< Isaya 41 >

1 “Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
Let the islands be silent before me, and let the nations take new strength. Let them draw near, and then speak. Let us apply for judgment together.
2 “Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
Who has raised up a just man from the east, and has called him to follow him? He will place the nations under his gaze, and he will rule over kings. He will cause them to be like dust before his sword, like chaff driven by the wind before his bow.
3 Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
He will pursue them. He will pass by in peace. No trace will appear after his feet.
4 Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
Who has worked and accomplished these things, calling to the generations from the beginning? “It is I, the Lord! I am the first and the last.”
5 Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
The islands saw it and were afraid. The ends of the earth were stupefied. They drew near and arrived.
6 kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
Each one will help his neighbor and will say to his brother, “Be strengthened.”
7 Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
The coppersmith striking with the mallet encouraged him who was forging at that time, saying, “It is ready for soldering.” And he strengthened it with nails, so that it would not be moved.
8 “Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
But you, O Israel, are my servant, O Jacob, whom I have chosen, the offspring of my friend Abraham.
9 nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
For his sake, I have taken you from the ends of the earth, and I have called you from its distant places. And I said to you: “You are my servant. I have chosen you, and I have not cast you aside.”
10 Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Do not be afraid, for I am with you. Do not turn away, for I am your God. I have strengthened you, and I have assisted you, and the right hand of my just one has upheld you.
11 “Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
Behold, all who fight against you shall be confounded and ashamed. They will be as if they did not exist, and the men who contradict you will perish.
12 Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
You will seek them, and you will not find them. The men who rebel against you will be as if they did not exist. And the men who make war against you will be like something that has been consumed.
13 Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
For I am the Lord your God. I take you by your hand, and I say to you: Do not be afraid. I have helped you.
14 Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Fear not, O worm of Jacob, you who are dead within Israel. I have helped you, says the Lord, your Redeemer, the Holy One of Israel.
15 “Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
I have established you like a new threshing cart, having serrated blades. You will thresh the mountains and crush them. And you will turn the hills into chaff.
16 Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
You will winnow them, and the wind will blow them away, and the whirlwind will scatter them. And you shall exult in the Lord; you shall rejoice in the Holy One of Israel.
17 “Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
The indigent and the poor are seeking water, but there is none. Their tongue has been dried up by thirst. I, the Lord, will heed them. I, the God of Israel, will not abandon them.
18 Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
I will open rivers in the high hills, and fountains in the midst of the plains. I will turn the desert into pools of water, and the impassable land into streams of water.
19 Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
I will plant the cedar in a deserted place, with the thorn, and the myrtle, and the olive tree. In the desert, I will plant the pine, and the elm, and the box tree together,
20 ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
so that they may see and know, acknowledge and understand, together, that the hand of the Lord has accomplished this, and that the Holy One of Israel has created it.
21 Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
Bring your case forward, says the Lord. Bring it here, if you have anything to allege, says the King of Jacob.
22 “Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
Let them approach and announce to us the things that will occur. Announce to us the things that were before. And we will apply our heart to them, and we will know their end. And so, reveal to us the things that will occur.
23 tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
Announce the things that will occur in the future, and we will know that you are gods. Likewise, accomplish good or evil, if you are able, and let us speak of it and see it together.
24 Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
Behold, you exist out of nothing, and your work is from what does not exist; he who has chosen you is an abomination.
25 “Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
I have raised up one from the north, and he will arrive from the rising of the sun. He will call upon my name, and he will reduce magistrates to mud, like a potter working with clay.
26 Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
Who has announced this from its rising, so that we may know it, or from its beginning, so that we may say, “You are just.” There is no one who either announces, or predicts, or hears your words.
27 Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
The first one will say to Zion: “Behold, they are here,” and to Jerusalem, “I will present an evangelist.”
28 Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
And I saw, and there was no one among any of them to consult, or who, when I asked, could answer a word.
29 Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.
Behold, they are all unjust, and their works are empty. Their idols are wind and emptiness.

< Isaya 41 >