< Isaya 40 >

1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
“Avutun halkımı” diyor Tanrınız, “Avutun!
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Yeruşalim halkına dokunaklı sözler söyleyin. Angaryanın bittiğini, Suçlarının cezasını ödediklerini, Günahlarının cezasını RAB'bin elinden İki katıyla aldıklarını ilan edin.”
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
Şöyle haykırıyor bir ses: “Çölde RAB'bin yolunu hazırlayın, Bozkırda Tanrımız için düz bir yol açın.
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Her vadi yükseltilecek, Her dağ, her tepe alçaltılacak. Böylelikle engebeler düzleştirilecek, Sarp yerler ovaya dönüştürülecek.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
O zaman RAB'bin yüceliği görünecek, Bütün insanlar hep birlikte onu görecek. Bunu söyleyen RAB'dir.”
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
Ses, “Duyur” diyor. “Neyi duyurayım?” diye soruyorum. “İnsan soyu ota benzer, Bütün vefası kır çiçeği gibidir.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
RAB'bin soluğu esince üzerlerine, Ot kurur, çiçek solar. Gerçekten de halk ottan farksızdır.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
Ot kurur, çiçek solar, Ama Tanrımız'ın sözü sonsuza dek durur.”
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Ey Siyon'a müjde getiren, Yüksek dağa çık! Ey Yeruşalim'e müjde getiren, Yükselt sesini, bağır, Sesini yükselt, korkma. Yahuda kentlerine, “İşte, Tanrınız!” de.
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
İşte Egemen RAB gücüyle geliyor, Kudretiyle egemenlik sürecek. Ücreti kendisiyle birlikte, Ödülü önündedir.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
Sürüsünü çoban gibi güdecek, Kollarına alacak kuzuları, Bağrında taşıyacak; Usul usul yol gösterecek emziklilere.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Kim denizleri avucuyla, Gökleri karışıyla ölçebildi? Yerin toprağını ölçeğe sığdıran, Dağları kantarla, Tepeleri teraziyle tartabilen var mı?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
RAB'bin düşüncesine kim akıl erdirebildi? O'na öğüt verip öğretebilen var mı?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
Akıl almak, adalet yolunu öğrenmek için RAB kime danıştı ki? O'na bilgi veren, anlayış yolunu bildiren var mı?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
RAB için uluslar kovada bir damla su, Terazideki toz zerreciği gibidir. Adaları ince toz gibi tartar.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
Adakları yakmaya yetmez Lübnan ormanı, Yakmalık sunu için az gelir hayvanları.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
RAB'bin önünde bütün uluslar bir hiç gibidir, Hiçten bile aşağı, değersiz sayılır.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
Öyleyse Tanrı'yı kime benzeteceksiniz? Neyle karşılaştıracaksınız O'nu?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Putu döküm işçisi yapar, Kuyumcu altınla kaplar, Gümüş zincirler döker.
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
Böyle bir sunuya gücü yetmeyen yoksul kişi Çürümez bir ağaç parçası seçer. Yerinden kımıldamaz bir put yapsın diye Usta bir işçi arar.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Bilmiyor musunuz, duymadınız mı? Başlangıçtan beri size bildirilmedi mi? Dünyanın temelleri atılalı beri anlamadınız mı?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
Gökkubbenin üstünde oturan RAB'dir, Yeryüzünde yaşayanlarsa çekirge gibidir. Gökleri perde gibi geren, Oturmak için çadır gibi kuran O'dur.
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
O'dur önderleri bir hiç eden, Dünyanın egemenlerini sıfıra indirgeyen.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
O önderler ki, yeni dikilmiş, yeni ekilmiş ağaç gibi, Gövdeleri yere yeni kök salmışken RAB'bin soluğu onları kurutuverir, Kasırga saman gibi savurur.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
“Beni kime benzeteceksiniz ki, Eşitim olsun?” diyor Kutsal Olan.
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Başınızı kaldırıp göklere bakın. Kim yarattı bütün bunları? Yıldızları sırayla görünür kılıyor, Her birini adıyla çağırıyor. Büyük kudreti, üstün gücü sayesinde hepsi yerli yerinde duruyor.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Ey Yakup soyu, ey İsrail! Neden, “RAB başıma gelenleri görmüyor, Tanrı hakkımı gözetmiyor?” diye yakınıyorsun?
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Bilmiyor musun, duymadın mı? Ebedi Tanrı, RAB, bütün dünyayı yaratan, Ne yorulur ne de zayıflar, O'nun bilgisi kavranamaz.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
Yorulanı güçlendirir, Takati olmayanın kudretini artırır.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Gençler bile yorulup zayıf düşer, Yiğitler tökezleyip düşerler.
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
RAB'be umut bağlayanlarsa taze güce kavuşur, Kanat açıp yükselirler kartallar gibi. Koşar ama zayıf düşmez, Yürür ama yorulmazlar.

< Isaya 40 >