< Isaya 40 >

1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
« Consolez, consolez mon peuple, dit votre Dieu.
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
« Parle avec réconfort à Jérusalem, et crie-lui que son combat est accompli, que son iniquité est pardonnée, qu'elle a reçu de la main de Yahvé le double de tous ses péchés. »
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
La voix de celui qui crie, « Préparez le chemin de Yahvé dans le désert! Faites une route plate dans le désert pour notre Dieu.
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Toute vallée sera exaltée, et toute montagne et toute colline seront abaissées. Le sol doit être nivelé, et les endroits rugueux une plaine.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
La gloire de Yahvé sera révélée, et toute chair le verra ensemble; car la bouche de Yahvé l'a dit. »
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
La voix de quelqu'un qui dit: « Crie! » L'un d'eux a dit: « Que dois-je pleurer? » « Toute chair est comme l'herbe, et toute sa gloire est comme la fleur des champs.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
L'herbe se fane, la fleur se fane, parce que le souffle de Yahvé souffle dessus. Les gens sont sûrement comme de l'herbe.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
L'herbe se fane, la fleur se fane; mais la parole de notre Dieu est éternelle. »
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
Vous qui annoncez de bonnes nouvelles à Sion, montez sur une haute montagne. Vous qui annoncez la bonne nouvelle à Jérusalem, élevez votre voix avec force! Soulevez-le! N'ayez pas peur! Dis aux villes de Juda: « Voici votre Dieu! »
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Voici, le Seigneur Yahvé viendra comme un puissant, et son bras gouvernera pour lui. Voici, sa récompense est avec lui, et sa récompense devant lui.
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
Il fera paître son troupeau comme un berger. Il rassemblera les agneaux dans son bras, et les porter dans son sein. Il conduira doucement ceux qui ont leurs petits.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
Qui a mesuré les eaux dans le creux de sa main, et a marqué le ciel de son empreinte, et a calculé la poussière de la terre dans un panier à mesurer, et a pesé les montagnes dans une balance, et les collines en équilibre?
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
qui a dirigé l'Esprit de Yahvé, ou l'a enseigné en tant que conseiller?
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
Avec qui a-t-il pris conseil? et qui l'a instruit, et lui a enseigné le chemin de la justice, et lui a enseigné la connaissance, et lui a montré le chemin de la compréhension?
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
Voici, les nations sont comme une goutte d'eau dans un seau, et sont considérés comme un grain de poussière sur une balance. Voici qu'il soulève les îles comme une toute petite chose.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
Liban n'est pas suffisant pour brûler, ni ses animaux suffisants pour un holocauste.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
Toutes les nations ne sont rien devant lui. Ils sont considérés par lui comme des moins que rien, et de la vanité.
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
A qui donc comparerez-vous Dieu? Ou quelle ressemblance lui ferez-vous?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Un ouvrier a coulé une image, et l'orfèvre le recouvre d'or, et jette des chaînes en argent pour lui.
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
Celui qui est trop pauvre pour une telle offrande choisit un arbre qui ne pourrit pas. Il cherche un ouvrier habile pour lui ériger une image sculptée qui ne sera pas déplacée.
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Vous ne le saviez pas? Tu n'as pas entendu? Ne vous a-t-on pas dit depuis le début? N'avez-vous pas compris depuis les fondations de la terre?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
C'est lui qui est assis au-dessus du cercle de la terre, et ses habitants sont comme des sauterelles; qui étend les cieux comme un rideau, et les déploie comme une tente pour y habiter,
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
qui réduit les princes à néant, qui rend les juges de la terre insignifiants.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
Ils sont à peine plantés. Ils sont peu semés. Leur stock a à peine pris racine dans le sol. Il souffle simplement sur eux, et ils se fanent, et le tourbillon les emporte comme du chaume.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
« A qui donc me comparerez-vous? Qui est mon égal? » dit le Saint.
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Lève tes yeux en haut, et voir qui les a créés, qui fait sortir son armée par numéro. Il les appelle tous par leur nom. par la grandeur de sa puissance, et parce qu'il est fort en puissance, pas un ne manque.
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
Pourquoi dis-tu, Jacob, et parle, Israël, « Mon chemin est caché de Yahvé, et la justice qui m'est due est méprisée par mon Dieu? »
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Vous ne savez pas? Tu n'as pas entendu? Le Dieu éternel, Yahvé, le Créateur des extrémités de la terre, ne s'évanouit pas. Il n'est pas fatigué. Son intelligence est insondable.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
Il donne du pouvoir aux faibles. Il augmente la force de celui qui n'a pas de force.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Même les jeunes gens se fatiguent et se lassent, et les jeunes hommes tombent complètement;
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
mais ceux qui espèrent en Yahvé renouvelleront leur force. Ils s'élèveront avec des ailes comme des aigles. Ils courront, et ne se lasseront pas. Ils marcheront, et ne s'évanouiront pas.

< Isaya 40 >