< Isaya 41 >
1 “Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
« Taisez-vous devant moi, îles, et que les peuples renouvellent leur force. Laissez-les s'approcher, alors laissez-les parler. Retrouvons-nous ensemble pour le jugement.
2 “Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
Qui a suscité un homme de l'Orient? Qui l'a rappelé à l'ordre dans la justice? Il lui remet les nations et le fait régner sur les rois. Il les donne comme la poussière à son épée, comme le chaume enfoncé dans son arc.
3 Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
Il les poursuit et passe en toute sécurité, même par un chemin qu'il n'avait pas emprunté avec ses pieds.
4 Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
Qui a travaillé et qui l'a fait, en appelant les générations depuis le début? Moi, Yahvé, le premier et le dernier, c'est moi. »
5 Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
Les îles ont vu, et elles craignent. Les extrémités de la terre tremblent. Ils s'approchent, et viennent.
6 kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
Chacun aide son voisin. Ils disent à leurs frères: « Soyez forts! »
7 Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
Ainsi le charpentier encourage l'orfèvre. Celui qui lisse avec le marteau encourage celui qui frappe l'enclume, disant de la soudure, « C'est bon ». et il le fixe avec des clous, pour qu'il ne chancelle pas.
8 “Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
« Mais toi, Israël, mon serviteur, Jacob que j'ai choisi, la descendance d'Abraham mon ami,
9 nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
vous que j'ai saisis des extrémités de la terre, et appelé depuis ses coins, et t'a dit: « Tu es mon serviteur. Je t'ai choisi et je ne t'ai pas rejeté ».
10 Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
N'ayez pas peur, car je suis avec vous. Ne soyez pas consternés, car je suis votre Dieu. Je vais te renforcer. Oui, je vais vous aider. Oui, je te soutiendrai avec la main droite de ma justice.
11 “Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
Voici que tous ceux qui s'enflamment contre toi seront déçus et confondus. Ceux qui luttent avec toi ne seront rien et périront.
12 Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
Tu les chercheras, et tu ne les trouveras pas, même ceux qui vous contestent. Ceux qui te font la guerre ne seront rien, comme une chose inexistante.
13 Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
Car moi, Yahvé ton Dieu, je tiendrai ta main droite, qui vous dit: « N'ayez pas peur. Je vais vous aider.
14 Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
N'aie pas peur, vermisseau de Jacob, et vous, hommes d'Israël. Je t'aiderai », dit Yahvé. « Votre rédempteur est le Saint d'Israël.
15 “Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
Voici, j'ai fait de toi un nouvel instrument de battage tranchant, avec des dents. Vous allez battre les montagnes, et les battre à petit feu, et rendra les collines semblables à de la paille.
16 Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Tu les vanneras, et le vent les emportera, et le tourbillon les dispersera. Vous vous réjouirez en Yahvé. Tu te glorifieras dans le Saint d'Israël.
17 “Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
Les pauvres et les indigents cherchent de l'eau, et il n'y en a pas. Leur langue manque de soif. Moi, Yahvé, je leur répondrai. Moi, le Dieu d'Israël, je ne les abandonnerai pas.
18 Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
J'ouvrirai des rivières sur les hauteurs dénudées, et des sources au milieu des vallées. Je ferai du désert un bassin d'eau, et la terre sèche des sources d'eau.
19 Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
Je mettrai dans le désert des cèdres, des acacias, des myrtes et des arbres à huile. Je mettrai ensemble des cyprès, des pins et des buis dans le désert;
20 ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
afin qu'ils puissent voir, connaître, considérer et comprendre ensemble, que la main de Yahvé a fait cela, et le Saint d'Israël l'a créé.
21 Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
Produisez votre cause, dit l'Éternel. « Sortez vos fortes raisons! » dit le roi de Jacob.
22 “Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
« Qu'ils nous annoncent et nous déclarent ce qui va arriver! Déclarez les choses passées, ce qu'elles sont, afin que nous puissions les considérer et en connaître la fin; ou nous montrer des choses à venir.
23 tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
Annoncez les choses qui doivent arriver dans l'au-delà, afin que nous sachions que vous êtes des dieux. Oui, fais le bien, ou fais le mal, pour que nous soyons consternés, et le voir ensemble.
24 Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
Voici, vous n'êtes rien, et votre travail n'est rien. Celui qui vous choisit est une abomination.
25 “Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
« J'ai suscité un homme du nord, et il est venu, dès le lever du soleil, celui qui invoque mon nom, et il s'abattra sur les chefs comme sur un mortier, et comme le potier foule l'argile.
26 Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
Qui l'a déclaré dès le commencement, afin que nous le sachions? et avant, pour que nous puissions dire: « Il a raison »? Certes, il n'y a personne qui déclare. Sûrement, il n'y a personne qui montre. Certes, il n'y a personne qui entende tes paroles.
27 Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
Je suis le premier à dire à Sion: « Voici, regarde-les ». et je donnerai à celui qui apporte de bonnes nouvelles à Jérusalem.
28 Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
Quand je regarde, il n'y a pas d'homme, même parmi eux, il n'y a pas de conseiller qui, lorsque je demande, puisse répondre à un mot.
29 Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.
Voici, toutes leurs actions ne sont que vanité et néant. Leurs images en fusion sont le vent et la confusion.