< Isaya 41 >

1 “Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
Iles, be stille to me, and folkis chaunge strengthe; neiye thei, and thanne speke thei; neiye we togidere to doom.
2 “Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
Who reiside the iust man fro the eest, and clepide hym to sue hym silf? He schal yyue folkis in his siyt, and he schal welde kyngis; he schal yyue as dust to his swerd, and as stobil `that is rauyschid of the wynd, to his bowe.
3 Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
He schal pursue hem, he schal go in pees; a path schal not appere in hise feet.
4 Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
Who wrouyte and dide these thingis? clepynge generaciouns at the bigynnyng. Y am the Lord; and Y am the firste and the laste.
5 Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
Ilis sien, and dredden; the laste partis of erthe were astonyed; thei camen niy, and neiyiden.
6 kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
Ech man schal helpe his neiybore, and schal seie to his brother, Be thou coumfortid.
7 Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
A smyth of metal smytynge with an hamer coumfortide him that polischyde, ethir made fair, in that tyme, seiynge, It is good, to glu; and he fastenede hym with nailis, that he schulde not be mouyd.
8 “Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
And thou, Israel, my seruaunte, Jacob, whom Y chees, the seed of Abraham, my frend, in whom Y took thee;
9 nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
fro the laste partis of erthe, and fro the fer partis therof Y clepide thee; and Y seide to thee, Thou art my seruaunt; Y chees thee, and castide not awei thee.
10 Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Drede thou not, for Y am with thee; boowe thou not awei, for Y am thi God. Y coumfortide thee, and helpide thee; and the riythond of my iust man vp took thee.
11 “Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
Lo! alle men schulen be schent, and schulen be aschamed, that fiyten ayens thee; thei schulen be as if thei ben not, and men schulen perische, that ayen seien thee.
12 Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
Thou schalt seke hem, and thou schalt not fynde thi rebel men; thei schulen be, as if thei ben not, and as the wastyng of a man fiytynge ayens thee.
13 Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
For Y am thi Lord God, takynge thin hond, and seiynge to thee, Drede thou not, Y helpide thee.
14 Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Nyle thou, worm of Jacob, drede, ye that ben deed of Israel. Y helpide thee, seith the Lord, and thin ayen biere, the hooli of Israel.
15 “Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
Y haue set thee as a newe wayn threischynge, hauynge sawynge bilis; thou schalt threische mounteyns, and schalt make smal, and thou schalt sette litle hillis as dust.
16 Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Thou schalt wyndewe hem, and the wynd schal take hem awei, and a whirlewynd schal scatere hem; and thou schalt make ful out ioie in the Lord, and thou schalt be glad in the hooli of Israel.
17 “Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
Nedi men and pore seken watris, and tho ben not; the tunge of hem driede for thirst. Y the Lord schal here hem, I God of Israel schal not forsake hem.
18 Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
Y schal opene floodis in hiy hillis, and wellis in the myddis of feeldis; Y schal sette the desert in to poondis of watris, and the lond without weie in to ryuers of watris.
19 Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
Y schal yyue in wildirnesse a cedre, and a thorn, and a myrte tre, and the tre of an olyue; Y schal sette in the desert a fir tre, an elm, and a box tre togidere.
20 ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
That thei se, and knowe, and bithenke, and vndurstonde togidere; that the hond of the Lord dide this thing, and the hooli of Israel made that of nouyt.
21 Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
Make ye niy youre doom, seith the Lord; brynge ye, if in hap ye han ony thing, seith the kyng of Jacob.
22 “Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
Neiy tho, and telle to vs, what euer thingis schulen come; telle ye the formere thingis that weren, and we schulen sette oure herte, and schulen wite; schewe ye to vs the laste thingis of hem, and tho thingis that schulen come.
23 tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
Telle ye what thingis schulen come in tyme to comynge, and we schulen wite, that ye ben goddis; al so do ye wel, ethir yuele, if ye moun; and speke we, and see we togidere.
24 Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
Lo! ye ben of nouyt, and youre werk is of that that is not; he that chees you, is abhomynacioun.
25 “Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
I reiside fro the north, and he schal come fro the risyng of the sunne; he schal clepe my name. And he schal brynge magistratis as cley, and as a pottere defoulynge erthe.
26 Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
Who tolde fro the bigynnyng, that we wite, and fro the bigynnyng, that we seie, Thou art iust? noon is tellynge, nether biforseiynge, nether herynge youre wordis.
27 Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
The firste schal seie to Sion, Lo! Y am present; and Y schal yyue a gospellere to Jerusalem.
28 Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
And Y siy, and noon was of these, that token councel, and he that was axid, answeride a word.
29 Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.
Lo! alle men ben vniust, and her werkis ben wynd and veyn; the symylacris of hem ben wynd, and voide thing.

< Isaya 41 >