< Isaya 40 >

1 Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
Our God says, “Encourage my people! Encourage them!
2 Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
Speak kindly to [the people of] Jerusalem; tell them that their suffering is ended, and that I have forgiven them for the sins that they have committed; I [SYN] have fully punished them for their sins.”
3 Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
I hear someone who is shouting, “Prepare in the desert a way for Yahweh to come [to you]; make a smooth road for our God (OR, Prepare yourselves to receive Yahweh when he comes, like people make a straight road for an important official [MET]).
4 Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
Fill in the valleys; flatten every hill and every mountain. Make the uneven ground smooth, and make the rough places smooth.
5 Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
[If you do that], it will become known that Yahweh is glorious/great, and all people will realize it at the same time. [Those things will surely happen] because it is Yahweh who has said [MTY] it.”
6 Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
Someone said to me, “Shout!” I replied, “What should I shout?” [He replied], “[Shout that] people are like [SIM] grass; their influence fades as quickly as flowers in the field.
7 Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
Grass withers and flowers dry up when Yahweh causes a hot wind from the desert to blow on them. And people are [MET] like that.
8 Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
The grass withers and the flowers dry up, but what our God promises will last forever.”
9 Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
You [people of] Jerusalem, you have good news to tell to people, so, shout it from the top of a high mountain! Shout it loudly, and do not be afraid! Tell the people in the towns of Judah, “Your God is coming here!”
10 Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
Yahweh your God will be coming with power; he will rule powerfully [MTY]. And when he comes, he will bring with him the people whom he has freed [MET] [from being slaves in Babylonia].
11 Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
He will take care of his people like [SIM] a shepherd takes care of his sheep, and carries the young lambs in his arms. He carries them close to his chest and he gently leads the female sheep that are nursing their young lambs.
12 Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
[There is no one like Yahweh]! (Who else has measured the water in the oceans in the palm of his hand?/No one else has measured the water in the oceans in the palm of his hand!) [RHQ] (Who else has measured the sky with his fingers?/No one else has measured the sky with his fingers!) [RHQ] (Who else knows how much the earth weighs?/No one else knows how much the earth weighs!) [RHQ] (Who else has weighed the mountains and hills on scales?/No one else has weighed the mountains and hills on scales!) [RHQ]
13 Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
And (who else can advise Yahweh’s Spirit?/No one else can advise Yahweh’s Spirit!) [RHQ] (Who can teach him or advise/tell him what he should do?/No one can teach him or advise/tell him what he should do!) [RHQ]
14 Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
(Has Yahweh consulted anyone else to get advice?/Yahweh has certainly not consulted anyone else to get advice!) [RHQ] (Does he need someone to tell him what is right to do and how to act justly?/He certainly does not need someone to tell him what is right to do and how to act justly!) [RHQ]
15 Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
[Yahweh considers that] the nations are [as insignificant as] [MET] one drop from a bucket [full of water]. They are [as insignificant as] dust on scales. He is able to weigh islands [as though they weighed no more than] grains of sand.
16 Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
There would be [not] enough wood from all the trees in Lebanon to make a suitable fire for [sacrificing animals to] him, and there are not enough animals in Lebanon to offer as sacrifices to him.
17 Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
The nations of the world are completely insignificant/unimportant to him; he considers that they are worthless and less than nothing [HYP, DOU].
18 Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
So, to whom can you compare God? What image resembles him?
19 Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
Can you compare him to an idol that is made in a mold, and then is covered with [a thin sheet of] gold and decorated with silver chains?
20 Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
A man who is poor [cannot buy silver or gold for his idol]; [so] he selects a piece of wood that will not rot, and he gives it to a craftsman to carve an idol that will not fall down!
21 Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
Have you(pl) not heard this? Do you not understand it? Are you unable to hear what God said long ago— [messages that he gave] before he created the earth?
22 Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
God sits [on his throne] above the earth, and the people [on the earth] below seem to be [as small] as [SIM] grasshoppers. He spreads out the sky like a curtain; it is like [SIM] a tent for him to live in.
23 Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
He causes kings to have no more power, and he causes the rulers to be worth nothing.
24 Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
They start to rule, like small plants start to grow and form roots; but then [he gets rid of them] as though [MET] they withered when he blew on them, like [SIM] chaff that is blown away by the wind.
25 “Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
The Holy One asks, “To whom will you compare me? Is anyone equal to me?”
26 Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
Look up toward the sky: Consider who [RHQ] created all the stars. [Yahweh created them], and at night he causes them to appear; he calls each one by its name. Because he is extremely powerful [DOU], all of the stars are there [LIT] [when he calls out their names].
27 Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
You people of Israel [DOU], why do you complain that Yahweh does not see the [troubles that you are experiencing]? Why do you say that he does not act fairly toward you?
28 Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
Have you never heard and have you never understood that Yahweh is the everlasting God; he is the one who created the earth, [even the] most distant places on the earth. He never becomes weak or weary, and no one can find out how much he understands.
29 Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
He strengthens [DOU] those who feel weak and tired.
30 Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
Even youths become faint and weary, and young men will fall when they are exhausted.
31 bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.
But those who trust in Yahweh will become strong again; [it will be as though] they will soar/fly high like [SIM] eagles do. They will run [for a long time] and not become weary; they will walk [long distances] and not faint.

< Isaya 40 >