< Isaya 41 >
1 “Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
Keep silence before mee, O ylands, and let the people renue their strength: let the come neere, and let them speake: let vs come together into iudgement.
2 “Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
Who raised vp iustice from the East, and called him to his foote? and gaue the nations before him, and subdued the Kings? he gaue them as dust to his sword, and as scattered stubble vnto his bowe.
3 Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
He pursued them, and passed safely by the way that he had not gone with his feete.
4 Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
Who hath wrought and done it? he that calleth the generations from the beginning. I the Lord am the first, and with the last I am ye same.
5 Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
The yles sawe it, and did feare, and the ends of the earth were abashed, drew neere, and came.
6 kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
Euery man helped his neighbour, and saide to his brother, Be strong.
7 Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
So the workeman comforted the founder, and he that smote with ye hammer, him that smote by course, saying, It is ready for the sodering, and he fastened it with nayles that it shoulde not be mooued.
8 “Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
But thou, Israel, art my seruant, and thou Iaakob, whom I haue chosen, the seede of Abraham my friend.
9 nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
For I haue taken thee from the endes of the earth, and called thee before the chiefe thereof, and saide vnto thee, Thou art my seruant: I haue chosen thee, and not cast thee away.
10 Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Feare thou not, for I am with thee: be not afraide, for I am thy God: I will strengthen thee, and helpe thee, and will susteine thee with the right hand of my iustice.
11 “Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
Beholde, all they that prouoke thee, shalbe ashamed, and confounded: they shalbe as nothing, and they that striue with thee, shall perish.
12 Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
Thou shalt seeke them and shalt not finde them: to wit, the men of thy strife, for they shall be as nothing, and the men that warre against thee, as a thing of nought.
13 Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
For I the Lord thy God will hold thy right hand, saying vnto thee, Feare not, I wil helpe thee.
14 Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Feare not, thou worme, Iaakob, and ye men of Israel: I wil helpe thee, sayth the Lord and thy redeemer the holy one of Israel.
15 “Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
Behold, I wil make thee a roller, and a newe threshing instrument hauing teeth: thou shalt thresh the mountaines, and bring them to pouder, and shalt make the hilles as chaffe.
16 Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Thou shalt fanne them, and the winde shall carie them away, and the whirlewinde shall scatter them: and thou shalt reioyce in the Lord, and shalt glory in the holy one of Israel.
17 “Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
When the poore and the needy seeke water, and there is none (their tongue faileth for thirst: I the Lord will heare them: I the God of Israel will not forsake them)
18 Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
I will open riuers in the toppes of the hils, and fountaines in the middes of the valleis: I will make the wildernesse as a poole of water, and the waste land as springs of water.
19 Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
I will set in the wildernesse the cedar, the shittah tree, and the mirre tree, and the pine tree, and I will set in the wildernesse the firre tree, the elme and the boxe tree together.
20 ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
Therefore let them see and knowe, and let them consider and vnderstande together that the hand of the Lord hath done this, and the holy one of Israel hath created it.
21 Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
Stand to your cause, saith the Lord: bring forth your strong reasons, saith ye King of Iaakob.
22 “Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
Let them bring foorth, and let them tell vs what shall come: let them shew the former things what they be, that wee may consider them, and knowe the latter ende of them: either declare vs things for to come.
23 tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
Shewe the things that are to come hereafter, that we may know that you are gods: yea, doe good or doe euill, that we may declare it, and beholde it together.
24 Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
Beholde, ye are of no value, and your making is of naught: man hath chosen an abomination by them.
25 “Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
I haue raised vp from the North, and he shall come: from the East sunne shall he cal vpon my Name, and shall come vpon princes as vpon clay, and as the potter treadeth myre vnder the foote.
26 Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
Who hath declared from the beginning, that we may knowe? or before time, that we may say, He is righteous? Surely there is none that sheweth: surely there is none that declareth: surely there is none that heareth your wordes.
27 Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
I am the first, that saieth to Zion, Beholde, beholde them: and I will giue to Ierusalem one that shall bring good tidings.
28 Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
But when I behelde, there was none, and when I inquired of them, there was no counsellor, and when I demaunded of them, they answered not a woorde.
29 Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.
Beholde, they are all vanitie: their worke is of nothing, their images are wind and confusion.