o ty mikalañe ty fità’o ankavana, hanoako ty hoe: Ko mirevendreven-drehe, Izaho ty hañolotse azo.
14 Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Ko hembañe ry oletse Iakobe, ry ondati’ Israeleo, fa holoreko, hoe t’Iehovà Mpijebañe azo, i Masi’ Israeley.
15 “Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
Ingo rinanjiko ho fandisañan-drehe, reketse nife masioñe; ho lisane’o o vohitseo, ho demohe’o, vaho hanoe’o kafo o tambohoo.
16 Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Ho tsongae’o, le hahofa’ i tiokey mb’eo, naho haboele’ i tangololahiy; naho hirebeha’o ty tahina’ Iehovà, handia-taroba amy Masi’ Israeley.
17 “Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
Mipay rano o rarakeo naho o poi’eo, fe tsy eo, kantañe an-karan-drano’e ty famele’ iareo; izaho Iehovà ty hanoiñe iareo, Tsy haforintseko; izaho Andrianañahare’ Israele.
18 Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
Hanokafako torahañe o haboan-diolioo, naho rano manganahana añivo’ o vavataneo; hanoako sihanake lifo-drano ty fatrambey naho rano ­mipororoake o tane kankañeo.
19 Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
Hapoko an-dratraratra ao ty mendorave naho ty roy, ty akao naho ty olive; hadoko an-diolio ao ty sohihy, reketse ty ­harandranto, vaho ty kobaiñe.
20 ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
Soa t’ie hahaisake naho haharendreke hitsakore naho hitrao-kilala te nanoem-pità’ Iehovà zao, vaho tsinene’ i Masi’ Israeley.
21 Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
Aboaho ty enta’ areo, hoe t’Iehovà; akaro ty filiera’ areo, hoe t’i Mpanjaka’ Iakobe.
22 “Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
Ee t’ie hakare’areo, hitsey ama’ay o hifetsakeo; o raha taoloo, te inoñe? Atalilio hitsakorea’ay, hahafohina’ay ty figadoña’e; he taroño ama’ay o raha ho avio.
23 tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
Itokio o raha mbe hiheo amy añeio, hahafohina’ay t’ie ndrahare; ke anò ty soa, he anò ty raty, hisamba’ay, hitraofa’ay fañeveñañe.
24 Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
Toe tsy manjofake nahareo, koake o sata’ areoo. Avivivioke ty mifale ama’areo.
25 “Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
Fa nitsekafeko i tavaratse añey, le fa pok’eo, boak’ am-panjiriha’ i àndroy añe; ie hitoka ty añarako vaho hivotrak’ amo mpifeheo hoe an-dietse, manahake ty fandialiàm-panao valàñe-tane i lietsey.
26 Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
Ia ty nitsey boak’ am-baloha’e haharendreha’ay: naho haehae añe, hahavolaña’ay t’ie to? Toe tsy amam-mpitaroñe, eka, leo raike tsy mitalily, toe tsy eo ty mahajanjiñe o lañona’oo.
27 Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
Izaho ty valoha’e nañitrik’ amy Tsione ty hoe: Heheke, ingo iereo; vaho hiraheko mb’e Ierosalaime mb’eo ty hinday talily soa.
28 Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
Mañente iraho, fe tsy ama’ ondaty; naho tsy amam-pamere, ie ho nañontaneako hahavalea’e.
29 Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.
Heheke fonga tsy vokatse, tsy jefa’e o sata’ iareoo, toe tioke naho hakoahañe avao o sare fatrana’ iareoo.

< Isaya 41 >