< Isaya 40 >

1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
Consolez, consolez mon peuple, dit votre Dieu.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Parlez au cœur de Jérusalem, et criez-lui que son temps d’épreuve est fini, que son crime est expié, qu’elle a reçu de la main du Seigneur double peine pour toutes ses fautes.
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
Une voix proclame: "Dans le désert, déblayez la route de l’Eternel; nivelez, dans la campagne aride, une chaussée pour notre Dieu!
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Que toute vallée soit exhaussée, que toute montagne et colline s’abaissent, que les pentes se changent en plaines, les crêtes escarpées en vallons!
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
La gloire du Seigneur va se révéler, et toutes les créatures, ensemble, en seront témoins: c’est la bouche de l’Eternel qui le déclare."
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
Une voix dit: "Proclame!" Et on a répondu: "Que proclamerai-je?" "Toute chair est comme de l’herbe, et toute sa beauté est comme la fleur des champs.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
L’Herbe se dessèche, la fleur se fane, quand l’haleine du Seigneur a soufflé sur elles. Or, le peuple est comme cette herbe.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
L’Herbe se dessèche, la fleur se fane, mais la parole de notre Dieu subsiste à jamais."
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Monte sur une montagne élevée, porteuse de bonnes nouvelles pour Sion, élève ta voix avec force, messagère de Jérusalem! Elève-la sans crainte, annonce aux villes de Juda: "Voici votre Dieu!"
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Oui, voici le Seigneur, l’Eternel, s’avançant en héros, avec son bras triomphant; voici, il apporte son salaire avec lui, et sa rémunération le précède.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
Tel un berger, menant paître son troupeau, recueille les agneaux dans ses bras, les porte dans son sein et conduit avec douceur les mères qui allaitent.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Qui a mesuré les eaux dans le creux de sa main, pris les dimensions du ciel à l’empan? Qui a jaugé la poussière de la terre, pesé au crochet les montagnes, et les coteaux avec une balance?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
Qui a embrassé l’esprit de l’Eternel? Qui a été le conseiller de sa pensée?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
Avec qui a-t-il délibéré pour s’éclairer, pour apprendre la voie de la justice? Qui lui a donné des leçons de sagesse et indiqué le chemin de l’intelligence?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Certes, les nations, à ses yeux, sont comme une goutte tombant du seau, comme un grain de poussière dans la balance; certes, il ballotterait les îles comme des atomes.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
Le Liban ne suffirait pas à nourrir le feu de son autel; ses bêtes ne suffiraient pas à un holocauste.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
Toutes les nations sont comme rien devant lui; il les considère comme le vide et le néant.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
À qui donc pourriez-vous comparer Dieu et quelle image lui donneriez-vous comme pendant?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Une statue est coulée par le fondeur, plaquée d’or par l’orfèvre, qui la garnit encore de chaînettes d’argent.
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
Celui qui est trop pauvre pour une telle offrande choisit un bois incorruptible, puis s’en va chercher un ouvrier habile, pour fabriquer une idole qui ne bronche jamais.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Vous ne savez donc pas! Vous ne comprenez donc pas! Ne vous l’a-t-on pas appris dès l’origine? Ne saisissez-vous pas ce qu’enseignent les fondements de la terre?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
C’Est Lui qui siège au-dessus du globe de la terre, dont les habitants sont pour lui comme des sauterelles; c’est Lui qui déroule les cieux comme une tenture, qui les déploie comme un pavillon, pour sa résidence.
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
C’Est lui qui réduit les princes à néant, qui fait un rien des arbitres du monde.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
À peine sont-ils plantés, à peine sont-ils semés, à peine leur tronc a-t-il pris racine dans le sol, que déjà il souffle sur eux et ils se dessèchent, et un ouragan les emporte comme le chaume.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
"À qui donc m’assimilerez-vous, à qui vais-je ressembler?" dit le Saint.
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Levez les regards vers les cieux et voyez! Qui les a appelés à l’existence? Qui fait défiler leur armée en bon ordre? Tous, il les appelle par leur nom, et telle est sa puissance et son autorité souveraine que pas un ne fait défaut.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Pourquoi dis-tu, ô Jacob, t’écries-tu, ô Israël: "Ma voie est inconnue à l’Eternel, mon droit échappe à mon Dieu?"
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Ne le sais-tu donc pas? Ne l’as-tu pas ouï dire? Le Seigneur est le Dieu de l’Eternité, le Créateur des dernières limites du monde; il n’éprouve ni fatigue, ni lassitude: il n’est point de bornes à son intelligence!
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
Il redonne la vigueur au courbaturé et double le courage de celui qui est à bout de forces.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Que les adolescents soient las et harassés, que les jeunes gens tombent en défaillance!
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
Ceux qui mettent leur espoir en Dieu acquièrent de nouvelles forces, ils prennent le rapide essor des aigles; ils courent et ne sont pas fatigués, ils vont et ne se lassent point.

< Isaya 40 >