< Isaya 40 >
1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
“Conforto, consolo meu povo”, diz seu Deus.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
“Fale confortavelmente com Jerusalém, e chame-a para que sua guerra seja cumprida, que sua iniquidade seja perdoada, que ela tenha recebido da mão de Javé o dobro por todos os seus pecados”.
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
A voz de quem chama, “Prepare o caminho de Yahweh no deserto! Fazer uma rodovia nivelada no deserto para nosso Deus.
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Todo vale deve ser exaltado, e todas as montanhas e colinas devem ser baixadas. O desnível deve ser nivelado, e as asperezas colocam uma planície.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
A glória de Yahweh deve ser revelada, e toda a carne deve vê-lo junto; pois a boca de Iavé o disse”.
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
A voz de quem diz: “Grite!” Um disse: “O que eu devo chorar?”. “Toda a carne é como a grama, e toda sua glória é como a flor do campo.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
A grama murcha, a flor se desvanece, porque o fôlego de Yahweh sopra sobre ele. Certamente, as pessoas são como a grama.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
A grama murcha, a flor se desvanece; mas a palavra de nosso Deus permanece para sempre”.
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Você que conta boas notícias a Zion, suba em uma montanha alta. Vocês que dão boas notícias a Jerusalém, levantem sua voz com força! Levantem-no! Não tenha medo! Diga às cidades de Judá: “Eis o seu Deus!”
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Eis que o Senhor Yahweh virá como um poderoso, e seu braço irá governar por ele. Eis que sua recompensa está com ele, e sua recompensa perante ele.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
Ele alimentará seu rebanho como um pastor. Ele reunirá os cordeiros em seu braço, e carregá-las em seu seio. Ele conduzirá gentilmente aqueles que têm seus filhotes.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Quem mediu as águas no oco de sua mão, e marcou o céu com seu vão, e calculou o pó da terra em uma cesta de medição, e pesou as montanhas em balanças, e as colinas em equilíbrio?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
Que dirigiu o Espírito de Yahweh, ou o ensinou como seu conselheiro?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
Com quem ele se aconselhou, e quem o instruiu, e o ensinou no caminho da justiça, e lhe ensinou conhecimentos, e lhe mostrou o caminho para a compreensão?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Eis que as nações são como uma gota em um balde, e são considerados como um grão de pó sobre um equilíbrio. Eis que ele levanta as ilhas como uma coisinha muito pequena.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
O Líbano não é suficiente para queimar, nem seus animais são suficientes para uma oferta queimada.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
Todas as nações são como nada antes dele. Eles são considerados por ele como menos que nada, e vaidade.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
A quem, então, você vai gostar de Deus? Ou que semelhança você vai comparar com ele?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Um operário lançou uma imagem, e o ourives a reveste com ouro, e funde correntes de prata para ele.
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
Aquele que é demasiado empobrecido para tal oferta escolhe uma árvore que não apodreça. Ele procura um artesão hábil para montar uma imagem esculpida para ele que não será movida.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Você ainda não sabia? Você ainda não ouviu falar? Você não foi avisado desde o início? Você não entendeu desde os fundamentos da terra?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
É ele quem se senta acima do círculo da terra, e seus habitantes são como gafanhotos; que estica os céus como uma cortina, e as espalha como uma tenda para morar dentro,
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
que traz os príncipes ao nada, que torna os juízes da terra sem sentido.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
Eles são pouco plantados. Elas são semeadas dificilmente. Seu estoque quase não se enraizou no solo. Ele apenas sopra neles, e eles murcham, e o redemoinho os leva como restolho.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
“A quem, então, você vai gostar de mim? Quem é meu igual?” diz o Santo.
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Levante os olhos para o alto, e ver quem os criou, que traz à tona seu exército pelo número. Ele os chama a todos pelo nome. pela grandeza de seu poder, e porque ele é forte no poder, não falta nenhuma.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Por que você diz, Jacob, e falar, Israel, “Meu caminho está escondido de Javé”, e a justiça que me é devida é desprezada pelo meu Deus”...
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Você já não sabia? Você ainda não ouviu falar? O Deus eterno, Yahweh, o Criador dos confins do mundo, não desmaia. Ele não está cansado. Seu entendimento é indecifrável.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
Ele dá poder aos fracos. Ele aumenta a força daquele que não tem poder.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Even os jovens desmaiam e ficam cansados, e os jovens caem por completo;
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
mas aqueles que esperam por Yahweh renovarão suas forças. Eles se erguem com asas como águias. Eles correrão, e não se cansarão. Eles caminharão, e não desmaiarão.