< Isaya 40 >
1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
Consolez-vous, mon peuple, consolez-vous, dit votre Dieu.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Parlez au cœur de Jérusalem et appelez-la; parce que sa malice est arrivée au terme, son iniquité a été pardonnée; elle a reçu de la main du Seigneur une double peine pour tous ses péchés.
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
Voici la voix de quelqu’un qui crie dans le désert: Préparez la voie du Seigneur; rendez droits dans la solitude les sentiers de notre Dieu.
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Toute vallée sera comblée, et toute montagne et colline sera abaissée; les chemins tortus seront redressés, et les raboteux deviendront des voies aplanies.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
Et la gloire du Seigneur sera révélée, et toute chair verra en même temps que la bouche du Seigneur a parlé.
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
Voici la voix de quelqu’un qui dit: Crie. Et j’ai dit: Que dirai-je? Toute chair est de l’herbe, et toute sa gloire est comme la fleur du champ.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
L’herbe s’est desséchée, et la fleur est tombée, parce que le souffle du Seigneur a soufflé sur elle. Vraiment l’herbe, c’est le peuple;
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
L’herbe s’est desséchée, et la fleur est tombée; mais la parole de notre Seigneur demeure éternellement.
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Sur une haute montagne, monte, toi qui évangélises Sion; élève avec force ta voix, toi qui évangélises Jérusalem; élève-la, ne crains pas. Dis aux cités de Juda: Voici votre Dieu;
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Voici que le Seigneur Dieu viendra dans sa puissance, et que son bras dominera; voici que sa récompense est avec lui, et que son œuvre est devant lui.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
Comme un pasteur, il paîtra son troupeau, et avec son bras il rassemblera les agneaux, et il les prendra dans son sein, il portera lui-même les brebis pleines.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Qui a mesuré les eaux dans sa poignée, et a pesé les cieux dans la paume de sa main? Qui a soutenu de trois doigts la masse de la terre, et a équilibré les montagnes au poids, et les collines dans la balance?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
Qui a aidé l’esprit du Seigneur? ou qui a été son conseiller et l’a enseigné?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
Avec qui est-il entré en conseil, et qui lui a donné l’intelligence, et lui a enseigné le sentier de la justice, et l’a formé à la science, et lui a montré la voie de la prudence?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Voici que les nations sont réputées comme une goutte coulant d’un seau, comme ce qui donne un mouvement à une balance; voici que les îles sont comme une poussière légère.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
Et le Liban ne suffira pas pour allumer le feu de son autel, et ses animaux ne suffiront pas pour un holocauste.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
Toutes les nations, comme si elles n’étaient pas, ainsi sont-elles devant lui; et elles sont réputées par lui comme le néant et le vide.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
À qui donc avez-vous fait semblable le Seigneur? quelle forme lui donnerez-vous?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Est-ce que l’ouvrier ne jette pas une statue en fonte, ou l’orfèvre ne la forme-t-il pas en or, et l’argenteur ne la recouvre-t-il pas de lames d’argent?
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
Il choisit un bois fort et incorruptible; l’artiste habile cherche comment il placera sa statue, pour qu’elle ne chancelle point.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Est-ce que vous ne savez pas? est-ce que vous n’avez pas entendu? est-ce qu’on ne vous a pas annoncé dès le commencement? est-ce que vous n’avez pas compris les fondements de la terre?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
Est-ce que vous n’avez pas compris qui est celui qui demeure sur le globe de la terre, et ses habitants sont comme des sauterelles; qui a étendu les cieux comme rien, et les a déployés comme un tabernacle qui doit être habité?
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
Qui réduit les scrutateurs des secrets à être comme s’ils n’étaient pas, et a fait des juges de la terre une chose vaine?
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
Et à la vérité leur tronc n’avait été ni planté, ni semé, ni enraciné dans la terre; soudain Dieu a soufflé sur eux et ils se sont desséchés, et un tourbillon les emportera comme la paille.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
Et à qui m’avez-vous assimilé et égalé, dit le saint?
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Levez en haut vos yeux, et voyez qui a créé ces choses; qui fait lever en nombre leur milice, qui les appelle toutes par leur nom; à cause de la grandeur de sa puissance, et de sa force et de sa vertu, pas une seule ne manque.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Pourquoi dis-tu, ô Jacob, et dis-tu, ô Israël: Ma voie a été cachée au Seigneur, et par mon Dieu mon jugement a été mis de côté?
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Est-ce que tu ne sais pas, ou n’as-tu pas appris? Dieu est l’éternel Seigneur qui a créé les limites de la terre; il ne défaudra pas, il ne se fatiguera pas, et l’investigation de sa sagesse n’est pas possible.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
C’est lui qui donne la vigueur l’homme las; et pour ceux qui ne sont pas, il augmente le courage et la force.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Les enfants défaudront, et se fatigueront, et les jeunes hommes tomberont par l’affaiblissement.
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
Mais ceux qui espèrent dans le Seigneur prendront une force nouvelle; ils prendront des ailes comme les aigles, ils courront, et ne se fatigueront pas; ils marcheront et ne défaudront pas.